Kwa wanandoa wanao jaribu kutunga mimba, sio rahisi kuwashauri wangoje hadi wafanye kipimo cha mimba kudhibitisha iwapo wana mimba. Huenda wakawa na shaka kuhusu baadhi ya vitu wanavyo hisi baada ya kupevuka kwa yai- je, ni ishara za ujauzito? Ishara za ujauzito huanza baada ya muda upi?
Ili kipimo cha mimba kidhihirishe matokeo sahihi, mwanamke anastahili kungoja siku chache baada ya kukosa kipindi chake cha hedhi. Hii ndiyo njia bora ya kufahamu ikiwa ana ujauzito ama la. Huenda akaanza kuona dalili nyepesi siku nne baada ya kupevuka kwa yai. Ukweli ni kuwa, ishara za mimba huanza kudhihirika siku 14 baada ya yai kurutubishwa. Lakini kuna utafiti unao dhihirisha kuwa baadhi ya dalili huenda zikaonekana mapema.
Ishara za mapema za mimba kabla ya siku 14

Hata ikiwa kuna baadhi ya wanawake ambao wanaweza shuhudia ishara za mapema kabla ya siku 14 baada ya kurutubishwa kwa yai kuisha. Huenda wengine waka ngoja hadi siku 14 ziishe. Tazama baadhi ya ishara za ujauzito ambazo unaweza ona:
- Kuvuja damu. Kuvuja damu siku chache baada ya kurutubishwa kwa yai huenda kukawa ni ishara ya yai kujipandikiza kwenye kuta za uterasi. Kunako fanyika siku 6-12 baada ya yai kurutubishwa.
- Kichefu chefu. Hii ni ishara maarufu katika ujauzito inayo sababishwa na ongezeko la viwango vya homoni mwilini.
- Kuumwa na tumbo. Katika siku za kwanza za mimba, mwanamke anaweza hisi kuumwa na tumbo. Uchungu sawa na anapo kuwa na kipindi chake cha hedhi.
- Chuchu laini. Chuchu za mwanamke kuwa nyeti sana. Ishara hii ni sawa na pale mwanamke anapo anza kupata kipindi chake cha hedhi.
Kukosa kipindi chako cha hedhi ni mojawapo ya ishara maarufu zaidi zinazo dhihirisha kuwa mwanamke ana mimba. Ishara zingine huenda zikachukua zaidi ya siku 9 baada ya kurutubishwa kwa yai kuanza kuonekana.
Ishara zingine za mapema za mimba ni kama vile:

- Kuhisi tumbo imefura
- Kutamani kula vyakula fulani
- Mhemko wa hisia
- Uchovu mwingi
Kuwa makini kuona mabadiliko mwilini mwako. Hakikisha una zungumza na daktari wako una poa mambo usiyo na uhakika kuyahusu. Ikiwa una maswali zaidi kuhusu ishara za ujauzito huanza baada ya muda upi, daktari wako atakusaidia.
Soma Pia:Sababu 6 Kuu Zinazo Sababisha Mwanamke Kupata Mimba Ya Ectopic