Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Ni Kiasi Gani Sawa Cha Kuvuja Damu Katika Ujauzito

3 min read
Ni Kiasi Gani Sawa Cha Kuvuja Damu Katika UjauzitoNi Kiasi Gani Sawa Cha Kuvuja Damu Katika Ujauzito

Kuvuja damu wakati wa ujauzito ni ishara ya jambo linalohitaji uchunguzi zaidi. Hivyo hakuna kiasi cha kuvuja damu kilicho kawaida katika mimba ila spotting.

Mama anaposhika mimba kuvuja damu huwa jambo la wasiwasi. Ila kiasi cha kuvuja damu kinaweza kuashiria iwapo ni hali ya dharura au la. Hivyo, kuna kiasi cha kuvuja damu kilicho kawaida katika mimba?

Kiasi Cha Kuvuja Damu Kilicho Kawaida Katika Mimba

kiasi cha kuvuja damu kilicho kawaida katika mimba

Kwa kawaida mama mjamzito hutokwa na damu kiasi kidogo mwanzoni  wa ujauzito. Hii hufahamikka kama implantation bleeding.  Yai linaporutubishwa kwenye mirija ya fallopian baada ya siku sita hadi siku kumi na mbili, lile yai husafiri hadi kwenye mfuko wa uterasi na kujipandikiza pale.

Huku kusafiri kwa hili yai hadi kuja kwa uterasi ndio hupelekea matone ya damu kutoka ukeni. Hivi hutoka kwa uchache mno kwenye kile kipindi mtu alifaa kupata siku zake hedhi. Hii huweza kutokea ndani ya  siku kumi hadi kumi na nne. Baadaye huja ikakoma.

Hii hukoma kwani lile tendo la yai kujipandikiza kwenye mfuko wa uzazi limekamilika. Pia hujulikana kama spotting. Hii huwa sawa kabisa na huwa si hatari aidha kwa mama au mtoto. Ila kuna hali zingine ambazo zinahitaji uchunguzi zaidi. Kama vile kuvuja damu iwapo mimba inatishia kutoka.

 Kwa Nini Mimba Itishie Kutoka?

Kuna mazinigira hatarishi kwa mama mjamzito kama vile:

  • Mama aligongwa tumboni ama mama alipata mshtuko. Dalili yake ni damu kutoka ukeni ikiambatanishwa na maumivu au yasiwe
  • Bakteria infection husababisha mimba kutishia kutoka. Hili hufanyika kwenye mji wa mfumo wa uzazi. Wakati wa uzazi sio uterasi pekee inayotanuka mbali pia servksi. Kwa hivyo kama kuna maambukizi mama huweza kuvuja  damu
  • Maambukizi ya virusi ikawa inaashiriwa na damu kutoka ukeni
  • Wale wenye uzito mkubwa wanaweza kuwa na dalili ya mimba kutishia kutoka na kuashiriwa pia na kutokwa na damu ukeni
  • Kuna plasenta ambayo hupitisha virutubishi kutoka kwa mama hadi kwa mtoto. Hii plasenta inafaa kuwa juu ya tumbo la uzazi. Ila kwa kina mama wengine inaweza kuwa iko chini au kwenye shingo la uzazi. Hii husababisha matone ya damu kutoka kwenye uke
  • Kubadilika kwa vichocheo vya homoni husababisha matone ya damu kutoka ukeni

Sababu Nyingine Kuu Za Kuvuja Damu

kiasi cha kuvuja damu kilicho kawaida katika mimba

Kuvuja damu kabla ya wiki 28 za ujauzito hudhaniwa kuwa ni kuvuja damu mapema katika ujauzito. Ikitokea baada ya wiki 28 huitwa utokaji wa damu wa baadaye katika ujauzito. Mkato huu wa wiki 28 umezingatia uwezekano wa kuishi ikiwa mtoto atazaliwa kabla ya tarehe iliyotarajiwa katika wiki 28.

Matumaini ya kuishi kabla ya wiki 28 ni madogo sana katika nchi nyingi zinazoendelea. Hii ni kwa kuwa  kuna upungufu wa vifaa vya afya vya utunzaji maalum kwa watoto wanaozaliwa  kabla ya wakati.

Visababishi vikuu vya kuvuja damu mapema katika ujauzito ni utoaji mimba, kutoka kwa mimba mapema kwa sababu ya kufa kwa fetasi, mimba iliyotungwa nje ya uterasi (ectopic pregnancy) na mimba isiyo kuwa ya kawaida.

Kama unatokwa na damu unashauriwa:

  • kupata mapumziko
  • kutofanya mapenzi
  • kuepuka kazi ngumu
  • kujiepusha na uvutaji sigara, kunywa pombe na madawa ya kulevya
  • Kuepuka mkazo wa mawazo

Kuvuja damu wakati wa ujauzito ni ishara ya jambo linalohitaji uchunguzi zaidi. Hivyo hakuna kiasi cha kuvuja damu kilicho kawaida katika mimba ila spotting.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Sababu Zinazo Athiri Kuchelewa Kwa Kipindi Chako Cha Hedhi

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Ni Kiasi Gani Sawa Cha Kuvuja Damu Katika Ujauzito
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it