Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Klabu ya The Alchemist Imefungwa Baada ya Kushtakiwa Kuwa na Ubaguzi wa Rangi

2 min read
Klabu ya The Alchemist Imefungwa Baada ya Kushtakiwa Kuwa na Ubaguzi wa RangiKlabu ya The Alchemist Imefungwa Baada ya Kushtakiwa Kuwa na Ubaguzi wa Rangi

Klabu ya alchemist imefungwa baada ya video kwenye mitandao kuibuka ikionyesha ubaguzi wa rangi kwenye klabu hiyo.

Klabu maarufu ya The Alchemist Bar iliyoko Westlands Nairobi imefungwa ili upelelezi ufanyike. Hii ni baada ya klabu hii kushtakiwa kuwa na ubaguzi wa rangi. Klabu ya Alchemist yafungwa baada ya Wakenya kuanzisha mada kuwa imekuwa na ubaguzi wa rangi kwa muda sasa.

Kulingana na kauli yao rasmi, uongozi wa klabu hii walisema kuwa hatua hii ni ya muda mfupi ili kuipa serikali ya kaunti ya Nairobi chanya na muda tosha kufanya upepelezi kuhusu mashtaki kuhusu klabu ile.

klabu ya alchemist imefungwa

Kauli yao ilisoma, “Baada ya kushauriana na serikali ya kaunti ya Nairobi, The Alchemist imekubali kufunga milango yake kwa muda huku upelelezi ukifanyika kwa siku chache zijazo.

Usiku wa Mei 20, 2022, video ilitanda kwenye mitandao ya kijamii ambapo Mkenya mmoja alionekana kufurushwa kutoka kwa laini ya wazungu. Video hiyo ilionyesha foleni mbili, moja ya wakenya na nyingine ya wazungu. Mwanamme huyo alipojaribu kujiunga na foleni ya wazungu, alifurushwa vikali na walinda lango.

Video hii imewakasirisha Wakenya ambao hawaamini kuwa ubaguzi wa rangi unatendeka kwa nchi yao. Huku Wakenya wengi wakijitokeza na kusema waliyoyapitia wakiwa kwenye klabu hii.

Gavana wa kaunti ya Nairobi Ann Kananu pia alibatilisha leseni ya klabu hii kuendelea na operesheni zake mjini wa Nairobi.

Klabu hii ilifunguliwa mwaka wa 2015, Disemba 31. Alchemist inamilikiwa na Peng Chen na mchumba wake Michelle Morgan.

klabu ya alchemist imefungwa

Picha: The Alchemist254 Instagram

Walinda lango watafanyiwa upelelezi kudhibitisha wanachostahili kufanyiwa. Kulingana na wasimamizi wa klabu hii, muda huu ambapo wamefunga utawapatia chanya cha kuajiri na kuwapa mafunzo wafanya kazi wapya.

Wakenya wamekuwa na maoni tofauti baada ya kusikia kuwa klabu ya alchemist imefungwa. Wengi wao wakifurahi na kukashifu ubaguzi wa rangi nchini mwao.

Chanzo: Africaparent

Soma Pia: Mavazi ya Watu Mashuhuri Kwenye L’Oreal High Tea Kenya

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Klabu ya The Alchemist Imefungwa Baada ya Kushtakiwa Kuwa na Ubaguzi wa Rangi
Share:
  • Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

    Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

  • Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

    Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

  • Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

    Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

  • Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

    Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

  • Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

    Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

  • Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

    Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it