Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Je, Kupima Mimba Ni Bei Ghali Ama Rahisi?

3 min read
Je, Kupima Mimba Ni Bei Ghali Ama Rahisi?Je, Kupima Mimba Ni Bei Ghali Ama Rahisi?

Muda wa kupima mimba hutofautiana kati ya mwanamke. Hii ni kwa sababu mizunguko ya hedhi hutofautiana kwa wanawake.

Ujauzito huwa jambo la furaha sana kwa wengi, ilihali kwa wengine huwa jambo la kutamausha. Ili kuwa na uhakika juu ya hali yako, ni vyema kuzingatia kipimo cha mimba. Kuna vipimo tofauti vya ujauzito  na pia bei ya kipimo cha mimba hutofautiana kutoka kipimo kimoja hadi kingine. Vingine havina gharama yoyote.

La kwanza, ni kuelewa kipimo cha mimba hufanya nini haswa? Baada ya yai lilorutubishwa kujipandikiza kwenye ukuta wa uterasi, huwa kuna  ongezeko la kichocheo cha hCG(human chorionic gonadotropin) mwilini. Hiki kichocheo/homoni  hutengenezwa mwilini baada ya siku sita baada ya yai kurutubishwa. Hiki kichocheo kinaweza patikana kwenye damu au mkojo.

bei ya kipimo cha mimba

Hivyo, kuna vipimo viwili maarufu vinavyotumika kutambua iwapo mwanamke ni mjamzito. Kipimo cha damu na mkojo.

  • Kipimo cha damu

Hiki kipimo kinahitaji daktari na maabara. Hakina uzoefu sana kwani gharama yake iko juu ikilinganishwa na vipimo vingine. Hiki kipimo huonyesha ongezeko la  kichocheo cha hCG kwenye damu. Iwapo kuna hCG mwilini humaanisha  una ujauzito.  Kina uwezo wa kuonyesha ongezeko ndogo  sana la hCG.  Hivi huwa bora kutambua ujauzito ata baada ya siku chache.  Pia hiki kipimo cha mimba kina uhakika wa zaidi ya asilimia 99.

  • Kipimo cha mkojo

Hiki kipimo chaweza kufanyika nyumbani  au kwenye maabara. Kipimo hiki cha ujauzito ni cha urahisi na gharama yake iko chini. Hupima kiwango cha homoni ya hCG kwenye mkojo. Kupima ujauzito nyumbani itabidi umenunua stripu (pregnancy test) kwenye duka la dawa. Ukitumia hii stripu unaweza kupima mimba kwa njia mbili:

  1. Weka mkojo kwenye chombo safi kisicho na mafuta ama kemikali yoyote. Hii huzuia kuharibika kwa matokeo. Kisha weka sehemu ya kupimia ndani ya chombo na ufuate maelezo.
  2. Weka sehemu ya kupima kwenye mtiririko unapokojoa ili ilowe. Baada ya vipimo hivi subiri kwa dakika chache ili kupata matokeo.

Majibu hutokea kwa kuonyesha mistari miwili yenye rangi ama alama chanya au hasi. Mifumo ya kidigitali huonyesha ujauzito ama hakuna ujauzito. Wakati mwingine kipimo hutoa majibu chanya. Hili linaweza kusababishwa na mambo kadhaa. Lakini baada ya vipimo viwili bado majibu ikitokea chanya, ni vizuri kutembelea daktari ili vipimo zaidi kufanyika.

Mambo ya kuzingatia unapopima mimba

bei ya kipimo cha mimba

Kujua ni wakati upi mwafaka wa kupima mimba ni muhimu. Wengi hukimbilia kupima siku ifuataye ilihali ata vipimo vya kisasa zaidi huwezi kupata majibu sahihi kwa muda mfupi  hivyo. Wakati mwafaka wa kupima kwa uhakika ni pale mwanamke anakosa kipindi chake cha hedhi. Huu wakati kichocheo cha HCG huwa juu zaidi. Muda wa kupima mimba hutofautiana kati ya mwanamke. Hii ni kwa sababu mizunguko ya hedhi hutofautiana, wengine wana mirefu na wengine mifupi. Yai la mwanamke linaporutubishwa huchukua takriban siku saba mpaka siku kumi kujipandikiza  kwenye ukuta wa uterasi. Baada ya hapo, siku mbili au tatu ili mimba iweze kusoma. Kwa hivyo, kwa ujumla inaweza kuchukua kati ya siku 14 hadi 21 kujua kwa uhakika kama una ujauzito.

Pia wakati mwafaka kwenye siku ni asubuhi pale ile homoni inaonekana vizuri. Bei ya kipimo cha mimba hutegemea ubora wa kipimo. Kipimo cha damu ni uhakika zaidi ya asilimia 99 na kile cha mkojo ni asilimia 99.

Soma Pia: Sababu Zinazo Sababisha Mama Kupata Mimba Ya Mtoto Zaidi Ya Mmoja

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Je, Kupima Mimba Ni Bei Ghali Ama Rahisi?
Share:
  • Je, Ni Wakati Upi Ulio Bora Kufanya Kipimo Cha Mimba?

    Je, Ni Wakati Upi Ulio Bora Kufanya Kipimo Cha Mimba?

  • Vipimo 6 Maarufu Zaidi Vya Kupima Mimba Vya Kinyumbani

    Vipimo 6 Maarufu Zaidi Vya Kupima Mimba Vya Kinyumbani

  • Njia Tofauti Za Kupima Mimba

    Njia Tofauti Za Kupima Mimba

  • Jinsi Ya Kutumia Kipimo Cha Mimba Kupima Iwapo Una Mimba

    Jinsi Ya Kutumia Kipimo Cha Mimba Kupima Iwapo Una Mimba

  • Je, Ni Wakati Upi Ulio Bora Kufanya Kipimo Cha Mimba?

    Je, Ni Wakati Upi Ulio Bora Kufanya Kipimo Cha Mimba?

  • Vipimo 6 Maarufu Zaidi Vya Kupima Mimba Vya Kinyumbani

    Vipimo 6 Maarufu Zaidi Vya Kupima Mimba Vya Kinyumbani

  • Njia Tofauti Za Kupima Mimba

    Njia Tofauti Za Kupima Mimba

  • Jinsi Ya Kutumia Kipimo Cha Mimba Kupima Iwapo Una Mimba

    Jinsi Ya Kutumia Kipimo Cha Mimba Kupima Iwapo Una Mimba

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it