Je, nitajuaje iwapo binti yule ananipenda ama la? Kufahamu ishara kuwa mwanamke anakupenda na vitu ambavyo mwanamke atafanya kama tu anakupenda kutakusaidia kuwa na uhakika iwapo anakupenda ama unatupa wasaa wako.
Ili kuwasaidia wanaume kufahamu iwapo kwa kweli wanapendwa ama wako kwa orodha ya marafiki wa kiume maarufu kama friendzone. Tuna angazia ishara zinazodokeza kuwa mwanamke anakupenda.
Ishara kuwa mwanamke anakupenda

- Anakuambia siri zake
Ni vigumu kwa mwanamke kumwambia mwanamme siri zake. Hofu kubwa huwa kuwachana naye kisha kuwa na siri ambazo mtu waliyekosana naye anazitambua. Mwanamke anapopatana na mwanamme anayempenda na kumwamini, atamwambia siri zake bila hofu kuwa zitatumika kumwumiza hapo baadaye.
2. Kufanya utani nawe
Ikiwa mwanamke ana uhuru wa kukufanyia utani, kucheka nawe, kukuiga kwa mfano, unavyotembea, kuongea ama kufanya mambo, bila shaka anakupenda.
3. Kukusamehe mara kwa mara
Mwanamke anapokupenda, kufumba jicho kwa mengi utakayoyafanya. Hii siyo sababu ya kumfanyia maradhau ama kumkosea mara kwa mara kisha uombe msamaha. La hasha. Hata hivyo, kumbuka kuwa kila mwanamke huwa na mipaka yake.
4. Yuko makini na mahitaji yako
Mwanamke anapopenda humtunza mchumba wake. Kumnunulia zawadi mara kwa mara, kudekezwa kwa kweli. Mara kwa mara, utaamkia zawadi kama vile viatu, soksi, chakula na vifaa vya kielektroniki kama play station ikiwa mchumba wako anajua unapenda vifaa kama hivyo. Ikiwa mchumba wako anapesa, huenda akakulipia mesi ama massage.
5. Anatabasamu nawe sana
Mwanamke anayekupenda ata tabasamu na kucheka sana akiwa karibu nawe. Hata bila sababu kubwa ya kucheka. Kila unapomwangalia, ata tabasamu na kuona haya kisha kuangalia chini. Hii ndiyo ishara ya kwanza na kubwa zaidi inayokudokezea kuwa binti huyu anakupenda.

6. Kuzungumza nawe mara nyingi kwa siku
Ukitaka kumkasirisha mwanamke aliye katika mapenzi, chukua rununu yake ama umtenge na kifaa cha mazungumzo anachokitumia. Kila mara anataka kuzungumza na mpenzi wake, kumjulia hali, kuuliza anachofanya, ikiwa amekula, anakoenda, walio naye. Maelezo yote ya nyanja zote za maisha yake, maisha ya kikazi, marafiki na kadhalika.
7. Kushauriana nawe kabla ya kufanya uamuzi
"Ngoja nimwulize mpenzi wangu kwanza." Usemi maarufu kati ya wanawake walio katika uhusiano wa siku mbili. Katika kila afanyacho, atataka kuuliza ushauri wako kwanza. Hata kama hatafuata ushauri wako, angali atakuuliza kusikia utakachosema. Siri - mpe sikio lako na umpe ushauri, usiwaze sana iwapo atafuata ushauri wako ama la. Wanawake wanapenda kupata ushauri kutoka kwa wanaume wanaowapenda.
Kwa hivyo ikiwa msichana usiye na uhakika iwapo anakupenda anakuomba ushauri mara kwa mara, una jibu lako.
Soma Pia: Ukweli Kuhusu Kufanya Mapenzi Ukiwa Na Mimba