Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Je, Kwa Nini Kipindi Changu Cha Hedhi Kimechelewa? Mambo Yanayo Sababisha

3 min read
Je, Kwa Nini Kipindi Changu Cha Hedhi Kimechelewa? Mambo Yanayo SababishaJe, Kwa Nini Kipindi Changu Cha Hedhi Kimechelewa? Mambo Yanayo Sababisha

Huenda ukawa miongoni mwa asilimia ya watu wanao kimbilia kutumia chumvi kupima mimba ama mbinu nyingine ili kudhihirisha iwapo wana tarajia mara tu wanapo kosa kushuhudia kipindi chao cha mimba. Ila, je, kuwa na mimba ndiyo sababu pekee inayo sababisha kipindi cha hedhi kuchelewa? La, hasha. Makala haya yana angazia sababu tofauti ambazo husababisha kipindi cha hedhi kuchelewa.

Kuna vipindi viwili katika maisha ya wanawake ambapo ni kawaida kwa vipindi vyake vya hedhi kutokuwa vya kawaida. Kipindi cha kwanza ni pale anapo anza kushuhudia vipindi vyake vya hedhi. Na pili, vipindi vya hedhi vinapo isha, al maarufu kama menopause kwa kimombo. Kabla ya umri huu kuwadia katika maisha ya mwanamke, hedhi yake huja baada ya siku 28. Ila siku hizi huwa tofauti kwa kila mwanamke, kati ya siku 21 hadi 35.

Kipindi chako kinapo chelewa na kuwa zaidi ya siku tulizo angazia. Huenda ikawa ni kwa sababu ya mambo yafuatayo.

Sababu Za Kuchelewa Kwa Kipindi Chako Cha Hedhi

  1. Uzito Mdogo Wa Mwili

Wanawake walio na matatizo ya kula, kama vile anorexia huenda wakakosa kushuhudia vipindi vyao vya hedhi. Uzito chini ya asilimia 10 ya uzito wa kawaida huenda ukabadilisha jinsi mwili unavyo fanya kazi na kukomesha kupevuka kwa yai. Ni vyema kupata ushauri wa kimatibabu kukusaidia kusuluhisha kasoro zako za kula. Kuongeza uzito kwa njia yenye afya kutakusaidia na kipindi chako. Wanawake wanao husika katika mbio za masafa marefu pia huenda waka kosa kushuhudia vipindi vyao vya hedhi mara kwa mara.

2. Uzito Mwingi Wa Mwili

Sawa na uzito mdogo wa mwili, uzito mwingi unasababisha mabadiliko ya homoni mwilini. Ili kusawasisha homoni mwilini mwako, daktari anaweza kushauri kubadilisha lishe yako na kula vyakula vyenye afya na pia kufanya mazoezi.

chumvi kupima mimba

3. Kukwazwa kimawazo/ fikira nyingi

Fikira nyingi huchangia pakubwa katika kubadili homoni mwilini mwako. Shughuli zako za kila siku na pia kuathiri ubongo wako. Kubadilika kwa homoni mwilini mwako kunasababisha kipindi chako cha hedhi kuchelewa. Kukwazwa na fikira kwa muda mrefu husababisha kupunguka kwa uzito. Ni vyema kujaribu mbinu za kupunguza fikira nyingi ili kusawasisha homoni mwilini mwako.

Je, Kwa Nini Kipindi Changu Cha Hedhi Kimechelewa? Mambo Yanayo Sababisha

4. Mbinu za kudhibiti uzalishaji

Huenda ukashuhudia mabadiliko katika kipindi chako cha hedhi ukitumia baadhi ya mbinu za kudhibiti uzalishaji ama unapo koma kuzitumia. Huenda ikachukua hadi miezi sita ili kipindi chako cha hedhi kusawasishwa.

5. Maradhi sugu

Maradhi kama kisukari huenda yaka athiri kipindi chako cha hedhi na kufanya kichelewe. Mabadiliko katika viwango vyako vya sukari mwilini vina husishwa na kuchelewa kwa kipindi chako ama kukifanya kisiwe cha kawaida.

Wakati wa kumwona daktari.

Ukishuhudia ishara hizi, hakikisha kuwa unamtembelea daktari wako bila kukawia:

  • Kutoa damu nyingi
  • Uchungu mwingi
  • Joto jingi mwilini
  • Kichefu chefu na kutapika
  • Kutoa damu zaidi ya siku saba
  • Kutoa damu hata baada ya kufikisha umri

Kwa hivyo unapokosa kipindi chako cha hedhi, usikue na mbio kutumia chumvi kupima mimba ama mbinu yoyote ile. Ila, hakikisha kuwa unafika kwenye kituo cha matibabu kufanyiwa vipimo kudhibitisha chanzo cha kuchelewa kwa kipindi chako cha hedhi.

Soma Pia: Matatizo Ambayo Wanafunzi Wa Kike Wanakumbana Nayo Wanaposhuhudia Hedhi

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Je, Kwa Nini Kipindi Changu Cha Hedhi Kimechelewa? Mambo Yanayo Sababisha
Share:
  • Jinsi Ya Kupata Mimba Baada Ya Kipindi Chako Cha Hedhi

    Jinsi Ya Kupata Mimba Baada Ya Kipindi Chako Cha Hedhi

  • Sababu Zinazo Athiri Kuchelewa Kwa Kipindi Chako Cha Hedhi

    Sababu Zinazo Athiri Kuchelewa Kwa Kipindi Chako Cha Hedhi

  • Vidokezo Vya Kupata Mimba Na Vipindi Vya Hedhi Visivyo Vya Kawaida

    Vidokezo Vya Kupata Mimba Na Vipindi Vya Hedhi Visivyo Vya Kawaida

  • Njia Za Kuanzisha Kipindi Cha Hedhi Kinapo Chelewa

    Njia Za Kuanzisha Kipindi Cha Hedhi Kinapo Chelewa

  • Jinsi Ya Kupata Mimba Baada Ya Kipindi Chako Cha Hedhi

    Jinsi Ya Kupata Mimba Baada Ya Kipindi Chako Cha Hedhi

  • Sababu Zinazo Athiri Kuchelewa Kwa Kipindi Chako Cha Hedhi

    Sababu Zinazo Athiri Kuchelewa Kwa Kipindi Chako Cha Hedhi

  • Vidokezo Vya Kupata Mimba Na Vipindi Vya Hedhi Visivyo Vya Kawaida

    Vidokezo Vya Kupata Mimba Na Vipindi Vya Hedhi Visivyo Vya Kawaida

  • Njia Za Kuanzisha Kipindi Cha Hedhi Kinapo Chelewa

    Njia Za Kuanzisha Kipindi Cha Hedhi Kinapo Chelewa

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it