Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Athari Za Uchovu Wa Ulezi Kwa Wachumba Na Watoto

2 min read
Athari Za Uchovu Wa Ulezi Kwa Wachumba Na WatotoAthari Za Uchovu Wa Ulezi Kwa Wachumba Na Watoto

Wazazi wanaposhuhudia uchovu wa ulezi, wanafikiria kuwa ni kawaida katika ulezi. Na kuhisi lawama wanapotaka kuchukua muda wa kupumzika.

Kama mzazi, unazingatia mahitaji ya familia yako, watoto, bwana, bibi, nyumba na kuhakikisha kuwa mambo yote yako shwari. Wazazi wengi huwa makini na watoto wao na kusahau mahitaji yao na kujipa muda. Na kuwafanya wapate uchovu wa ulezi ambapo wanahisi kuwa wamechoka na hawana nishati ya kuendelea.

Wazazi wengi wanaposhuhudia jambo hili, wanafikiria kuwa ni kawaida katika ulezi. Na kuhisi lawama wanapotaka kuchukua muda wa kupumzika. Pia wana aibu ku wa wataonekana kuwa wao sio wazazi wazuri. Uchovu huu wa ulezi huwa na athari hasi kwenye afya ya kiakili, kihisia na hata kifizikia.

Athari za uchovu wa ulezi

uchovu wa ulezi

Kuchoka katika ulezi humfanya mzazi kuhisi kuchoka wakati wote, kujitenga kihisia na watoto na mchumba, kuwa na lawama na kuhisi kuwa yeye sio mzazi bora. Athari ambazo zina athiri afya kwa ujumla. Mzazi huenda akahisi kuwa anatatizika kufikiria, kufanya uamuzi, kuhisi kuchanganyikiwa, kusombwa na mawazo, kusahau ovyo, kuhisi ako peke yake, ama hata kukosa usingizi.

Kwa wanawake, uchovu wa viwango vya juu huenda ukasababisha mabadiliko ya viwango vya homoni mwilini, kisukari, ugonjwa wa moyo, kukosa usingizi na kukosa hamu ya kufanya mapenzi.

Uhusiano kati ya wachumba utaathiriwa. Ambapo kutakua na matatizo ya mazungumzo, kuto sikizana ama hata kuchukiana.

Mzazi anayetatizika na uchovu wa mzazi atahisi kuwa uhusiano wake na watoto umeathiriwa na kuhisi kuwa kuna umbali kati yao.

Kutatua suala hili

 

  • Kuzungumza

Mara nyingi, huenda mchumba asifahamu kinachoendelea. Kumweleza ni jambo la kwanza ili aweze kusaidia katika majukumu ya kinyumbani na kuwachunga watoto. Msaada wa kihisia ni muhimu kutatua hali hii. Usipomweleza mchumba wako unavyohisi, ni vigumu kwake kukusaidia ama kuelewa yanayokukumba.

  • Fanya mazoezi

uchovu wa ulezi

Mazoezi huboresha utoaji wa vichocheo vya kuhisi vizuri mwilini, na kupunguza mawazo mengi na kusombwa na mawazo. Kufanya mazoezi kunaweza kuwa kuogelea kwa dakika chache kwa siku ama kutembea kwa dakika 20.

  • Usiwe na lawama

Jamii inawasingizia wanawake kuhisi lawama wanapowaacha watoto na kwenda likizo kupumzika. Ukweli ni kuwa, ulezi ni jukumu kubwa na sio jambo jipya mzazi wa kimsingi kuhisi kuwa anazidiwa na majukumu yote aliyotwikwa. Ni muhimu kuchukua mapumziko ya mara kwa mara.

Chanzo : WebMD

Soma Pia: Matatizo Ya Ulezi (Changamoto 3 Kuu Za Ulezi Katika 2021)

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Athari Za Uchovu Wa Ulezi Kwa Wachumba Na Watoto
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it