Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mbinu Asili Za Kuondoa Michirizi Baada Ya Kujifungua

3 min read
Mbinu Asili Za Kuondoa Michirizi Baada Ya KujifunguaMbinu Asili Za Kuondoa Michirizi Baada Ya Kujifungua

Sharubati la viazi hutumika kuondoa alama zinazo baki baada ya kidonda kupona na mwanamke anaweza kutumiakuondoa michirizi mwilini.

Michirizi ama alama za kunyoosha sio jambo geni kwa wanawake hasa baada ya kujifungua. Katika mimba, mwili wa mwanamke hupitia mabadiliko mengi. Kuongeza uzito hufanya mwili kupata alama za michirizi kufuatia mabadiliko ya kasi. Mara nyingi, sehemu zinazo athiriwa na alama za michirizi ni kwenye matiti, tumbo, mapaja na pia mikono. Ni vigumu kuondoa michirizi mwilini lakini kuna mbinu za kupunguza kuonekana kwake.

Jinsi ya kuondoa michirizi

Kuna njia asili za kupunguza kuonekana kwake kama vile kwa kutumia mafuta ya kupiga masi. Kuzingatia utaratibu wa kupaka mafuta haya muda kwa muda, michirizi hii itapungua baada ya muda.

  • Kutumia aloe vera

Aloe Vera, kuondoa michirizi

Aloe vera imekuwa ikitumika kwa muda mrefu kurekebisha hali tofauti za ngozi. Kupaka aloe kwenye sehemu iliyoathiriwa na michirizi kunasaidia kupunguza kuonekana kwake. Paka kwenye ngozi kisha uwache ibaki kwa dakika 15 kabla ya kuisugua sehemu hiyo.

  • Kutumia mafuta

kuondoa michirizi

Kupaka na kisha kusugua mafuta kwenye sehemu zilizo na michirizi husaidia pakubwa na kupunguza kuonekana kwa michirizi mwilini na kuifanya ngozi ilainike.

Baadhi ya mafuta bora kufanya hivi ni kama vile mafuta ya olive na mafuta ya kupiga masi.

Utaratibu wa kufuata

  • Weka mafuta kwenye mikono kisha usugue sehemu iliyoathirika
  • Kisha uiwache kwa dakika 30
  • Safisha sehemu hiyo kisha uokoge mwili
  • Kuna baadhi ya watu wanaofanya uamuzi wa kupaka mafuta wanapolala
  • Kumbuka kuwa jambo hili litachukua muda

Sharubati ya limau

kuondoa michirizi

Limau ina nguvu za kupunguza kuonekana kwa alama ya kidonda mwilini. Hivyo basi inatumika kupunguza michirizi mwilini.

Tia sharubati ya limau kwenye kontena. Kisha upake kwenye sehemu iliyo na michirizi. Iwache itulie kwa dakika 15. Baada ya hapo, safisha kwa kutumia maji ya vuguvugu. Zingatia utaratibu huu kila siku ili uone mabadiliko.

  • Asali

kuondoa michirizi

Asali ina uwezo wa kupunguza kuonekana kwa vidonda mwilini. Weka kiwango kidogo cha asali mkononi, kisha uwekelee kwenye sehemu iliyoathiriwa hadi ikauke. Unaweza amua kutumia kipande cha mavazi. Baada ya kukauka, safisha kwa kutumia maji ya vuguvugu.

Mbali na mbinu hizi, mwanamke anaweza kutumia mchanganyiko wa sukari, maziwa na maji kuondoa michirizi mwilini. Sharubati la viazi hutumika kuondoa alama zinazo baki baada ya kidonda kupona na hutumika kupunguza kuonekana kwa sana kwa michirizi.

Ni vyema kwa wanawake kukumbuka kuwa mbinu hizi huchukua muda kabla ya matokeo kuanza kuonekana. Pia, wanapaswa kuzingatia utaratibu huu kwa muda bila kukoma. Mwili wako unapendeza kwa njia yoyote ile, haijalishi iwapo una michirizi sehemu nyingi mwilini. Upende mwili wako ulivyo huku ukichukua hatua kuufanya upendeze zaidi.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Jinsi Ya Kupunguza Uzani Wa Mwili Kwa Mama Aliye Jifungua

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Mbinu Asili Za Kuondoa Michirizi Baada Ya Kujifungua
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it