Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jinsi Ya Kushika Mimba Kwa Kasi Kwa Muda Chini Ya Miezi Miwili

3 min read
Jinsi Ya Kushika Mimba Kwa Kasi Kwa Muda Chini Ya Miezi MiwiliJinsi Ya Kushika Mimba Kwa Kasi Kwa Muda Chini Ya Miezi Miwili

Wanandoa wanaotarajia kushika mimba chini ya miezi miwili wanapaswa kuzingatia vidokezo hivi vya jinsi ya kuboresha uwezo wa kushika mimba kwa kasi.

Makala haya yanazungumzia vidokezo muhimu vya kumsaidia mwanamke aliye katika umri wake wa kupata watoto. Ikiwa unahisi kwamba huu ni wakati bora wa kuanza familia, vidokezo hivi vitakusaidia kuboresha uwezo wa kushika mimba chini ya miezi miwili.

Vidokezo vya kuboresha uwezo wa uzalishaji

kuboresha uwezo wa kushika mimba

  1. Wasiliana na mtaalum wa afya ya kike

Asilimia 40 ya wanawake huwa na nafasi ya kutunga mimba chini ya miezi miwili wanapofanya ngono bila kinga. Kabla ya kuanza juhudi za kushika mimba, ni vyema wakati wowote ule mwanamke kuwasiliana na mtaalum wa afya ya kike. Hasa miezi mitatu hadi sita kabla ya wakati anapopanga kutunga mimba. Vipimo kabla ya kutunga mimba vinamsaidia mwanamke kujua hali yake ya afya na iwapo kuna mabadiliko anayostahili kufanya kabla ya kushika mimba.

Baadhi ya vipimo vinavyofanyika ni kama vile:

Kipimo cha ujumla. Kudhibitisha iwapo wazazi wote wana matatizo yoyote ya kiafya.

Kipimo cha afya ya uzazi. Kipimo cha pap ama pelviki kinafanyika kubaini afya ya uzazi ya mwanamke.

Vipimo vya maambukizi ya kingono. Kutibiwa maambukizi haya kuna boresha nafasi za mwanamke za kutunga mimba.

2. Zingatia afya bora

Kwa wanandoa ambao wangependa kutunga mimba, ni muhimu kuwa makini na afya yao na kuhakikisha kuwa wanazingatia mitindo bora ya kiafya. La kwanza ni kupunguza utumiaji wa vileo na ikiwezekana kuvitupilia mbali. Kisha kujitenga na utumiaji wa sigara. Zina uwezo wa kupunguza nafasi za kutunga mimba kwa kuathiri afya ya mfumo wa uzazi na mishipa ya damu.

3. Kula lishe bora

Ili kuutayarisha mwili kubeba mtoto, mwanamke anastahili kuutunza zaidi na mojawapo ya njia za kufanya hivi ni kwa kula lishe bora. Kuhakikisha kuwa mwili unapata virutubisho tosha. Mbali na mwili wa mama kupata nguvu za kuusaidia kubeba mimba, mtoto atapata virutubisho tosha kumsaidia kukua ipasavyo.

Kupunguza ulaji wa vyakula vilivyo kaangwa kwa mafuta nyingi, vyakula vilivyo na sukari nyingi. Kupunguza ulaji wa wanga nyingi na ngano nyingi pia ni muhimu.

4. Kufanya mazoezi

vyakula vinavyosafisha mirija ya uzazi

Kufanya mazoezi mara kwa mara kunausaidia mwili kustahili safari ya mimba na kujifungua. Mama anashauriwa kufanya mazoezi angalau mara tatu kwa wiki kwa dakika 30-45. Ikiwezekana, kufanya mazoezi kila siku ya wiki ni bora. Mwili unapata nguvu zaidi za kustahimili mabadiliko yanayofanyika katika mimba.

5. Fahamu siku zako za kupevuka kwa yai

Ikiwa ungependa kutunga mimba kwa kasi, fahamu mzunguko wa hedhi na siku ya kupevuka kwa yai. Mara nyingi, hii huwa siku ya kumi na nne baada ya kuanza kwa kipindi chako cha hedhi. Wanandoa wanapofanya mapenzi bila kinga katika siku hii, wana nafasi zaidi za kutunga mimba. Wasiliana na daktari wako ikiwa una tatizika kufahamu siku ya kupevuka kwa yai.

Ni muhimu kwa wanandoa kukumbuka kuwa maisha huwa hayaendi kulingana na mipango yao. Na mara nyingi mambo hufanyika tofauti na tunavyo tarajia. Kuwa wavumilivu na msikate tamaa katika juhudi zenu za kutafuta mtoto na mzidi kutumia mbinu hizi za kuboresha uwezo wa kushika mimba.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Kuharibika Kwa Mimba Na Umuhimu Wa Kusafisha Mji Wa Uzazi

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Trying To Conceive
  • /
  • Jinsi Ya Kushika Mimba Kwa Kasi Kwa Muda Chini Ya Miezi Miwili
Share:
  • Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

    Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

  • Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

    Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

  • Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

    Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

  • Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

    Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

  • Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

    Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

  • Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

    Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it