Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Wazazi Kuchoka Katika Ulezi, Ishara Na Vyanzo Vyake

2 min read
Wazazi Kuchoka Katika Ulezi, Ishara Na Vyanzo VyakeWazazi Kuchoka Katika Ulezi, Ishara Na Vyanzo Vyake

Kuchoka katika ulezi hufanyika mzazi anapozidiwa na mawazo na kuwa na shaka kuhusu jinsi atakavyo tosheleza mahitaji ya watoto wake.

Ulezi sio jukumu rahisi. Mara nyingi, huenda mzazi akahisi kuwa amechoka kihisia, kiakili na kifizikia kufuatia ulezi. Mzazi anapofanya hivi, mara nyingi atajipata akijitenga na watoto wake na marafiki wa karibu. Mzazi anaye tatizika na hali ya kuchoka katika ulezi huenda akasahau vitu, kupuuza majukumu yake ama kufilisika kimawazo.

Mzazi anapokuwa na shaka nyingi kuhusu kutekeleza mahitaji ya watoto wake, huenda akapata tatizo hili. Hasa kufuatia janga la Covid-19 ambapo watu wengi wamesimamishwa makazi zao, huku wengine wakipata mapato yaliyo punguka na hayatoshi kukimu mahitaji yao. Ni kawaida kwa mzazi kuwa na shaka na wasiwasi kuhusu karo ya shule na chakula cha familia yake.

Ishara za kuchoka katika ulezi

kuchoka katika ulezi

  • Uchovu, kuhisi hauna nguvu kila wakati
  • Kujitenga na watu wengine
  • Kuumwa na kichwa wakati wote
  • Kukosa motisha
  • Kukasirika ovyo
  • Kuhisi kana kwamba uko peke yako duniani

Wazazi wanaohisi uchovu huenda wakajipata wakitumia mihadarati na vileo, ili kujituliza akili.

Jinsi ya kukabiliana na tatizo hili

  • Zungumza na mchumba wako

Matatizo mengi hupunguka na kusuluhishwa kwa mazungumzo. Kuzungumza na mchumba wako ni hatua ya kwanza kubwa. Kuwa wazi katika mazungumzo yako na umweleze unachokipitia. Usiwe na hofu kuwa ataona kana kwamba hufurahii kuwa mzazi. Nafasi kubwa ni kuwa utasikiliza na kukusaidia na baadhi ya majukumu ya nyumbani.

  • Pumzika vya kutosha

Kutopata usingizi na mapumziko tosha huwa na athari hasi kwa afya. Hata kama una kazi inayochukua masaa mengi na kisha kuwa na majukumu zaidi ya kinyumbani, ni muhimu kuhakikisha kuwa unapata wakati tosha wa kupumzika. Kulala kwa masaa manane kwa siku kunaimarisha afya yako ya kiakili.

kuchoka katika ulezi

  • Kufanya mazoezi

Mazoezi husaidia katika kupunguza mawazo mengi, kwa hivyo kufanya mazoezi kwa dakika chache kila siku kutapunguza hisia za uchovu kwa walezi.

  • Kuwa na marafiki wa kukuegemeza

Kuwa katika vikundi vya wazazi ni njia bora ya kuwa miongoni mwa watu walio na majukumu sawa nawewe. Kuzungumza nao kuhusu matatizo unayoyapitia kutakusaidia kuhisi kuwa una sikilizwa na maoni yako ni muhimu.

Kuwa mzazi ni hatua moja ya maisha na wala sio jukumu la kipekee. Ni kwa hivyo ni vyema kwa wazazi kuzidi kufanya mambo waliyopendelea kufanya hapo awali na kujitunza. Kumbuka kuwa mzazi asiye jitunza itakuwa vigumu kwake kutunza watoto na familia yake. Hakikisha unajipenda kwanza na kuitunza afya yako ya kihisia, kiakili na kifizikia.

Soma Pia: Je, Unafahamu Mbinu Hatari Ya Ulezi Ya Sharenting?

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Wazazi Kuchoka Katika Ulezi, Ishara Na Vyanzo Vyake
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it