Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jitenge na Vitu Hivi 7 Katika Mimba

2 min read
Jitenge na Vitu Hivi 7 Katika MimbaJitenge na Vitu Hivi 7 Katika Mimba

Kipindi cha mimba huwa nyeti kwa afya ya mama na mtoto. Jitenge na vitu hivi katika mimba ili kuwa na mimba salama.

Kuna masharti mengi kuhusu vitu unavyopaswa kufanya na usivyopaswa kufanya katika mimba. Masharti ya kawaida ni kama kujitenga na utumiaji wa pombe na dawa za kulevya. Mbali na masharti hayo ya kawaida, jitenge na vitu hivi katika mimba.

Jitenge na vitu hivi katika mimba

1.Kukandwa mwili

jitenge na vitu hivi katika mimba

Kukandwa mwili huwa na manufaa kwa mwili na hasa katika mimba. Hata hivyo, kuna aina za kukandwa zisizo salama kwa mama katika miezi ya kwanza mitatu ya mimba. Aina ya kukandwa mwili ambapo mtu hudungwa sindano ndogo kwenye mgongo sio salama kwa mama katika miezi ya kwanza mitatu. Pia, tumbo ya mama haipaswi kukandwa katika miezi ya kwanza mitatu.

2. Paka

Mjamzito anapaswa kujitenga na kusafisha uchafu wa paka, kwani kinya cha paka huenda kikawa na maambukizi ya toxoplasmosis. Maambukizi haya humweka mama katika hatari ya kupoteza mimba ama mtoto kuzaliwa na matatizo ya ubongo ama kuona.

3. Kemikali za kusafisha

Kemikali nyingi za kusafisha huwa na onyo kwa wanawake wajawazito. Kwani bidhaa zilizotumika huwa hatari kwa afya ya mama na mtoto. Kabla ya kutumia kemikali hizi, ni muhimu kwa mama kuhakikisha kuwa hazina onyo kwa mama mjamzito. Dirisha zinapaswa kuwa wazi mama anaposafisha na kuhakikisha kuwa chumba kinapata hewa tosha.

4. Rangi

Rangi inayopakwa kwenye kuta huwa hatari kwa ukuaji wa mtoto katika trimesta ya kwanza ya mimba. Ni vigumu kudhibitisha kiwango cha hatari kwa mtoto. Hatari yoyote ile huathiri ukuaji wake, kwa hivyo ni vyema kwa mjamzito kukaa mbali na mahali penye rangi ambayo haijakauka.

5. Dawa zisizoagizwa na daktari

jitenge na vitu hivi katika mimba

Kununua dawa kwa maduka ya dawa bila ushauri wa daktari ni hatari. Katika mimba, dawa ambazo mjamzito anachukuwa zinapaswa kuwa zimeagizwa na daktari ili kuhakikisha kuwa ni salama kwa afya yake na ya mtoto.

6. Kahawa

Kunywa vikombe vingi vya kahawa katika mimba kunaongeza shinikizo la damu na mpigo wa moyo. Mfumo wa kimetaboliki wa mtoto ungali unakua kwa hivyo kunywa kaffeini nyingi kunaushinikiza. Kaffeini inatokana na kahawa, soda, chokleti na baadhi ya dawa.

7. Vileo

Vileo vya aina yoyote ile katika mimba huwa na athari hasi kwa mama na fetusi. Kupitia kwa mfumo wa damu, vileo hupita kwenye placenta na kumfikia mtoto. Inaathiri ukuaji wa ubongo na viungo vingine vya mwili. Athari hasi katika mimba ni kama vile kuharibika kwa mimba, kujifungua mtoto kabla ya wakati, kuathiri ubongo wake ama mtoto kuzaliwa na matatizo ya kimaumbile.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Jitenge na Vitu Hivi 7 Katika Mimba
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it