Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Athari 5 Hasi za Sukari Kwenye Afya

3 min read
Athari 5 Hasi za Sukari Kwenye AfyaAthari 5 Hasi za Sukari Kwenye Afya

Athari hasi za sukari nyingi kwenye afya ni kama vile kukuweka katika hatari ya kuugua magonjwa kama ugonjwa wa moyo, figo na saratani.

Kulingana na mwongozo wa lishe wa Umarekani, watu hula vijiko 16 vya sukari ya kuongeza kila siku. Athari hasi za sukari mwilini ni kama vile kukuweka katika hatari ya kuugua magonjwa kama ugonjwa wa moyo, figo na saratani.

Unapaswa kula kiwango cha sukari kilicho chini ya asilimia 10 ya kalori unazochukua kwa siku. Ikiwa unachukua kalori 1,000 kwa siku, sukari unayoila siku hiyo inapaswa kuwa 100.

Ishara kuwa unakula sukari nyingi

athari hasi za sukari

Kukosa furaha. Kulingana na utafiti, watu wanaokula sukari nyingi huwa na nafasi za juu kukwazwa kimawazo na mhemko wa hisia.

Kufura tumbo. Aina fulani za sukari husababisha gesi kujaa tumboni na kufura tumbo kunako ambatana na matatizo ya mengi ya mfumo wa kuchakata chakula.

Viwango vya chini vya nishati. Lisaa limoja baada ya kula sukari, utahisi  uchovu mwingi.

Athari hasi za sukari nyingi mwilini

1.Ongezeko la uzito wa mwili

Kula sukari nyingi kwenye chakula na vinywaji na sukari za kuongeza kunahusishwa na ongezeko la uzito. Vinywaji kama vile sharubati, soda, chai na kahawa. Kula na kunywa vinywaji vyenye sukari hukufanya uhisi njaa baada ya muda mfupi na kutamani vyakula zaidi vyenye sukari. Kula chakula kingi na hasa chenye sukari kunaongeza kalori zaidi mwilini na kuchangia katika ongezeko la uzani wa mwili.

2. Kusababisha chunusi kwenye uso

Lishe yenye wanga, kalori na sukari nyingi zimehusishwa na kuongeza hatari ya kupata chunusi kwenye uso. Vyakula vyenye sukari huongeza sukari kwenye damu na kuongeza utoaji wa ufuta, unaosababisha chunusi kutokea. Lishe isiyo na vyakula vingi vya kuchakatwa hulinda dhidi ya chunusi kutokea.

3. Kuongeza hatari za ugonjwa wa moyo

Vyakula vyenye sukari nyingi vimehusishwa na kuongeza hatari ya magonjwa kama vile ya moyo yanayosababisha vifo vingi. Kula chakula chenye sukari husababisha ongezeko la uzani na uzani wa kupindukia ama obesity, sukari ya damu na shinikizo la damu. Magonjwa haya huongeza hatari ya kuugua ugonjwa wa moyo.

 4. Hatari ya kuugua saratani

Kula sukari nyingi kunaongeza hatari ya kuugua aina fulani za saratani.

Vyakula vyenye sukari nyingi husababisha ongezeko la kupindukia la uzito na kuongeza hatari ya saratani. Lishe zenye sukari nyingi husababisha kuvimbiwa na kupunguza kiwango cha insulin kinachotelewa mwilini. Zote ambazo zinaongeza hatari ya kuugua saratani.

5. Ngozi kuzeeka kwa kasi

Kupata makunyanzi huwa dhibiti asili ya kuzeeka. Unavyozidi kuzeeka, ndivyo yanavyozidi kutokea mwilini. Walakini, kula chakula duni na hasa chenye sukari nyingi kunaongeza mchakato huu kufanyika kwa kasi. Ngozi inazeeka mapema kabla ya muda.

Mbali na athari tulizo angazia, ulaji mwingi wa sukari husababisha ugonjwa wa figo, afya ya meno kudidimia na kuathiri afya ya kiakili.

Jinsi ya kupunguza kiwango cha sukari

athari hasi za sukari

  • Kunywa maji na vinywaji vyenye afya ikilinganishwa na kunywa soda na sharubati.
  • Kunywa kahawa bila kuongeza sukari
  • Kula matunda na sharubati za matunda freshi ikilinganishwa na sharubati za kununua
  • Tupilia mbali unywaji wa pombe

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Manufaa 7 ya Tufaha za Kijani Kwa Afya na Urembo

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Athari 5 Hasi za Sukari Kwenye Afya
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it