Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Je, IVF Ni Nini? Yote Unayopaswa Kujua Kuhusu Mbinu Hii Ya Kupata Mtoto

2 min read
Je, IVF Ni Nini? Yote Unayopaswa Kujua Kuhusu Mbinu Hii Ya Kupata MtotoJe, IVF Ni Nini? Yote Unayopaswa Kujua Kuhusu Mbinu Hii Ya Kupata Mtoto

Watu wanao uliza swali, 'je, IVF ni nini' mara nyingi wanataka kujua nafasi za kufaulu kwa mbinu hii. Kuna sababu nyingi zinazo changia ufanisi wake.

Katika siku za hapo awali, IVF iliongelelewa kwa sauti za chini ambazo hazingependa kusikika. Je, IVF ni nini? Hivi leo, mambo ni tofauti na IVF ni jina maarufu. Sio tu njia ya wazungu ya kupata mimba. Tuna angazia kwa kina maana ya IVF.

Je, IVF ni nini?

ivf ni nini

Ufupi wa In vitro fertilization, ni njia inayotumia teknolojia kumsaidia mwanamke kutunga mimba kwa kusaidia uwezo wake wa kuwa na rutuba, ukuaji wa fetusi na kujipandikiza kwa yai kwenye uterasi. Wanandoa wanapata mimba kwa urahisi.

IVF hufanyika kwa kutoa ovari za mwanamke na manii ya kiume kisha kuchanganywa kwenye maabara ya kimatibabu. Ili kukubalisha manii kurutubisha mayai. Mimba inapofanyika na fetusi kuchukua shepu, mtaalum ataipandikiza kwenye uterasi.

Kwa nini IVF inatumika?

Mbinu hii hutumika kwa sababu tofauti. Baadhi ya wanandoa huitumia kama njia ya mwisho, huku wengine wakiitumia kwasababu wangependa kupata mtoto zaidi ya mmoja.

Baadhi ya sababu kwa nini watu hutumia IVF:

  • Kwa visa ambapo ovari inakosa kufanya kazi, kuwa na fibroids kwenye uterasi na matatizo ya kupevuka kwa yai
  • Endometriosis
  • Kuwa na fallopian tubes zisizo fanya kazi
  • Mzazi mmoja ama wawili kuwa na tatizo la kijeni ambalo hawangependa kupitisha kwa kizazi chao
  • Kwa visa ambapo mirija ya kizazi imetolewa kupitia kwa upasuaji
  • Mchumba wa kiume ana tatizika na ugumba kama kuwa na idadi ya chini ya manii ama manii kukosa uwezo wa kusafiri

Ufanisi wa IVF

ivf ni nini

Watu wanao uliza swali, 'je, IVF ni nini' mara nyingi wanataka kujua nafasi za kufaulu kwa mbinu hii. Ni muhimu kufahamu kuwa asilimia ya kufaulu kwa mbinu hii kunategemea:

  • Umri wa mama
  • Mitindo ya maisha
  • Historia ya uzalishaji
  • Endometriosis
  • Chanzo kikuu cha ugumba

Kulingana na utafiti, asilimia 33 ya mbinu za IVF hufaulu. Na kumaanisha kuwa asilimia 33 ya wanawake hupata mimba na kujifungua kwa ufanisi mara ya kwanza baada ya kujaribu IVF.

Kufuatia sababu fulani za hatari, mbili kati ya mimba tatu ya IVF huenda ikaharibika. Lakini kuna hatua ambazo wanawake wanaweza kuchukua kuongeza nafasi zao za kubeba mimba hadi ikomae.

  • Pumzika vya kutosha
  • Kupunguza mawazo mengi
  • Kukoma mitindo kama kuvuta sigara na kunywa pombe
  • Kula vyakula vyenye afya hasa matunda na mboga
  • Kuchukua vitamini za prenatal inavyofaa
  • Kunywa maji kwa wingi
  • Kwenda kwa kliniki za antenatal

Ni vyema kwa wanawake kukumbuka kuwa, kujifungua kupitia kwa IVF hakukufanyi kuwa mama mchache ikilinganishwa na wengine. Furahi kuwa umepata baraka zako.

Kumbukumbu: NHS

IvfWorldwide.com

Soma Pia: Athari Hasi Za Kutumia Tembe Za Kupanga Uzazi

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Trying To Conceive
  • /
  • Je, IVF Ni Nini? Yote Unayopaswa Kujua Kuhusu Mbinu Hii Ya Kupata Mtoto
Share:
  • Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

    Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

  • Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

    Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

  • Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

    Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

  • Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

    Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

  • Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

    Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

  • Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

    Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it