Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Kisiwa Cha Zanzibar Kuzungumziwa Kwenye Mitandao Baada Ya Msafiri Wa Kipekee Wa Kike Kukisi Kuwa Alidhulumiwa Kingono Katika Mojawapo Ya Hoteli Huko

2 min read
Kisiwa Cha Zanzibar Kuzungumziwa Kwenye Mitandao Baada Ya Msafiri Wa Kipekee Wa Kike Kukisi Kuwa Alidhulumiwa Kingono Katika Mojawapo Ya Hoteli HukoKisiwa Cha Zanzibar Kuzungumziwa Kwenye Mitandao Baada Ya Msafiri Wa Kipekee Wa Kike Kukisi Kuwa Alidhulumiwa Kingono Katika Mojawapo Ya Hoteli Huko

Kisiwa cha Zanzibar kimekuwa kikizungumziwa kila mahali baada ya mtalii wa kipekee wa kike kukisi kuwa alidhulumiwa kingono huko.

Katika wikendi iliyopita, Kisiwa cha Zanzibar imekuwa ikiongoza kwenye mitandao ya kijamii hasa Twitter kwa sababu zote zisizofaa. Hii ni baada ya mtalii mmoja wa kike kutoka Nigeria kwa jina Zainab Oladehinde kuchukulia mtandao wa kijamii wa Twitter kuhadithia jinsi alivyodhulumiwa kingono alipokuwa katika mojawapo ya mahoteli huko Zanzibar mwaka uliopita.

Kisa cha Zainab katika Kisiwa cha Zanzibar

kisiwa cha zanzibar

Picha: Picha ya kurusa ya twitter

Zainab alielezea jinsi alivyofunga safari kutoka nchi yake ya Nigeria na kuelekea Zanzibar ambapo ni mahali pa utalii panaposifika kwa sana duniani kote. Alikuwa na furaha tele kwani, angesherehekea siku ya kuzaliwa kwake na kuidhinisha kufika umri wa miaka 23 katika mahali pa utalii pa ndoto zake.

Kuamkia siku ya Jumamosi, Zainab aliandika kwenye kurasa yake ya Twitter, “Ni wakati nizungumze kuhusu shuhudio langu katika Zanzibari kama msafiri wa kipekee wa kike. Tukio hili lilifanyika mwaka mmoja uliopita katika mwezi wa Aprili 2021, ila sijaweza kulizungumzia kwani nimekuwa katika tiba ama therapy kwa mwaka mmoja kupona kutokana na kiwewe cha kisaikolojia nilichokipata.”

kisiwa cha zanzibar

Zainab alieleza jinsi ambavyo mtu asiye mfahamu karibia alimbaka kwenye chumba chake cha kulala katika hoteli ya pwani ya Warere huko Zanzibari. Juhudi zake za kupata haki katika kituo cha polisi huko Nungwi hazikufua dafu.

Siku ya kuwasili kwake

kisiwa cha zanzibar

Picha: pexels

Zainab aliwasili katika hoteli hii jioni. Baada ya kuzungumza na jamii na marafiki wake na kuwajuza kuwa aliwasili salama, alizima sitima kisha kulala, kwani alikuwa na uchovu mwingi. Usiku alihisi mtu akimshika na mara ya kwanza kudhani kuwa alikuwa anaota. Alipogutuka usingizini, alifahamu kuwa kulikuwa na mwanamme juu yake aliyekuwa akijaribu kumdhulumu kingono. Aliweza kutoroka alipomwambia kuwa ana virusi vya ukimwi.

Siku iliyofuatia, alienda kuripoti kwenye kituo cha polisi, alipojulishwa kuwa hawawezi kufanya chochote kwani hakubakwa.

Usemi wa hoteli

Katika chapisho ambalo hoteli ilifanya katika mwitikio wa suala hilo. Walisema kuwa ni kweli Zainab alikuwa kwa hoteli yao katika kipindi kilichosemwa. Aliripoti kuwa mfanyikazi wa usalama wa kiume aliingia kwenye chumba chake na kujaribu kulala naye. Katika juhudi zao za kumsaidia Zainab, walimpeleka kwenye kituo cha polisi kuripoti. Alikataa kuendeleza suala hilo kortini na badala yake kuitisha malipo ya kifedha ya taslimu $10,000 kwa uharibifu uliofanyika.

Kauli ya serikali ya Zanzibar

Tume ya utalii ya kisiwa cha Zanzibar ilihakikisha kuwa imefungua utafiti kudadisi zaidi kilichotokea kuhusu kisa hicho cha kujutwa. Utafiti umeanza na ripoti itafanyika, tume ilizidi kusema.

Soma Pia: Zahanati Bora Zaidi Za Uzazi Nchini Kenya

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Kisiwa Cha Zanzibar Kuzungumziwa Kwenye Mitandao Baada Ya Msafiri Wa Kipekee Wa Kike Kukisi Kuwa Alidhulumiwa Kingono Katika Mojawapo Ya Hoteli Huko
Share:
  • Rihanna Amejifungua Mtoto Wa Kiume

    Rihanna Amejifungua Mtoto Wa Kiume

  • Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol

    Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol

  • Ishara 7 Dhabiti Kuwa Mwanamke Anakupenda

    Ishara 7 Dhabiti Kuwa Mwanamke Anakupenda

  • Rihanna Amejifungua Mtoto Wa Kiume

    Rihanna Amejifungua Mtoto Wa Kiume

  • Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol

    Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol

  • Ishara 7 Dhabiti Kuwa Mwanamke Anakupenda

    Ishara 7 Dhabiti Kuwa Mwanamke Anakupenda

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it