Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Fahamu Njia Tofauti Za Kupima Mimba Nyumbani

3 min read
Fahamu Njia Tofauti Za Kupima Mimba NyumbaniFahamu Njia Tofauti Za Kupima Mimba Nyumbani

Kipimo cha ujauzito kwenye simu kinashauriwa sana lakini ni vyema baada ya kukifanya umwone daktari wako ili aweze kukuelekeza iwapo matokeo ni chanya.

Kipimo cha ujauzito kwenye simu kina manufaa sana kwa mwanadada yeyote anayetaka kufahamu kama ana mimba au la.Teknolojia imesaidia sana jinsia ya kike kwani wamewezesha kipimo cha kupima mimba kwenye simu. Kuna vipimo aina nyingi ambazo kina dada hutumia kupima mimba kama vile ya zahanatini au ya kinyumbani. Kupitia njia hii mpya ya kupima mimba kwenye simu, kujua hali yako Imerahisishwa kwa kuwa mtu anapata matokeo hapo hapo na kwa haraka. Kulinganisha na vipimo vya hapo awali,kina dada walilazimika kwenda mpaka hostipitalini kupimwa,kisha baadae asubiri kwa muda mrefu ili apate matokeo.

Vipimo hivi vya simu vinafanya kazi vipi?

kipimo cha ujauzito kwenye simu

 

Kipimo hiki cha mimba hufanya kazi kama vipimo hivi vingine vya zahanatini. Kipimo hiki hupima kiwango cha homoni inayoitwa HCG, ambayo huanza kutengenezwa na mwili wa kina dada siku sita baada ya yai la uzazi lililorutubishwa na mbegu ya kiume kujipandikiza kwenye nyuta za uterasi.

Kuna kijiti ambacho mtu hutumia kupima mkojo, katika teknolojia hii kijiti hiki huunganishwa na Bluetooth,kisha baadae matokeo hutumwa kwenye simu yako. Ili uweze kujua kama una mimba au la. Kipimo hiki huchukua muda wa dakika tatu. Unaposubiri unaweza kupata wosia kuhusu jinsi ya kulea mtoto,chakula bora ya kukula ukiwa mjamzito, njia bora mbali mbali za kuongeza kiwango cha uzazi.

Vipimo tofauti tofauti za kupima mimba

kipimo cha ujauzito kwenye simu

Kuna aina nyingi sana ambazo zinaweza kudhibitisha kama una mimba au la.

Kipimo cha mkojo

Kipimo hiki hususisha kuweka kijiti cha kupima mimba kwenye mkojo. Utafiti umetamatisha kwamba ni vyema kuchukua mkojo asubui ukiamka kabla ya kula kiamsha kinywa ili uweze kupata matokeo yaliyo sahihi kwa kiwango cha asilimia 99.Unapoeka mkojo katika kontena yako ,tia kijiti kile humo ndani.

Utafiti wa wataalam tofauti tofauti wa kisayannsi huhimiza kina dada kuchukua kipimo cha kipima mimba kwenye simu siku 14 baada ya siku ya yai la uzazi kurutubishwa kwenye kuta za uterasi.

Kipimo cha damu

Kiwango cha usahihi katika kipimo hiki huwa juu sana.Kipimo hiki huwa ni cha kisayansi. Kipimo hiki hupima asalimia ya homoni ya HCG katika  mwili wako. Kina dada wanaweza kupima mimba wiki ya kwanza baada ya yai la uzazi kurubitishwa na kujipachika kwenye kuta za uterasi.

Dawa tofuati tofauti zinazoweza kuathiri matokeo ya kipimo cha mimba

  • Promethazine
  • Chlorpromazine
  • Opioids
  • Anticonvulsants
  • Diuretics
  • Dawa za kuongeza kiwango cha uzazi
  • Dawa za usingizi

APP tofauti tofauti za kupima mimba kwenye simu

Kuna vipimo vingi ambavyo vinaweza kutumika kupima mimba kwenye simu. Kama vile:

  • Pregnancy PRO
  • Pregancy test Checker
  • easyRead App
  • Pregnancy APP
  • Peanut

Uzuri wa APP hizi ni kuwa kuna kitufe ambacho unaweza kutumia kama unataka kutuma matokeo yako kwa mtu mwingine.Pia teknolojia hii huweza kukumbusha ingawa una miadi ya kumuona daktari wako. Kipimo cha ujauzito kwenye simu kinashauriwa sana lakini ni vyema baada ya kutumia kipimo hiki umwone daktari wako ili aweze kukuelekeza iwapo matokeo ni chanya.

Baadhi ya vipimo humshauri mtu kupima mara mbili au zaidi ili uweze kupata matokeo sahihi.i wapo utapima mara mbili kisha upate matokeo tofauti ni vyema kumuona daktari ili aweze kukupa majibu.

Chanzo: Healthline

Soma Pia:Nani Anapaswa Kuwa Na Mama Katika Chumba Cha Kujifungua?

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Fahamu Njia Tofauti Za Kupima Mimba Nyumbani
Share:
  • Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

    Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

  • Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

    Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

  • Ishara 7 za Mapema za Ujauzito za Kuangazia

    Ishara 7 za Mapema za Ujauzito za Kuangazia

  • Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

    Vyakula 7 Bora Vya Kichefuchefu na Ugonjwa wa Asubuhi

  • Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

    Jinsi ya Kukabiliana na Ugonjwa wa Asubuhi Katika Mimba

  • Ishara 7 za Mapema za Ujauzito za Kuangazia

    Ishara 7 za Mapema za Ujauzito za Kuangazia

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it