Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mambo Ambayo Wanawake Wanaogopa Katika Uhusiano

3 min read
Mambo Ambayo Wanawake Wanaogopa Katika UhusianoMambo Ambayo Wanawake Wanaogopa Katika Uhusiano

Kuna sababu nyingi ambazo huchangia uhusiano kuisha. Ni jambo linalo waumiza wachumba wote wawili, hata ingawa mwanamke huumia zaidi kwani ni rahisi kwa mwanamke kupenda.

Baadhi ya wakati, mwanamke hukosa kujihusisha na mwanamme yoyote ama kuingia katika uhusiano naye kufuatia uwoga na hofu za wanawake katika uhusiano. Sio kana kwamba hangependa kupenda ama kupendwa, mbali kuna vitu anavyo hofia kuwa zitatendeka katika uhusiano huo na kumwumiza mtima wake. Huenda ikawa hofu hizi ni kutoka uhusiano alio kuwa nao hapo awali ama mambo aliyo ona yakiwatendekea watu walio karibu naye.

Na sababu hizi kumfanya abaki peke yake bila mchumba. Ni muhimu kwa mwanamke kufahamu mambo yanayo mtia kiwewe na shaka ili apate njia ya kukumbana na hofu hizi. Tazama orodha yetu itakayo kujuza kuhusu mambo ambayo wanawake wengi siku hizi wanaogopa katika ndoa.

Hofu za wanawake katika uhusiano

hofu za wanawake katika uhusiano

  1. Kutoka nje

Kila mtu anaogopa kuwa kwenye uhusiano na mtu ambaye baada ya wakati ataanza kutoka nje na kutafuta wachumba wengine. Jambo hili linawafanya wanawake wengi kufanya uamuzi wa kubaki peke yao bila kujihusisha katika uhusiano wowote ule. Kutoka nje huwa na athari hasi kwa mwanamke kwa sababu ataanza kujiuliza maswali na kushangaa kama hatoshi ama ikiwa kuna mambo anayo yafanya isivyo faa.

2. Kuwa na mchumba asiye mtosheleza

Wanawake wengi wana hofu ya kuwa na wanaume wasio kimu mahitaji yao ya kihisia, kiakili ama hata kifedha. Hasa ikiwa mwanamke huyu ana uwezo wa kuyakimu mahitaji yake bila matatizo yoyote yale. Pia, kuna hofu ya kuwa na mwanamme ambaye wakati wote anatarajia uende mrama na imani zako ili kumtosheleza.

3. Mwanamme sawa na mchumba wake wa awali

Mabinti huwa na uwoga kuwa wanaume wote ni sawa. Kumaanisha kuwa kama mchumba wako wa hapo awali alikuumiza, huenda utakaye mpata baada yake awe sawa na akufanyie mambo sawa na kukuumiza.

4. Kuto heshimiwa

hofu za wanawake katika uhusiano

Hakuna anaye penda kuto patiwa heshima, hasa katika uhusiano. Unapo ingia kwenye uhusiano na mtu yeyote yule, maono yako ni kuwa mtakuwa pamoja kwa muda mrefu na mapenzi yenu yatadumu. Ila ndoto hizi hukatizwa mmoja wenu anapo anza kuto heshimu mwingine.

5. Kufikiria kuwa yeye sio mrembo vya kutosha

Mabinti wengi hufikiria kuwa wanapaswa kuwa warembo vya kutosha ikiwa mwanamme atabaki nao. Wakati mwingi, ama wakati wote, sio lawama ya mwanamke mwanamme anapo toka nje ya ndoa. Na jambo hili humvunja mwanamke moyo.

6. Uhusiano kuisha baada ya wakati mdogo

Kuna sababu nyingi ambazo huchangia uhusiano kuisha. Ni jambo linalo waumiza wachumba wote wawili, hata ingawa mwanamke huumia zaidi kwani ni rahisi kwa mwanamke kupenda. Wanawake wengi hawaoni haja ya kuwa katika uhusiano kisha ukaisha baada ya siku chache. Na kufanya uamuzi wa kuto penda ama kupendwa.

Soma Pia: Sababu Kwa Nini Mchumba Wako Atatoka Nje Ya Ndoa Yenu

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Mambo Ambayo Wanawake Wanaogopa Katika Uhusiano
Share:
  • Kemia Na Utangamano Katika Uhusiano: Nini Muhimu Zaidi?

    Kemia Na Utangamano Katika Uhusiano: Nini Muhimu Zaidi?

  • Kwa Nini Una Harakisha Kufunga Ndoa?

    Kwa Nini Una Harakisha Kufunga Ndoa?

  • Mazungumzo Muhimu Kabla Ya Kuingia Katika Uhusiano!

    Mazungumzo Muhimu Kabla Ya Kuingia Katika Uhusiano!

  • Jinsi Ya Kukuza Imani Katika Uhusiano: Njia Za Kujenga Uaminifu

    Jinsi Ya Kukuza Imani Katika Uhusiano: Njia Za Kujenga Uaminifu

  • Kemia Na Utangamano Katika Uhusiano: Nini Muhimu Zaidi?

    Kemia Na Utangamano Katika Uhusiano: Nini Muhimu Zaidi?

  • Kwa Nini Una Harakisha Kufunga Ndoa?

    Kwa Nini Una Harakisha Kufunga Ndoa?

  • Mazungumzo Muhimu Kabla Ya Kuingia Katika Uhusiano!

    Mazungumzo Muhimu Kabla Ya Kuingia Katika Uhusiano!

  • Jinsi Ya Kukuza Imani Katika Uhusiano: Njia Za Kujenga Uaminifu

    Jinsi Ya Kukuza Imani Katika Uhusiano: Njia Za Kujenga Uaminifu

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it