Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vyakula Muhimu Kwa Mtoto: Umuhimu Wa Uji Wa Muhogo Kwa Mtoto!

3 min read
Vyakula Muhimu Kwa Mtoto: Umuhimu Wa Uji Wa Muhogo Kwa Mtoto!Vyakula Muhimu Kwa Mtoto: Umuhimu Wa Uji Wa Muhogo Kwa Mtoto!

Kuongeza kalori mwilini na kuwa chanzo kizuri cha vitamini C, K na thiamine ni baadhi ya faida za uji wa muhogo kwa mtoto.

Chakula sahihi cha kumpatia mtoto anayeanza kula ni moja ya mambo muhimu ambayo huwasumbua wazazi wengi.  Kwa kawaida, mtoto kuanzia umri wa miezi sita huanza kupewa uji maalum kama  kianzio cha kujifunza kula. Uji wa muhogo kwa mtoto huwa ndio chaguo la wengi. Soma zaidi kuhusu faida za uji wa muhogo kwa mtoto.

Kwa Nini Uji wa Muhogo Kwa Mtoto?

faida za uji wa muhogo kwa mtoto

Muhogo ni zao la mzizi.  Ni zao maarufu sana kwa sababu linavumilia ukame na kustawi vizuri bila ya kuhitaji mbolea. Hili zao limefahamika vizuri sana kwa sababu muhogo na unga wa muhogo ni chanzo kizuri na rahisi cha wanga.

Watu huandaa na kula chakula cha muhogo kwa njia mbalimbali katika sehemu mbalimbali za dunia. Kuoka, kuchemsha, na pia watu huvundika na kutumia katika mfumo wa unga.

Unga salama wa mtoto ni ule ambao hauja kaa muda mrefu,  hauna mchanganyiko wa vitu vingi sana, na uwe umezingatia vipimo vya kila kiungo. Muhimu pia ni kuhakikisha nafaka  unazo weka zimeandaliwa vizuri hazija vunda, zimeoshwa vizuri  na kukauka.

Faida Za Uji Wa Muhogo Kwa Mtoto

  • Ni chakula chenye kalori nyingi zaidi kuliko mazao mengine ya mizizi na majani
  • Pamoja na kuwa muhogo una protini nyingi na mafuta kwa kiasi kidogo kuliko mazao ya nafaka, bado kiwango hiki ni kikubwa kuliko cha mazao mengine ya mizizi
  • Muhogo hauna kemikali iitwayo gluten ambayo inaweza  kusababisha athari za magonjwa kwa mlaji
  • Majani machanga ya muhogo hutumika kutengeneza mboga aina ya kisamvu. Huwa chanzo kizuri cha protini na vitamini K. Vitamin K huimarisha mifupa
  • Muhogo ni chanzo kizuri cha vitamini C, thiamine, riboflavin na niacin, madini ambayo ni muhimu sana katika utendaji murua wa mwili wako
  • Madini kama vile chuma, potasiamu, zinki, magnesiamu,shaba na manganizi hupatikana kwa wingi katika chakula cha muhogo

Je,  Muhogo Huwa Na Sumu?

faida za uji wa muhogo kwa mtoto

Hupaswi  kula muhogo mbichi kwa sababu una aina mbili za sumu ya cyanide. Kuupika na  kuuloweka muhogo  kwa ajili ya kuandaa unga wa uji ama ugali huondoa sumu hiyo. Kula chakula hiki pasipo kuandaliwa vyema au kwa namna isiyo sawa kunaweza kusababisha  athari mbaya za kiafya.

Hata hivyo, bidhaa zinazotokana na zao la muhogo kama vile unga ni salama kuliwa kwa kupikwa. Hii ni kwa sababu tayari sumu inakuwa imeondolewa kupitia jua au kulowekwa na kuanikwa juani.

Madhara makubwa yanayoweza  kutokana na kushindwa kuandaa vyema uji wa mtoto ni:

  • Nafaka zikiwa chafu mtoto ataharisha. Na ikitokea mahindi au nafaka nyingine yoyote ilikuwa na dawa na ukapika bila kuosha vizuri mtoto anaweza pata matatizo ya ini
  • Pia nafaka ambazo hazikukauka vizuri mfano yaweza kuwa karanga, mahindi au yoyote ikivunda kuna sumu ambayo inaitwa flatoxin inapatikana humo inaweza pia leta tatizo la ini
  • Kama kiwango cha wanga kimezidi sana unampa mtoto nguvu nyingi ambayo haitaji kwa muda huo. Na kwa mtoto mwenye kisukari  ukimpa uji wenye wanga mwingi lazima sukari itakuwa inapanda.

Kupata mtoto ni safari mpya wazazi huanza kupitia, ni kipindi ambacho hubadilisha maisha na mipango ya wazazi. Chaguo la uji wa muhogo kwa mtoto wako ni bora kwa sababu ya manufaa mengi kwa afya yake. Faida za uji wa muhogo kwa mtoto ni nyingi na muhimu katika ukuaji na maendeleo yake.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Chakula Bora Cha Mtoto Wa Miezi Tatu

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Feeding & Nutrition
  • /
  • Vyakula Muhimu Kwa Mtoto: Umuhimu Wa Uji Wa Muhogo Kwa Mtoto!
Share:
  • Ukweli Kuhusu Lishe Ya Mboga Na Imani Zisizo Za Kweli

    Ukweli Kuhusu Lishe Ya Mboga Na Imani Zisizo Za Kweli

  • Je, Kuna Uhusiano Kati Ya Kula Lishe Ya Mboga Pekee Na Kupoteza Uzito?

    Je, Kuna Uhusiano Kati Ya Kula Lishe Ya Mboga Pekee Na Kupoteza Uzito?

  • Fahamu Manufaa Ya Kunyonyesha Kwa Wote Mama Na Mtoto

    Fahamu Manufaa Ya Kunyonyesha Kwa Wote Mama Na Mtoto

  • Ukweli Kuhusu Lishe Ya Mboga Na Imani Zisizo Za Kweli

    Ukweli Kuhusu Lishe Ya Mboga Na Imani Zisizo Za Kweli

  • Je, Kuna Uhusiano Kati Ya Kula Lishe Ya Mboga Pekee Na Kupoteza Uzito?

    Je, Kuna Uhusiano Kati Ya Kula Lishe Ya Mboga Pekee Na Kupoteza Uzito?

  • Fahamu Manufaa Ya Kunyonyesha Kwa Wote Mama Na Mtoto

    Fahamu Manufaa Ya Kunyonyesha Kwa Wote Mama Na Mtoto

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it