Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jinsi Ya Kuboresha Ubora Na Idadi Ya Manii Ili Kudumisha Uzalishaji Katika Wanaume!

2 min read
Jinsi Ya Kuboresha Ubora Na Idadi Ya Manii Ili Kudumisha Uzalishaji Katika Wanaume!Jinsi Ya Kuboresha Ubora Na Idadi Ya Manii Ili Kudumisha Uzalishaji Katika Wanaume!

Ni muhimu kwa wanandoa walio katika harakati za kutunga kuwasiliana na mtaalum wa afya ili kupata maarifa kuhusu kuboresha afya ya manii.

Mwanamme anapotoa idadi ndogo ya manii kuliko ilivyo kawaida, huenda akawa na matatizo ya uzalishaji. Kuna mambo kadhaa yanayoathiri uwezo wa uzalishaji wa mwanamme. Tuna angazia jinsi ya kuboresha afya ya manii katika wanaume.

Idadi na ubora wa manii

kuboresha afya ya manii

Wanaume wanavyozidi kuzeeka, ndivyo idadi na ubora wa manii yao unavyozidi kupunguka. Kuna sababu nyingi zinazomfanya mwanamme kuwa na manii yasiyo na ubora. Kama vile kupunguka kwa testosterone kadri mwanamme anavyozidi kuzeeka. Mishipa inayosafirisha manii inapoziba, inafanya iwe vigumu kwa mwanamme kumwaga katika kitendo cha ndoa.

Sababu zinazoathiri ubora wa manii ni kama vile magonjwa ya kingono kama vile kisonono, matibabu hasa yanayolenga prostate gland, shinikizo la damu la juu, kusombwa na mawazo na kisukari.

Uzalishaji katika wanaume unahusiana na afya ya manii na unyevunyevu wa semina. Maji ya semina huwa na manii na virutubisho vingine vinavyo athiri ubora wa manii na uwezo wa kuzalisha mtoto. Uwezo wa kusonga katika manii ni ishara chanya ya uzalishaji.

Tatizo la kutoshaliza katika wanaume husababishwa na mambo kama; utoaji wa idadi ndogo ya manii, manii kushindwa na mwendo, maumbile duni ya manii, mishipa inayosafirisha manii kuziba, magonjwa, uzee kuingia na kadhalika. Wanaume wanapozidi kuzeeka, idadi na ubora wa manii wanayotoa hupunguka, hasa wanapofika umri wa miaka 40.

Jinsi ya kuongeza idadi ya manii

kuboresha afya ya manii

Mfumo wa maisha ambayo mwanamme anaishi unachangia pakubwa katika afya yake ya kijumla na ubora wa manii.

Lishe, ni muhimu kwa mwanamme kuhakikisha kuwa chakula anachokiongeza mwilini. Na kuhakikisha kuwa wakati wote chakula chake kinaongeza virutubisho mwilini. Vyakula kama, maharagwe, samaki, mayai, nyama na viazi.

Mazoezi, yanasaidia katika kuzibua mishipa ambayo huenda ikawa imeziba na kusaidia katika usafirishaji wa manii mwilini.

Kupunguza utumiaji wa vileo. Vileo vina athiri idadi na manii yanayotolewa mwilini. Hasa kwa wanandoa wanaojaribu kutunga mimba, ni vyema kukoma kutumia vileo ili kuboresha manii yanayo tolewa mwilini.

Ni vyema wanaume kujitenga na hali za anga zilizo na joto ya kupindukia kwani zinapunguza ubora wa manii yao.

Kwa wanandoa walio katika harakati zao za kutunga mimba, ni vyema kuwasiliana na mtaalum wa afya na kufanyiwa vipimo kudhibitisha iwapo wana matatizo yoyote na kupata maarifa jinsi ya kuboresha afya ya manii.

Soma Pia: Vidokezo Vya Kukusaidia Kujua Ikiwa Manii Yana Afya Kwa Kuangalia

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Jinsi Ya Kuboresha Ubora Na Idadi Ya Manii Ili Kudumisha Uzalishaji Katika Wanaume!
Share:
  • Sababu 6 Kwa Nini Tumbo Haipunguki Hata Baada ya Kufanya Mazoezi

    Sababu 6 Kwa Nini Tumbo Haipunguki Hata Baada ya Kufanya Mazoezi

  • Tiba za Kinyumbani za Maumivu ya Kichwa Unazopaswa Kujua

    Tiba za Kinyumbani za Maumivu ya Kichwa Unazopaswa Kujua

  • Vyakula 7 Bora Kupigana Dhidi Ya Vidonda Vya Tumbo

    Vyakula 7 Bora Kupigana Dhidi Ya Vidonda Vya Tumbo

  • Sababu 6 Kwa Nini Tumbo Haipunguki Hata Baada ya Kufanya Mazoezi

    Sababu 6 Kwa Nini Tumbo Haipunguki Hata Baada ya Kufanya Mazoezi

  • Tiba za Kinyumbani za Maumivu ya Kichwa Unazopaswa Kujua

    Tiba za Kinyumbani za Maumivu ya Kichwa Unazopaswa Kujua

  • Vyakula 7 Bora Kupigana Dhidi Ya Vidonda Vya Tumbo

    Vyakula 7 Bora Kupigana Dhidi Ya Vidonda Vya Tumbo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it