Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Chunusi Ni Dalili Ya Ujauzito: Chunusi Na Vyanzo Vyake

3 min read
Chunusi Ni Dalili Ya Ujauzito: Chunusi Na Vyanzo VyakeChunusi Ni Dalili Ya Ujauzito: Chunusi Na Vyanzo Vyake

Chunusi ni dalili ya ujauzito? Swali maarufu kati ya wanawake wanaotarajia kupata mimba, ila la, chunusi husababishwa na vyanzo tofauti mbali na kuwa na mimba.

Kwa kawaida ngozi ya mwanamke huwa tofauti na ya mwanamume. Hutakiwa kuwa laini, nyororo na isiyo na madoa wala ukavu.  Hii ni kutokana na kuwepo kwa homoni ya estrogeni inayozalisha vichocheo kwa ajili ya ngozi nzuri. Je, chunusi ni dalili ya ujauzito?

Chunusi Ni Nini?

chunusi ni dalili ya ujauzito

Chunusi hutokea pale ambapo vinyweleo vinapozibwa na mafuta  pamoja na seli za ngozi zilizokufa. Kwa kawaida hutokea  usoni, kifuani, mabegani na mgongoni. Chunusi hutokea zaidi kwenye umri wa kubalehe ingawa inaathiri watu wa rika lolote.

Nini Husababisha Chunusi?

Kuna sababu nne kuu zinazosababisha  chunusi kutokea:

  • Kuzalisha mafuta kwa wingi
  • Bakteria
  • Vinyweleo kuzibwa na mafuta na ngozi iliyokufa
  • Kuzidi kwa homoni kama vile androgen

Chunusi Ni Dalili Ya Ujauzito?

Wakati wa ujauzito homoni huongezeka na kuongeza kiwango cha sebum kwenye ngozi.  Hii husababisha ngozi ya  mafuta. Mafuta haya pamoja na ngozi iliyokufa huziba  vijitundu vya vinyweleo na kusababisha mafuta kujirundika ndani ya ngozi.

Na hapo ndipo bakteria huingia na kutengeneza aina ya usaha unaotoka kwenye chunusi. Hii aina ya chunusi sio tofauti na zile zingine kama wakati vijana wanabalehe.  Asilimia 50 ya wanawake wajawazito hupatwa na chunusi ila sio jambo la kuogopa.

Cha kuzingatia ni utaratibu wa usafi zaidi ili kuepuka makovu na alama za baadaye.  Kadri  miezi ya ujauzito inavyopita mwili huanza kutulia. Viwango vya estrogeni huanza kuongezeka na kupunguza athari za homoni. Kwa hivyo bila shaka chunusi ni dalili ya ujauzito. Na kina mama walio na shida ya chunusi wana uwezekano mkubwa wa chunusi wakati wa ujauzito.

Sababu Zinazochochea Chunusi Kutokea Na Kuongezeka

chunusi ni dalili ya ujauzito

  • Mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito na matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango husababisha chunusi. Pia kuwepo kwa homoni androgen wakati vijana wanabalehe
  • Tafiti zinaonyesha kuwa vyakula vya wanga kama mkate, chips huongeza makali ya chunusi
  • Msongo wa Mawazo. Msongo wa Mawazo huchochea tatizo la chunusi
  • Mazingira yenye mafuta. Mazingira kama ya jikoni yanaweza kuchochea chunusi
  • Vipodozi vyenye mafuta mengi huchochea chunusi

Jinsi Ya Kuondoa Chunusi

  • Osha uso wako kwa mara mbili kwa siku kuondoa uchafu na mafuta kutoka kwenye ngozi
  • Usisugue uso wako kwani inaweza kusababisha chunusi kuwa mbaya zaidi
  • Tunza nywele zako katika hali ya usafi kwani mafuta kutoka kwa nywele yakifika usoni husababisha chunusi
  • Jihadhari na kutumbua chunusi hii husababisha uvimbe na makovu
  • Pata ushauri wa daktari ili kupambana na chunusi
  • Punguza vyakula vinavyohusishwa na chunusi
  • Usitumie vipodozi ama bidhaa za mafuta kwa sababu unaweza kuwa na chunusi zaidi

Chanzo: WebMD

Soma Pia:Mabadiliko Mwilini Mama Anapokuwa Na Mimba Ya Mwezi Mmoja

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Chunusi Ni Dalili Ya Ujauzito: Chunusi Na Vyanzo Vyake
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it