Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Ishara Za Mimba Yenye Afya Na Isiyo Na Afya Kwenye Uterasi

3 min read
Ishara Za Mimba Yenye Afya Na Isiyo Na Afya Kwenye UterasiIshara Za Mimba Yenye Afya Na Isiyo Na Afya Kwenye Uterasi

Kutoa shaka zote kuwa mimba yako ina tatizo na mtoto ana afya kwenye uterasi, ni muhimu kwa mama kufahamu ishara za mimba yenye afya na isiyo na afya. 

Kutoa shaka zote kuwa mimba yako ina tatizo na kuwa mtoto anakua ipasavyo na ana afya kwenye uterasi, ni muhimu kwa mama kufahamu ishara za mimba yenye afya na isiyo na afya.

Ishara za mimba yenye afya

ishara za mimba yenye afya

Mwendo wa fetusi

Mama anapofikisha miezi tano ya ujauzito, fetusi huanza kuwa na mwendo kwenye uterasi. Mwendo wa mtoto huongezeka kunapokuwa na mwangaza. Katika mwezi wa saba, mwendo wa mtoto huathiriwa na sauti, mwangaza na uchungu. Mama anapofikisha mwezi wa nane, mwendo wa mtoto huongezeka na kupunguka katika mwezi wa tisa kufuatia kukosa nafasi tosha tumboni.

Kuongeza uzito katika mimba

Kwa kawaida, mama mwenye mimba huongeza kati ya kilo 10 hadi 15 za uzani anapokuwa na mimba. Kila anapoenda kliniki, uzito wake hupimwa kudhibitisha iwapo mtoto anakua ipasavyo. Ikiwa kuna mabadiliko yoyote, ni vyema kwa mama kuwasiliana na daktari wake.

Ukuaji wa kawaida

Fetusi hukua kwa inchi mbili kila mwezi. Katika mwezi wa saba, fetusi huwa inchi 14. Mama anapokaribia kujifungua katika mwezi wa tisa, fetusi inapaswa kuwa kati ya inchi 18 hadi 20 za urefy na kilo kati ya 2.5 na 3. Kipimo cha ultrasound hufanyika kudhibitisha iwapo mtoto anakua kwa njia ipasayo na iwapo ana changamoto zozote za kifizikia.

Mpigo wa moyo

Moyo wa mtoto aliye kwenye uterasi huanza kupiga katika wiki ya tano ya ujauzito. Kuna kipimo kinachofanyika kudhibitisha mpigo wa moyo wa mtoto. Unapaswa kuwa kati ya 110 na 160 kwa kila dakika.

Nafasi ya mtoto katika kipindi cha uchungu wa uzazi

Katika mwezi wa tisa, fetusi huwa imekua na kuchukua nafasi nyingi kwenye uterasi, na hivyo basi kupunguza mwendo wa fetusi tumboni. Mtoto mwenye afya huwa na kichwa chini katika uchungu wa uzazi ili kichwa kianza kutoka mama anapojifungua.

Ishara za fetusi isiyo na afya

ishara za mimba yenye afya

Urefu usio wa kawaida

Kipimo cha kudhibitisha ukuaji wa mtoto hufanyika ili daktari aweze kufahamu iwapo mtoto anakua apasavyo kadri mimba inavyozidi kukua.

Fetusi kukosa mpigo wa moyo

Moyo wa fetusi huanza kupiga katika wiki ya tano, hata hivyo, udhibiti bayana hufanyika katika wiki ya 10. Kuna kifaa cha kieletroniki kinachotumika kudbitisha mpigo wa moyo wa fetusi. Mtoto asipofikisha mpigo unaohitajika, wanafahamu kuwa kuna tatizo.

Kuumwa na tumbo zaidi katika mimba

Ujauzito ni kipindi cha kusisimua pamoja na kuhisi uchungu na uchovu. Maumivu mepesi ya tumbo muda kwa muda huwa sawa. Ila, maumivu haya yanapozidi, ni ishara kuwa kuna kasoro na mama anapaswa kuwasiliana na daktari.

Kutokwa na damu katika ujauzito

Kuna baadhi ya wanawake wanaoshuhudia kutokwa na damu wanapokuwa na mimba. Hata hivyo, damu hii huwa kiasi kidogo. Kutokwa na kiasi kikubwa cha damu ni ishara ya hatari na huenda ikadhihirisha kuwa mama anapoteza mimba.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Vidokezo 5 Vya Kuwa Na Ujauzito Salama Na Wenye Afya

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Ishara Za Mimba Yenye Afya Na Isiyo Na Afya Kwenye Uterasi
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it