Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jinsi Ya Kulea Watoto Wasio Dhani Ni Haki Yao Kupata Kila Kitu

2 min read
Jinsi Ya Kulea Watoto Wasio Dhani Ni Haki Yao Kupata Kila KituJinsi Ya Kulea Watoto Wasio Dhani Ni Haki Yao Kupata Kila Kitu

Kufanya kazi pamoja na watoto wako nyumbani kunawasaidia kujifunza jinsi ya kufanya kazi wanapokuwa kwa timu.

Watoto wetu wako katika kizazi tofauti na kilicho na raslimali zaidi. Hawafahamu njaa na kukosa ni nini. Kila wanapo enda kwenye duka na kusema wangependa hiki, wanakipata. Kutia juhudi sio jambo wanalo elewa kwa undani. Lakini wanapokua na kukumbana na dunia isiyo kuwa na huruma, hawajui jinsi ya kuishi. Na hakuna mzazi anayetaka watoto wake wakumbane na jambo hili. Suala kuu kuwa, jinsi ya kuwalea watoto wasiotarajia kupata vitu vyote wanavyo vitaka.

Jinsi ya kuwalea watoto

  • Kubali kusaidiwa

jinsi ya kuwalea watoto

Kuna baadhi ya familia ambazo huwapatia watoto wao pesa kila wiki. Huku wazazi wengine wakiamini kuwa, watoto wao wanapaswa kufanya kazi za kinyumbani ili kupata pesa- kuwafunza dhamani ya kila shilingi.

Kulingana na wataalum wa mahusiano ya kijamii, Beth Johnson, wazazi wanao wapatia watoto pesa baada ya kufanya kazi za kinyumbani, wanawasaidia kuhisi ni haki yao. Kulingana na mtaalum huyu, watoto hawa wataanza kutarajia kulipwa baada ya kufanya kazi ndogo nyumbani. Wazazi wanapaswa kuwafunza watoto kusaidia na kazi za kinyumbani kwani wao ni timu moja kubwa.

Professa David Lancy kutoka Chuo Kikuu cha Utah, watoto huwa tayari kusaidia na kazi za kinyumbani wanapotimiza miezi 18. Katika tamaduni zingine, watoto huwa tayari wameanza kusaidia na kazi za kinyumbani bila kutarajia malipo yoyote. Kwa upande mwingine, baadhi ya wazazi huwafanyia watoto kila kitu bila kuwapa nafasi ya kusaidia. Watoto hawa huhisi kuwa kusaidia ni kazi ngumu na sio jukumu lao. Wanapo zidi kukua, hawataki kusaidia wazazi wao tena.

  • Kuhusisha majukumu ya kinyumbani na pesa kunawachanganya watoto

jinsi ya kuwalea watoto

Kufanya majukumu ya kinyumbani kunawasaidia watoto kuwajibika kifamilia. Pia ni ishara ya jinsi mwanao atakavyo fuzu katika kazi zao za usoni. Majukumu yanawasaidia watoto kufanya kazi vyema wakiwa kwa timu.

Kuwalipa watoto wako kwa kusafisha nyumba, vyombo na vyumba vyao hakuna manufaa yoyote. Hata hivyo, watoto wanaweza patiwa pesa wanapofanya kazi zaidi lakini isiwe kama malipo.

Hakuna umri mdogo sana kwa watoto kuanza kusaidia na majukumu ya kinyumbani - hasa kama wanajitolea kusaidia. Watakuwa wanauliza maswali mengi, kwa hivyo ni vyema kuwa na upole. Chukua muda kuwaelezea kivipi na maana ya kufanya mambo haya nyumbani.

Ila, usiwe wakali sana kwao, katika umri huu, wangali wanajifunza kufanya kazi. Kama ni kutengeneza kitanda, usitarajie kiwe kimetengenezwa kwa viwango vyako. Pongeza juhudi zao. Fuata vidokezo hivi viwili vya jinsi ya kuwalea watoto ili kuwalea watoto wasiodhani kuwa ni haki yao kupata kila wanacho kitaka.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Hatari Za Kuongea Mabaya Kuhusu Mchumba Wako Kwa Familia Na Marafiki Wako

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Jinsi Ya Kulea Watoto Wasio Dhani Ni Haki Yao Kupata Kila Kitu
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it