Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vidokezo 3 Muhimu Vya Jinsi Ya Kutumia Mitandao Kwa Wanandoa

2 min read
Vidokezo 3 Muhimu Vya Jinsi Ya Kutumia Mitandao Kwa WanandoaVidokezo 3 Muhimu Vya Jinsi Ya Kutumia Mitandao Kwa Wanandoa

Mitandao ya kijamii ni vyombo ambavyo vinaweza kutumika kuboresha mahusiano yetu na wachumba wetu na watu wengine, ila huenda vikawa na athari hasi visipo tumika vyema.

Mitandao ya kijamii- jinsi ya kuitumia. Siku hizi, tumezoea mitandao ya kijamii sana kama vyombo vya mawasiliano vinavyo tusaidia kuwajulisha watu kinachofanyika maishani mwetu, kujua jinsi wengine wanavyo endelea na kuungana tena na marafiki wetu wa hapo awali. Je, utumizi wa mitandao ya kijamii inaweza kuathiri ndoa zetu kivipi? Inalingana na jinsi ambavyo mitandao hii inavyo tumika. Tazama vidokezo muhimu vya jinsi ya kutumia mitandao kwa wanandoa.

Jinsi ya kutumia mitandao kwa wanandoa

jinsi ya kutumia mitandao kwa wanandoa

  1. Kuwa na mipaka

Sote tunafahamu jinsi ambavyo wakati hupita kwa kasi tunapo anza kutumia mitandao kama Facebook ama Instagram. Tukichambua kurasa baada ya nyingine kuangalia kinacho tendeka na habari za hivi punde. Wengine wetu huenda wakawa na hatia ya kutumia muda zaidi kwenye mitandao ikilinganishwa na tunavyo zungumza na wachumba wetu. Huenda tukachukua muda zaidi kutuma jumbe kuhusu chakula chetu kwenye mitandao badala ya kuzungumza na wachumba wetu. Tusipokuwa makini, kuwasiliana na dunia huenda ikachukua kipau mbele ikilinganishwa na kuzungumza na wachumba wetu.

Fikiria kuhusu kuweka mipaka kwenye wakati unaotumia katika mitandao ya kijamii. Kwa mfano, nusu saa kila siku ama unapo zuru peke yako. Wanandoa wanapaswa kujadiliana kuhusu matarajio yao kuhusu mitandao ya kijamii. Mawasiliano yanayo fanyika kwenye mitandao ya kijamii hasa na jinsia tofauti. Pia mambo msiyopaswa kuweka kwenye mitandao ya kijamii.

2. Kuwa wazi

Kuwa na uwazi ni muhimu katika ndoa zote, ambapo wanandoa hawafichi kitu chochote. Hata inapofika kwa mitandao ya kijamii. Mkubalishe mchumba wako aweze kuona mitandao  yako ya kijamii na unachokifanya. Hata kumpa neno lako la siri.

jinsi ya kutumia mitandao kwa wanandoa

3. Kuwa na heshima

Ikiwa umemkasirikia mchumba wako, mitandao ya kijamii sio mahali pa kumtolea mchumba wako hasira zako. Sharti moja ni kuwa, haupaswi kuweka ujumbe wowote kwenye mitandao ya kijamii ambayo hauwezi pendelea ukiwekwa kwenye kurasa ya kwanza ya gazetti. Badala yake, kuwa na jumbe chanya kwenye mitandao. Unapokuwa na tatizo lolote na mchumba wako, litatue mbali na mitandao. Epuka kuweka picha ambazo mchumba wako hapendelei kwenye mitandao.

Mitandao ya kijamii ni vyombo ambavyo vinaweza kutumika kuboresha mahusiano yetu na wachumba wetu na watu wengine, tunapofuata vidokezo tulivyo angazia.

Iwapo una mawazo zaidi kuhusu njia bora za kutumia mitandao ya kijamii, tujulishe kwa kuwacha ujumbe mdogo hapa!

Chanzo: family.org

Soma Pia: Kumchukia Bwana Baada Ya Kujifungua: Vyanzo Na Suluhu La Jambo Hili

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Vidokezo 3 Muhimu Vya Jinsi Ya Kutumia Mitandao Kwa Wanandoa
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it