Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Fahamu Jinsi Vipimo Vya Ujauzito Hufanya Kazi

3 min read
Fahamu Jinsi Vipimo Vya Ujauzito Hufanya KaziFahamu Jinsi Vipimo Vya Ujauzito Hufanya Kazi

Vipimo vya mimba hupima kiwango cha kichocheo ama homoni ya human chorionic gonadotropin kwa mkato HCG kwenye damu ama mkojo.

Vipimo vya ujauzito ni muhimu katika kumsaidia mwanadada ama wanandoa kufahamu ikiwa wana tarajia mtoto ama la. Kuna aina tofauti ya vipimo vinavyo tumika kupima mimba. Kama vile kipimo cha asili cha kupima mimba kutumia chumvi ama kupima damu. Makala haya yana lenga kukuelimisha jinsi vipimo vya mimba vinavyo fanya kazi.

Jinsi vipimo vya mimba vinafanya kazi

jinsi ya kutumia kipimo cha mimba

Vipimo vya mimba hupima kiwango cha kichocheo ama homoni ya human chorionic gonadotropin kwa mkato HCG kwenye damu ama mkojo. Kichocheo hiki huchakatwa mwilini siku sita baada ya yai lililo rutubishwa kujipandikiza kwenye kuta za uterasi ama kuta za mji wa mimba. Idadi ya kichocheo hiki huongezeka mara mbili baada ya siku 6 na kuzidi kuongezeka kwa kiasi hicho baada ya kila siku 2 ama 3.

Aina za vipimo

kupima mimba kutumia kitunguu maji

Kuna vipimo vya aina mbili vinavyo tumika kupima mimba ili kufahamu kama mwanadada ana mimba. Hasa kipimo cha damu ama cha mkojo.

  1. Kipimo cha damu

Kipimo hiki huwa dhabiti na sahihi zaidi. Ila, haiwezekani kufanyia nyumbani. Kipimo cha aina hii kina hitaji utaalum na kinafanyika kwenye maabara ama zahanati. Kina uwezo wa kudhibitisha ikiwa mwanamke ana mimba baada ya siku 6 ama 8 za kufanya ngono isiyo salama. Tofauti na kipimo cha mkojo ambapo matokeo yake yana onekana kwa kasi, kipimo hiki huchukua muda kidogo kabla ya matokeo kubainika.

Kipimo hiki huwa na malengo mawili, na haya ni: 

  • Kupima uwepo wa kichocheo cha HCG. Kipimo cha aina hii huwa na mafanikio kinapo fanyika baada ya siku 10. Kina dhibitisha kuwepo ama kutowepo kwa kichocheo hiki kwenye mkojo.
  • Kupima wingi wa kichocheo cha HCG. Kipimo hiki hupima idadi ama wingi wa homoni hii kwenye damu. Faida nyingine ya kipimo hiki ni kusaidia kujua matatizo yoyote katika kipindi cha mimba. Kupitia kwa kipimo hiki, daktari anaweza jua ikiwa mimba ilitungwa nje ya kizazi.

2. Kipimo cha mkojo

Kipimo hiki huwa cha kasi, rahisi, cha bei nafuu na kinaweza fanyika nyumbani ama hospitalini.

Unapo fuata maagizo ya kukitumia ipasavyo, utapata matokeo ya kweli. Maagizo yake ni rahisi kufuata.

Vipimo hivi vya mimba huwa na usahihi wa asilimia 99. Ukiamua kutumia mbinu yoyote ile ya kupima mimba, kipimo cha asili cha kupima mimba ama kipimo cha damu, una nafasi asilimia 99 ya kupata matokeo sahihi.

Ukigundua kuwa una mimba, hakikisha kuwa unaenda kwa kituo cha afya ikiwa ulifanyia kipimo chako nyumbani. Daktari atakushauri jinsi utakavyo anza utunzaji kabla ya kujifungua.

Soma Pia: Ishara 5 Kuwa Unapaswa Kufanya Kipimo Cha Mimba

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Fahamu Jinsi Vipimo Vya Ujauzito Hufanya Kazi
Share:
  • Aina Mbili Kuu Za Vipima Mimba Vilivyoko!

    Aina Mbili Kuu Za Vipima Mimba Vilivyoko!

  • Vipimo 6 Maarufu Zaidi Vya Kupima Mimba Vya Kinyumbani

    Vipimo 6 Maarufu Zaidi Vya Kupima Mimba Vya Kinyumbani

  • Jinsi Ya Kufanya Kipimo Cha Mimba Kwa Usahihi

    Jinsi Ya Kufanya Kipimo Cha Mimba Kwa Usahihi

  • Vipimo Asili Vya Mimba Vya Kubaini Kuwepo Kwa Mimba

    Vipimo Asili Vya Mimba Vya Kubaini Kuwepo Kwa Mimba

  • Aina Mbili Kuu Za Vipima Mimba Vilivyoko!

    Aina Mbili Kuu Za Vipima Mimba Vilivyoko!

  • Vipimo 6 Maarufu Zaidi Vya Kupima Mimba Vya Kinyumbani

    Vipimo 6 Maarufu Zaidi Vya Kupima Mimba Vya Kinyumbani

  • Jinsi Ya Kufanya Kipimo Cha Mimba Kwa Usahihi

    Jinsi Ya Kufanya Kipimo Cha Mimba Kwa Usahihi

  • Vipimo Asili Vya Mimba Vya Kubaini Kuwepo Kwa Mimba

    Vipimo Asili Vya Mimba Vya Kubaini Kuwepo Kwa Mimba

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it