Ugonjwa wa kansa umekuwa maarufu sana. Ni vyema kufahamu ishara za kansa na wakati unapopaswa kwenda kwenye kituo cha afya kufanyiwa vipimo.

Kuwa na doa kwenye ngozi inayobadilika saizi, shepu na rangi huenda ikawa ishara ya saratani ya ngozi. Huenda ikawa doa hii ni tofauti na doa zingine mwilini mwako. Unapogundua kuwa una ishara zisizo za kawaida, ni vyema kukaguliwa na daktari wa ngozi. Vipimo vya ngozi hutoa seli kidogo za uso ili kubaini iwapo kuna seli za saratani zinazokua.
Mabadiliko kwenye matiti mara zote sio kufuatia saratani. Hata hivyo, mwanamke anapaswa kujikagua mara kwa mara kwa kugusa matiti yake kuona iwapo kuna uvimbe. Ishara za hatari ni kama uvimbe, mabadiliko kwenye chuchu, kuhisi uchungu ama chuchu kuwa nyekundu.
Kwa watu wasiovuta sigara, kuna kiwango cha nafasi kuwa, kuwa na kikohozi kisicho isha ni ishara ya saratani. Kikohozi huenda kikasababishwa na maambukizi ama astham. Kinapozidi kwa muda mrefu na kuanza kukohoa damu, unapaswa kuenda kwenye kituo cha afya. Vipimo vitadhibitisha iwapo una saratani ya mafua.
Kuhisi uchungu kwenye koo unapomeza chakula ama vinywaji mara nyingi husababishwa na baridi ama aina fulani ya dawa. Ni vyema kutembea kwenye kituo cha afya. Kutatizika kumeza vitu huenda ikawa ni ishara ya saratani ya koo. Vipimo vitabaini iwapo ni tatizo la kawaida ama kwa kweli una saratani inayokua.
Kufura tumbo husababishwa na kuwa na mawazo mengi ama lishe hafifu. Ishara hii inapoambatana na uchovu, kuhisi mnyonge, kukata uzani na uchungu kwenye mgongo, ni vyema kufanyiwa vipimo. Kuhisi uvimbe mara kwa mara katika wanawake huenda ikawa ishara ya saratani ya ovari.
- Kuvuja damu kusiko kwa kawaida kutoka kwa uke
Kuvuja damu na sio hedhi mara nyingi huhusishwa na kuwa na fibroids ama kutumia aina ya uzazi wa mpango. Unapovuja damu ovyo bila kufahamu chanzo, ni vyema wakati wote kuwasiliana na daktari ili vipimo vifanyike kubaini chanzo cha tatizo lile.

Mojawapo ya ishara maarufu za kansa ni kukata uzani kwa kasi. Kuna sababu zingine ambazo huenda zikamfanya mtu kukata uzito wa mwili. Kama unapoanza kufanya mazoezi na kula lishe bora, ila, uzani utakuwa wenye afya. Unapoanza kupunguza uzito kwa kasi bila chanzo, ni vyema kuwasiliana na daktari.
Kuona damu unapoenda msalani sio jambo la kawaida. Kwa hivyo unapoenda msalani kisha uone damu ama uvimbe, kuna nafasi huenda ukawa unaugua saratani ya koloni ama ya kibofu.
Soma Pia: Unaufahamu Ugonjwa Wa Listeria Katika Ujauzito?