Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Ishara Za Mapema Za Mimba Na Wakati Zinapo Anza Kuonekana

3 min read
Ishara Za Mapema Za Mimba Na Wakati Zinapo Anza KuonekanaIshara Za Mapema Za Mimba Na Wakati Zinapo Anza Kuonekana

Matiti hubadilika na kuhisi laini zaidi, kufura ama kuuma kufuatia ongezeko la homoni mwilini. Mabadiliko haya huanza kufanyika kutoka wiki ya 4 hadi ya 6.

Kipimo cha mimba na kufanya ultrasound ndizo njia hasa za kufahamu iwapo mwanamke ana mimba ama la. Kujua ishara za mapema za mimba zinaweza saidia kujua mwanamke anapokuwa mjamzito. Mbali na kukosa kipindi cha hedhi, kuna ishara zingine ambazo zina ashiria kuwepo kwa mimba. Unafahamu dalili za mimba huanza kuonekana lini?

Ishara za mimba huanza kuonekana lini?

Umri wa mimba hulingana na wakati mama alianza kupata kipindi cha hedhi. Hiyo ndiyo inayo fahamika kama wiki ya kwanza ya ujauzito, hata kama bado hauna mimba. Wakati unapo tarajia kujifungua huhesabiwa wiki 40 baada ya siku ya kwanza ya hedhi yako ya mwisho.

Dalili za mimba na wakati zinapo anza kushuhudiwa

dalili za mimba huanza kuonekana lini

  • Kukosa hedhi

Yai linapo jipandikiza kwenye kuta za uterasi, homoni hutolewa mwilini na kudhibiti ovari kuto toa yai lingine. Na kumfanya mwanamke kukosa kupata hedhi ya kila mwezi. Mimba inapotungwa, mwili hutoa kichocheo cha hCG kinacho uegemeza ujauzito.

Unapokosa kipindi chako cha hedhi, ni vizuri kufanya kipimo cha nyumbani cha mimba. Vipimo hivi hugundua kuwepo kwa homoni ya mimba ya hCG. Kinapo dhibitisha kipimo chanya, wasiliana na daktari ili uanze kliniki.

  • Kuumwa na tumbo na matone ya damu

Dalili hizi huonekana kati ya wiki ya kwanza hadi ya nne ya ujauzito. Mabadiliko katika kipindi hiki huwa yana tendeka kwenye seli. Matone ya damu yanayo toka baada ya yai kujipandikiza kwenye kuta za uterasi ni tofauti na damu ya hedhi.

Damu hii huwa ya rangi ya pinki ama hudhurungi. Huwa nyepesi na huisha kwa kupunguza kutumia tishu. Uchungu sio mwingi sana ikilinganishwa na uchungu wa hedhi. Na kwa wastani hutoka kwa siku tatu.

  • Mpigo wa moyo ulioongezeka

Katika wiki ya 8 hadi ya 10, moyo wa mwanamke huanza kupiga kwa kasi zaidi. Husababishwa na ongezeko la homoni mwilini.

  • Kichefuchefu na ugonjwa wa asubuhi

chumvi kupima mimba

Katika wiki ya 4 ama ya 6 ya ujauzito, mwanamke huanza kuhisi kichefuchefu na ugonjwa wa asubuhi na pia kutapika. Ishara hizi hushuhudiwa wakati wowote ule wa mchana. Mwanamke ana shauriwa kunywa maji mengi ili kupunguza dalili hizi.

  • Mabadiliko ya matiti

Mabadiliko haya hufanyika kati ya wiki ya 4 hadi ya 6. Matiti hubadilika na kuhisi laini zaidi, kufura ama kuuma kufuatia ongezeko la homoni mwilini. Wiki chache baada ya mwili kuzoea viwango vipya vya homoni, ishara hizi hufifia.

Katika wiki ya 11, rangi ya chuchu hukolea zaidi na kuwa kubwa zaidi.

Ikiwa ulikuwa na shaka dalili za mimba huanza kuonekana lini, makala haya yamekuelimisha zaidi kuhusu dalili unazo paswa kuangazia na wakati upi.

Soma Pia:Je, Masi Rutuba Inaweza Saidia Na Kutunga Mimba?

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Ishara Za Mapema Za Mimba Na Wakati Zinapo Anza Kuonekana
Share:
  • Dalili 3 Kuu Zinazo Ashiria Kuwa Mwanamke Ana Mimba!

    Dalili 3 Kuu Zinazo Ashiria Kuwa Mwanamke Ana Mimba!

  • Je, Mwanamke Anaweza Pata Dalili Za Mimba Siku 4 Baada Ya Kurutubishwa Kwa Yai?

    Je, Mwanamke Anaweza Pata Dalili Za Mimba Siku 4 Baada Ya Kurutubishwa Kwa Yai?

  • Dalili 6 Za Mimba Za Kushangaza Zinazo Shangaza Zaidi

    Dalili 6 Za Mimba Za Kushangaza Zinazo Shangaza Zaidi

  • Je, Ni Yapi Ungependa Kujua Kuhusu Ujauzito?

    Je, Ni Yapi Ungependa Kujua Kuhusu Ujauzito?

  • Dalili 3 Kuu Zinazo Ashiria Kuwa Mwanamke Ana Mimba!

    Dalili 3 Kuu Zinazo Ashiria Kuwa Mwanamke Ana Mimba!

  • Je, Mwanamke Anaweza Pata Dalili Za Mimba Siku 4 Baada Ya Kurutubishwa Kwa Yai?

    Je, Mwanamke Anaweza Pata Dalili Za Mimba Siku 4 Baada Ya Kurutubishwa Kwa Yai?

  • Dalili 6 Za Mimba Za Kushangaza Zinazo Shangaza Zaidi

    Dalili 6 Za Mimba Za Kushangaza Zinazo Shangaza Zaidi

  • Je, Ni Yapi Ungependa Kujua Kuhusu Ujauzito?

    Je, Ni Yapi Ungependa Kujua Kuhusu Ujauzito?

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it