Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Ishara 5 Kuwa Hauko Tayari Kufunga Ndoa

2 min read
Ishara 5 Kuwa Hauko Tayari Kufunga NdoaIshara 5 Kuwa Hauko Tayari Kufunga Ndoa

Kuwa na uhusiano na wachumba wa hapo awali na kutokuwa na nguvu za kusamehea mara kwa mara ni ishara kuwa hauko tayari kufunga ndoa.

Ikiwa uko katika uhusiano na kuwa na shaka kuhusu uhusiano wenu na iwapo utafunga ndoa na mchumba wako. Ishara hizi zinaashiria kuwa hauko tayari kufunga ndoa.

Ishara kuwa hauko tayari kufunga ndoa

ishara hauko tayari kufunga ndoa

  1. Unahisi kuwa kuna mengi haujafanya

Kuna watu wengi wanaoingia kwenye ndoa bila kufanya uamuzi dhahiri kuwa wanataka kuwa katika ndoa. Wanahisi kuwa hawajamaliza kufanya mambo fulani ya maisha ya kuwa pekee kabla ya kuwa na familia. Hata kama unahisi kuwa mchumba wako anakufurahisha na ungependa kuwa na familia naye, hisia za kutomalizana na maisha ya kuwa pekee yatakujia. Kuwa na mazungumzo wazi na mchumba wako kuhusu unavyohisi na unachotaka.

2. Una uhusiano na wachumba wako wa hapo awali

Kuwa marafiki na wachumba wako wa awali sio chanzo cha shaka. Wajulishe wako huru kuja kwenye harusi yako na kufanya urafiki na watu wengine. Lakini ikiwa ungali una hisia zao na ungependa kuwa na zaidi ya urafiki nao, ni ishara kuwa kamwe hauko tayari kufunga ndoa. Hisia na akili zako ziko mbali na mchumba wako wa hivi sasa. Ikiwa ungali una urafiki na wachumba wako wa hapo awali, ni vyema kuwa na mipaka dhahiri ambayo wao pia wanafahamu na kuiheshimu.

3. Humwamini mchumba wako na siri zako

Kabla ya kufunga ndoa na mpenzi wako, ni muhimu kuhakikisha kuwa unamwamini na habari zako za siri. Tunaelewa kuwa kuna baadhi ya vitu ambavyo sio lazima kumjulisha. Hata hivyo, kuhisi kuwa humwamini mchumba wako na siri zako ni bendera nyekundu. Huenda ikawa kuna jambo linalokufanya kuhisi hivyo. Ikiwa una hofu zinazokufanya usihisi kuwa huru kuzungumza naye, mjulishe na kwa pamoja mtaweza kupata suluhu. Suluhu inapokosekana, ni ishara kuwa hamko tayari kufunga pingu za maisha.

ishara hauko tayari kufunga ndoa

4. Hauna ndoto za maisha yenu pamoja baada ya harusi

Watu wengi hufurahishwa na harusi na kuyafumbia macho maisha baada ya ndoa. Ikiwa hauna maono ya maisha yenu pamoja baada ya kufunga ndoa. Hiyo ni ishara kuwa haujayafikiria maisha yenu pamoja kwa kina.

5. Wewe ni mgumu kusamehea

Watu wanapoishi pamoja, ni vigumu kuto vurugana. Mara kwa mara mtakosania vitu vidogo na mchumba wako. Huenda mchumba wako akasahau kutupa takataka kwenye pipa na badala yake kuacha jikoni. Ikiwa hauko tayari kumsamehea mara kwa mara hata anapofanya vitu vinavyokaa vya kitoto machoni mwako, hauyuko tayari kufunga ndoa.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Faida Ya Kufanya Tendo La Ndoa Wakati Wa Ujauzito

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Ishara 5 Kuwa Hauko Tayari Kufunga Ndoa
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it