Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Ishara 5 Zinazo Dhibitisha Kuwa Mwanamme Ni Baba Mwema Kwa Watoto Wake

3 min read
Ishara 5 Zinazo Dhibitisha Kuwa Mwanamme Ni Baba Mwema Kwa Watoto WakeIshara 5 Zinazo Dhibitisha Kuwa Mwanamme Ni Baba Mwema Kwa Watoto Wake

Ulezi ni kazi inayohitaji juhudi na nishati bora. Kila mwanamme angependa kuwa baba mwema kwa watoto wake, tazama ishara za baba mwema!

Kuna usemi maarufu kuwa, " Mwanamme yeyote anaweza kuwa baba, lakini inachukua mwanamme kamili kuwa mzazi." Kuwa baba kuna maana kuwa wewe ndiye nguzo ya nguvu, kuegemezwa na nidhamu. Je, ishara za baba mwema ni zipi? Na vipi unaweza kuwa mmoja?

Sawa na kuwa mama, jukumu la kuwa baba linahitaji juhudi zisizoisha, lakini kuna fanaka nyingi kuona mtoto wako akikua kuwa mtu mzima. Tazama baadhi ya vidokezo vya kukusaidia kuwa baba anayependwa na watoto wake!

Ishara za baba mwema

Ishara za baba mwema

  1. Patia familia yako kipau mbele ikilinganishwa na kazi yako

Jukumu la kulisha familia yako ni mojawapo ya majukumu ambayo baba huchukulia kwa kina. Walakini, kazi inaweza chukua muda wako mwingi ambao unaweza kutumika na watoto na bibi yako.

Kama baba, unaweza kuwa na juhudi na kuwa bora katika uyafanyayo, lakini kumbuka kuwa familia huja kwanza, wakati wote. Fanya kazi unapokuwa kazini na usibebe kazi za ofisini kuzimalizia nyumbani. Ili upate wakati tosha wa kuwa na familia yako.

2. Husika katika masomo na michezo ya mwanao

Baba mwema siye anayewajibika kuwalisha watoto wake tu, mbali anachukua hatua zaidi katika kuhakikisha kuwa amehusika katika kazi zote za watoto wake. Kuwajulia jinsi siku yao nyumbani ama shuleni ilivyokuwa. Kwa kuwasaidia kufanya kazi za ziada pamoja, kucheza nao baada ya kazi. Ni muhimu kwa baba kuuliza maswali haya.

Siku yako shuleni imekuwa vipi leo?

Umepata marafiki wapya shuleni?

Mwalimu alifunza nini leo?

Je, unapendelea somo gani zaidi?

Hakikisha kuwa, unamsaidia mke wako kuwalaza watoto. Wasomee hadithi kabla ya kulala kisha uombe nao.

3. Kuwa na wakati tosha na familia

dad-proof-recipes

Mfunze mtoto wako jinsi ya kuendesha baiskeli na kupika. Cheza na vidoli vyake, tazama vipindi vya watoto anavyopenda naye. Onyesha hamu katika vitu anavyopenda kufanya. Kumbuka kuwa unaweza kutengeneza fedha zaidi lakini sio makumbusho yasiyoweza kulipiwa.

4. Wafunze maadili mema

Maadili unayowafunza watoto wangali wachanga ndiyo watafuata hata uzeeni wao. Wafunze kufungulia mabinti milango, kutoa sahani mezani baada ya kula. Baba mwema atafanya kadri awezavyo kuwafunza watoto wake maadili. Kuwa funza kuwa wapole, kuheshimu watu na kutokata tamaa ni maadili muhimu kwa watoto wangali wachanga. Kuwa mfano mwema wa kuigwa. Kumbuka kusisitiza nidhamu kwa watoto wako, waelewe sawa na mbaya wangali wachanga. Kutumia maneno kama, pole, shukrani, niwie radhi ni muhimu.

5. Mpende na umheshimu mama yao

Je, unasaidia mkeo na kazi za kinyumbani kama kuwalisha watoto, kuwalaza ama kupika? Je, unambusu bibi yako kabla ya kwenda kazini? Ikiwa jibu la maswali haya ni "ndiyo", wewe ni baba mwema! Ulezi sio rahisi na huchukua muda na nishati nyingi, kutoka kwako na bibi yako. Hata hivyo, ni muhimu kuhakikisha kuwa unamsaidia bibi yako ili asiwe amechoka wakati wote. Wakati mwingine, mpe muda afanye vitu anavyovipenda ama apumzike.

Chanzo: Independent

Soma Pia: Kwa Nini Watoto Wengi Hupendelea Kuwa Na Mama Zao Na Wala Sio Baba

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Ishara 5 Zinazo Dhibitisha Kuwa Mwanamme Ni Baba Mwema Kwa Watoto Wake
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it