Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jinsi Ya Kupata Usingizi Haraka: Njia 5 Kuu Za Kupata Usingizi Kwa Kasi

2 min read
Jinsi Ya Kupata Usingizi Haraka: Njia 5 Kuu Za Kupata Usingizi Kwa KasiJinsi Ya Kupata Usingizi Haraka: Njia 5 Kuu Za Kupata Usingizi Kwa Kasi

Mwanga wa buluu hutokana na vifaa vya kielektroniki kama vile simu, runinga na tarakilishi na kupunguza utoaji wa kichocheo cha melatonin mwilini kinachotufanya tulale.

Ikiwa unatatizika na kulala na kushangaa jinsi ya kupata usingizi kwa haraka, tuna kudokezea siri zitakazokusaidia. Kupata usingizi tosha ni muhimu katika utendaji kazi wa mwili wa kila siku. Kulingana na Sayansi, unapaswa kupumzika kwa masaa manane kila usiku. Lakini kufuatia mabadiliko ya kimaisha na haja ya kufanya kazi ili kukimu mahitaji ya kimaisha, inakuwa vigumu kulala kwa masaa haya yote. Hata hivyo, kutolala vya kutosha kuna athari hasi kwa mwili. Ikiwa unatatizika kulala, tazama vidokezo hivi.

Jinsi ya kupata usingizi kwa haraka

jinsi ya kupata usingizi kwa haraka

  1. Tumia godoro na mto bora

Watu wengi hupuuza umuhimu wa kutumia godoro na mto bora, na kusema kuwa hakuna haja ya kununua godoro ya kikliniki, na kuwa ina bei ghali. Ni muhimu kubadilisha mto na godoro baada ya muda. Kulalia godoro iliyozeeka huumiza mgongo na shingo na huenda ikafanya usingizi kupotea usiku. Huenda ukagundua kuwa unalala kama mtoto unapokuwa kwenye hoteli ila mambo yanakuwa tofauti ukiwa kwako. Hii ndiyo sababu. Badilisha godoro na mto unaotumia, nunua kwenye chapa zinazoaminika.

2. Tazama na usikilize vitu vinavyopuzisha akili usiku

Kusikiliza na kutazama vitu vinavyopumzisha akilini jioni ni muhimu, ili kuiweka akili katika mazingira ya kutulia tayari kulala. Tofauti na kusikiliza muziki wenye sauti ya juu na filamu za kutisha ambazo zinahusisha akili kufikiria. Kusoma kitabu kinacholiwaza na kuburudisha kunaituliza akili.

3. Tengeneza chumba cha kulala

jinsi ya kupata usingizi kwa haraka

Chumba chako cha kulala kinaathiri uwezo wako wa kulala kwa kasi ama kukosa usingizi. Paka rangi isiyo shouting sana. Hakikisha kuwa unatengeneza kitanda chako kwa kutumia matandiko safi. Punguza mwanga unaoingia chumbani chako usiku, epuka kutumia radio na runinga chumbani cha kulala. Hakikisha pia chumba chako kinapata hewa safi na tosha.

4. Punguza mwanga wa buluu usiku

Mwanga wa buluu hutokana na vifaa vya kielektroniki kama vile simu, runinga na tarakilishi. Kulingana na utafiti, mwanga wa buluu hupunguza utoaji wa kichocheo cha melatonin mwilini kinachotufanya tulale. Epuka kutumia mitandao ya kijamii usiku, badala yake, soma kitabu.

5. Kuwa na ratiba maalum ya kulala

Kuzingatia ratiba maalum ya kulala na kuamka kunasaidia kuizoesha akili yako kuwa wakati fulani unapaswa kuwa ukilala, huku ukiamka wasaa fulani. Zingatia ratiba hii na baada ya muda utafahamu kuwa hautatiziki kuamka wala kulala. Kubadilisha ratiba yako ya kulala huenda kukaathiri usingizi wako.

Soma Pia: Faida 7 Za Kufanya Yoga Kwa Afya Yako

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Jinsi Ya Kupata Usingizi Haraka: Njia 5 Kuu Za Kupata Usingizi Kwa Kasi
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it