Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mwanamke Anapaswa Kula Nini Katika Mimba? Virutubisho Muhimu Na Vyanzo Vyake

3 min read
Mwanamke Anapaswa Kula Nini Katika Mimba? Virutubisho Muhimu Na Vyanzo VyakeMwanamke Anapaswa Kula Nini Katika Mimba? Virutubisho Muhimu Na Vyanzo Vyake

Ikiwa mama ana tatizika kuchagua chakula muhimu katika ujauzito, ni vyema kuwasiliana na mtaalum wa mlo amshauri kuhusu chakula na viwango vya kuchukua.

Lishe yenye afya kwa mama mjamzito inapaswa kuwa na wanga, protini, ufuta, madini, vitamini na maji. Madaktari huwashauri wanawake wajawazito wanacho paswa kukula kila siku. Kuhakikisha kuwa sahani ina rangi zote na kila kundi la chakula. Ili wawe na virutubisho tosha kutosheleza mahitaji yao na ya fetusi. Tuna angazia chakula muhimu katika ujauzito.

Tazama virutubisho tofauti na chakula kinacho kuwa na virutubisho hivi:

Protini

chakula muhimu katika ujauzito

Ni muhimu kwa ukuaji wa seli na kuchakata damu. Protini ina patikana kwa vyakula kama nyama, samaki, mayai, maharagwe na nyama kutoka kwa ndege wa kinyumbani.

Wanga

Virutubisho muhimu katika kupata nishati ya kila siku. Zinapatikana kwenye vyakula kama vile mchele, mkate, viazi, matunda na mboga.

Iron

Muhimu katika kutengeneza seli nyekundu za damu. Zina epusha kuugua kutokana na anaemia ama upungufu wa damu mwilini. Vyanzo vikuu vya iron ni kama vile nyama nyekundu laini, mchicha na nafaka nzima.

Kalisi

Inasaidia katika kutengeneza mifupa yenye nguvu, meno, misuli na kuboresha utendaji kazi wa neva mwilini. Inapatikana kwenye vyakula kama vile, cheese, maziwa, maziwa ya bururu, na mchicha na sardines.

Vitamini A

chakula muhimu katika ujauzito

Vitamini A inasaidia kuwa na ngozi laini, kuboresha uwezo wa kuona na ukuaji wa mifupa. Inapatikana kwenye mimea kama vile viazi vitamu, karoti, na mboga za kijani.

Vitamini B6

Inatumika katika kutengeneza seli nyekundu za damu, kuboresha uchakataji wa protini, wanga na ufuta mwilini. Inapatikana kwenye nyama ya nguruwe, ndizi na nafaka nzima ambazo hazija chakatwa.

Vitamini B12

chakula muhimu katika ujauzito

Ina dumisha mfumo wa neva na kuhakikisha una afya. Pia inatumika katika kutengeneza seli nyekundu za damu. Inapatikana kwenye nyama, samaki, maziwa, na wanyama wa nyumbani.

Vitamini C

Ufizi  na mifupa yenye afya zina egemezwa na vitamini C. Inatumika kuboresha utumikaji wa iron mwilini. Matunda, nyanya na sharubati za matunda na broccoli ni vyanzo vikuu vya vitamini C.

Vitamini D

Ina saidia kuwa na mifupa na meno yenye nguvu na pia kusaidia katika utumizi mwilini wa kalisi. Vitamini D inapatikana kwenye bidhaa za maziwa, nafaka na mikate.

Ufuta

chakula muhimu katika ujauzito

Hifadhi ya ufuta unao tumika kutoa nishati baada ya vipindi virefu bila kupata chakula. Vyanzo vyake ni kama vile nyama, maziwa, njugu, bidhaa za maziwa na siagi.

Folic acid

Muhimu sana katika mimba. Inasaidia katika kutengenezwa kwa protini na damu. Mboga za kijani na matunda ya kinjano, mboga, njugu na maharagwe huwa na viwango vya juu vya folic acid.

Maji ni sehemu ya lishe. Mama anapaswa kuchukua maji angalau glasi nane kila siku. Kuna virutubisho ambavyo havipatikani kwa idadi tosha kwenye chakula. Na mwanamke hupatiwa tembe anazo paswa kumeza ili kutimiza viwango vya virutubisho vinavyo hitajika mwilini. Ikiwa mama ana tatizika kuchagua chakula muhimu katika ujauzito, ni vyema kuwasiliana na mtaalum wa mlo. Amwagize anacho paswa kula na katika viwango gani.

Soma Pia: Vyakula Visivyo Na Acid Vinavyo Paswa Kuwa Kwenye Lishe Yako Wakati Wote!

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Mwanamke Anapaswa Kula Nini Katika Mimba? Virutubisho Muhimu Na Vyanzo Vyake
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it