Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mwimbaji Wa Nyimbo Za Injili Kasolo Kumtishia Mwanawe Maisha Na Athari Hasi Za Kumtishia Mtoto

3 min read
Mwimbaji Wa Nyimbo Za Injili Kasolo Kumtishia Mwanawe Maisha Na Athari Hasi Za Kumtishia MtotoMwimbaji Wa Nyimbo Za Injili Kasolo Kumtishia Mwanawe Maisha Na Athari Hasi Za Kumtishia Mtoto

Athari hasi za kumtishia mtoto ni kama vile mtoto kutatizika kuwasiliana na watu wengine, kukosa kujiamini na kujaribu kuwafurahisha wengine.

Athari hasi za kumtishia mtoto ni kama vile mtoto kutatizika kuwasiliana na watu wengine. Katika video iliyovuja mitandao mapema mwezi huu, mwimbaji wa nyimbo za injili Kasolo anaonekana nyumbani mwake akimtetesha na kumtishia mtoto wake wa kike maisha. Katika kisa hiki, mwimbaji alimtaka mtoto wake mdogo kumwelezea kwa nini alikuwa anacheza na chupa ya maji, na asipo angemnyonga.

athari hasi za kumtishia mtoto

Kwa maneno yake, alisikika akisema, "Unacheza aje na kitu ya kunywa maji? Kwanini umevunja mpira ya pesa nyingi hivyo, nikuue?" Mtoto anaonekana akilia kwa nguvu. "Nikunyonge mimi, nikuue? Utavunja tena?" Mtoto anajibu, "Nakupenda baba". Mwimbaji anaonekana akicheka na kutabasamu baada ya kuyasikia maneno haya kutoka kwa mwanawe.

Athari hasi za kumtishia mtoto

Wazazi wengi hasa wa kiafrika wana tamaduni ya kuwatishia watoto. Kulingana na wazazi hawa, kuwatishia watoto kunawasaidia kuwa na nidhamu zaidi. Je, hii ni kweli? Kuwatishia watoto kwa kutumia maneno makali kama, nitakuua, nitakunyonga, nitakufukuza, mimi siyo mzazi wako na kadhalika kuna athari hasi katika saikolojia ya mtoto. Tazama jinsi watoto wanaokua katika mazingira wanapotishiwa kila mara na wazazi wao wanavyoathiriwa.

  1. Kuharibu uhusiano kati ya mama na mzazi

Mtoto anapotishiwa kila mara na mzazi wake, anaanza kuwa na chuki kwake. Anahisi kuwa mzazi wake hamwelewi, huku mzazi akihisi kuwa haheshimiwi. Inageuka kuwa ushindani wa atakayesikizwa wa kwanza. Huenda mtoto akajitenga na mzazi wake kabisa. Hata anapokuwa na tatizo, hawezi kumwambia mzazi wake.

2. Mtoto kudhani ni jukumu lake kumfurahisha mtoto

Katika kisa tulichoangazia hapo mwanzoni, mtoto mchanga tayari anajua kuwa anapaswa kumwambia mzazi wake kuwa anampenda ili asiathibiwe. Hata kama mtoto huyu mara nyingi anahisi kumchukia ama kumwogopa mzazi wake, njia ya kipekee ya kuepuka adhabu ni kwa kumfurahisha. Jambo litakalokuwa na athari hasi kwa saikolojia ya mtoto, kwani atajaribu kufanya hivi kwa watu wote hata walimu na marafiki kuepuka kuwakasirisha. Mwishowe, watu wengi watamtumia isivyofaa.

3. Kuharibu motisha ya mtoto

athari hasi za kumtishia mtoto

Kuna baadhi wazazi wanaowatishia watoto wasipofuzu darasani. Kuwatishia watoto siyo njia sawa ya kuwapa motisha, badala yake, mtoto anakosa motisha, hamu ya kusoma ama kufuzu. Huenda watoto wa aina hii pia wakaanza kukosa kwenda shuleni, kwani wanahisi kuwa juhudi zao masomoni hazithaminiwi. Athari nyingine kwa watoto hawa ni kuanza kuwachukia walimu na kujitenga na watoto wengine shuleni.

4. Kuathiri mawasiliano ya mtoto

Mtoto anapotishiwa mapema maishani mwake, anahisi kuwa mzazi wake hamwelewi. Pia atakuwa na uwoga kuwa huenda chochote atakachokisema kitamkasirisha mzazi wake. Kwa njia hii, mtoto ataepuka kuzungumza na mzazi wake, kuepuka mazungumzo ya mada anazohisi kuwa huenda zikamkasirisha mzazi wake. Mtoto anapokua bila kuzungumza, hatafahamu jinsi ya kujieleza hata anapokuwa mtu mkubwa.

Soma Pia:Wazazi Kuchoka Katika Ulezi, Ishara Na Vyanzo Vyake

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Mwimbaji Wa Nyimbo Za Injili Kasolo Kumtishia Mwanawe Maisha Na Athari Hasi Za Kumtishia Mtoto
Share:
  • Je, Kisukari Kina Athari Zipi Kwa Maisha Yako Ya Kingono?

    Je, Kisukari Kina Athari Zipi Kwa Maisha Yako Ya Kingono?

  • Manufaa Ya Kutumia Kondomu Na Athari Hasi Za Kuzivalia

    Manufaa Ya Kutumia Kondomu Na Athari Hasi Za Kuzivalia

  • Jinsi Ya Kuwa Na Mipaka Yenye Afya Na Wazazi

    Jinsi Ya Kuwa Na Mipaka Yenye Afya Na Wazazi

  • Je, Kisukari Kina Athari Zipi Kwa Maisha Yako Ya Kingono?

    Je, Kisukari Kina Athari Zipi Kwa Maisha Yako Ya Kingono?

  • Manufaa Ya Kutumia Kondomu Na Athari Hasi Za Kuzivalia

    Manufaa Ya Kutumia Kondomu Na Athari Hasi Za Kuzivalia

  • Jinsi Ya Kuwa Na Mipaka Yenye Afya Na Wazazi

    Jinsi Ya Kuwa Na Mipaka Yenye Afya Na Wazazi

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it