Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Athari Hasi za Kutumia Uzazi wa Mpango Kwa Wanawake

2 min read
Athari Hasi za Kutumia Uzazi wa Mpango Kwa WanawakeAthari Hasi za Kutumia Uzazi wa Mpango Kwa Wanawake

Athari hasi za uzazi wa mpango kwa mwanamke ni kama vile kuathiri kipindi chake cha hedhi, kusababisha maumivu ya kichwa na kuongeza uzito.

Kuna njia tofauti za uzazi wa mpango zinazolinda dhidi ya kupata mimba. Baadhi ya njia hizi ni kama vile kutumia tembe, kondomu ama IUD. Tembe inalinda dhidi ya kupata mimba kwa kuufanya mwili usitoe yai. Manii yanapoingia mwilini mwa mwanamke, hakuna yai la kurutubisha na mimba haiwezi fanyika. Kondomu kama njia ya kupanga uzazi haina athari hasi inapotumika ipasavyo. Tuna angazia athari hasi za uzazi wa mpango.

Mbinu za kupanga uzazi huwa na homoni za estrogen ama progesterone ama zote mbili. Homoni hivi zinaweza kuathiri mwanamke na kumfanya ahisi uchungu mwingi wakati wa hedhi, apate chunusi ama kuwa na vipindi vizito vya hedhi.

Athari Hasi za Uzazi wa Mpango

Tembe za kupanga uzazi huathiri viwango vya homoni mwilini na kuathiri utendaji kazi wa kawaida wa mwili.

  1. Kuhisi kichefuchefu

athari za uzazi wa mpango

Baadhi ya wanawake huhisi kichefuchefu baada ya kuchukua tembe lakini hisia hizi hupunguka baada ya muda. Tembe za uzazi wa mpango hazipaswi kuwafanya wanawake wagonjeke, ni muhimu kuwasiliana na daktari hali ya kuhisi kichefuchefu isipopungua.

2. Kuvunja damu

athari za uzazi wa mpango

Kuvunja damu katikati ya vipindi vya hedhi huwa mojawapo ya athari hasi za uzazi wa mpango. Kuvunja damu husababishwa na mabadiliko ya viwango vya homoni mwilini. Hali hii ikiendelea kwa zaidi ya miezi mitatu, hakikisha kuwa unarudi hospitalini.

3. Ongezeko la uzani

athari za uzazi wa mpango

Wanawake wengi hutatizika kutokana na ongezeko la uzani wanapotumia IUD ya uzazi wa mpango. Huku wanawake wengine wakidhibitishwa kupoteza uzani wanapotumia tembe za kupanga uzazi.

4. Maumivu ya kichwa

athari za uzazi wa mpango

Tembe zinazotumika kupanga uzazi zinaongezeka maumivu ya kichwa. Mabadiliko ya homoni za kingono za progesterone na estrogen husababisha maumivu ya kichwa.

5. Kukosa kipindi cha hedhi

kukosa hedhi na tumbo kuuma

Kutumia uzazi wa mpango huathiri vipindi vya hedhi, na kuvifanya viwe vizito ama vyepesi. Miezi ya kwanza michache baada ya kuwekwa IUD, huenda mwanamke akakosa kupata vipindi vyake vya hedhi. Iwapo atapata vipindi vya hedhi, huenda vikawa vyepesi ama vizito zaidi.

Mbali na athari za uzazi wa mpango tulizoangazia, mwanamke huenda akawa na hamu ya chini ya kufanya mapenzi na kuwa na maziwa laini kuliko ilivyo kawaida.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Sababu 3 za Kukosa Hedhi Baada ya Kutumia Uzazi wa Mpango

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Athari Hasi za Kutumia Uzazi wa Mpango Kwa Wanawake
Share:
  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it