Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jinsi Ya Kudhibiti Hasira Kama Mzazi: Mwongozo Kwa Wazazi Wote

3 min read
Jinsi Ya Kudhibiti Hasira Kama Mzazi: Mwongozo Kwa Wazazi WoteJinsi Ya Kudhibiti Hasira Kama Mzazi: Mwongozo Kwa Wazazi Wote

Imedhihirika kuwa ni vigumu kulewa watoto bila wao kukukasirisha katika wakati mmoja. Kwa sababu hii, ni muhimu kwa mzazi kufahamu jinsi ya kudhibiti hasira yake ili kuepuka matendo atakayojuta baadaye.

Imedhihirika kuwa ni vigumu kulewa watoto bila wao kukukasirisha katika wakati mmoja ama mwingine, ama asilimia 50 ya wakati. Mzazi ni binadamu kama watu wengine. Wana matatizo ya kimaisha, kazi kando na majukumu ya kinyumbani na gharama za kulipa. Kwa hivyo katikati ya nyakati hizi, mtoto wako anaweza kufanya kosa na kufuatia fikira zote mzazi alizonazo, ahisi hasira nyingi. Tazama baadhi ya vidokezo vya kudhibiti hasira yako kama mzazi.

Jinsi Ya Kudhibiti Hasira Yako Kama Mzazi

kudhibiti hasira yako kama mzazi

  1. Tulia kwanza kabla ya hatua

Hasira ni hisia inayowasukuma binadamu kutaka kuchukua hatua kwa kasi. Kwa hivyo, ili kuepuka kuchukua hatua bila kufanya uamuzi wa kina, chukua muda utulie kwanza. Inasaidia kufahamu jinsi ambavyo hasira hufanya kazi na kujikumbusha kupumua ama hata kutabasamu. Kutabasamu ama kuumua kunasaidia kubadili hali ya hisia zako. Kutabasamu hutuma ujumbe kwa ubongo wako kuwa hali sio ya dharura. Kisha mwili wako unaanza kutulia.

Kwa baadhi ya watu, huenda wakahitaji njia ya kutoa hasira zao. Kama kubadili mazingira na kwenda chumbani kingine. Ikiwa wewe ni baadhi ya watu ambao lazima wagonge kitu ili kujituliza, jaribu kugonga mto. Usifanye hivi mbele ya watoto wako.

2. Chukua dakika moja

Unapojipata umekasirishwa na tabia za wanao ukiwa nyumbani, chukua dakika moja uende nje. Hasira huziba fikira za mtu, kwa hivyo chochote ufanyacho dakika hiyo, huenda ukajuta baadaye. Kwa wazazi wengi, hasa wa Afrika, kuna imani kuwa ukimwomba mtoto wako radhi, kuna maana kuwa wewe ni mnyonge na ameshinda. Sio kweli. Kuondoka kunamzungumzia mtoto wako undani wa kosa lake na kuwa unaweza kujidhibiti.

3. Ahirisha kumpa nidhamu

Kumpa mtoto nidhamu sio lazima kuwa dakika moja baada ya kufanya kosa. Hatapotea, na bila shaka hata anapokimbia na kwenda kwa shangazi yake, atarudi kwako jioni. Zungumza naye na umweleze kuwa hujapendelea alichofanya, kisha umweleze kuwa utafikiria kuhusu adhabu utakayo mpa.

kudhibiti hasira yako kama mzazi

4. Chochote kinachofanyika, usimgonge mtoto wako

Ni vigumu kupata mzazi wa kiafrika ambaye hajawahi kumgonga mtoto wake baada ya kukasirishwa. Hili ni la kizazi kijacho, kwa wanaopanga kupata watoto.

Nguvu za kifizikia sio njia bora ya kumpa mtoto wako nidhamu. Huenda ukahisi vyema baada ya kumgonga mtoto na kutoa hasira zako. Badala yake, tumia vidokezo tulivyoangazia hapo awali. Kadri unavyotoa hasira yako kwa kumgonga mtoto wako, ndivyo unavyozidi kuzoea kufanya hizi.

5. Epuka kutumia vitisho

Ni rahisi kufuata mkondo wa kumtishia mtoto wako kila anapokosea na kukukasirisha. Maneno makali kama vile, "nitakuchapa uzirahi, nitakuua leo, utanifahamu leo". Haya ni maneno ambayo wazazi wengi hutumia watoto wanapokosea, ila sio vyema. Kumbuka kuwa maneno unayoyatumia ndiyo watoto wako watakayo yatumia wanapoenda nje ya nyumba yako. Sio sawa.

Hitimisho

Ikiwa baada ya kujaribu haya yote ungali una hasira, inasaidia kukumbuka kuwa, hasira ni njia ya kujikinga ambayo binadamu hutumia kujilinda dhidi ya hisia kama vile hofu ama uwoga. Tafuta chanzo cha hasira. Una hofu ya nini? Nini unachokiogopa? Kufahamu haya kutakusaidia kutulia na kuchukua mkondo tofauti kumpa mtoto wako nidhamu. Hisia hizi zikizidi, mtafute mshauri.

Tengeneza orodha ya njia zinazokubalika za kukabiliana na hasira. Zungumza na watoto wako pia. Wafahamishe kinachokubalika na kisichokubalika. Mnaweza kutengeneza orodha hii kwa pamoja.

Soma Pia: Vidokezo Vya Kuwa Mzazi Bora

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Jinsi Ya Kudhibiti Hasira Kama Mzazi: Mwongozo Kwa Wazazi Wote
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it