Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Siri 7 za Kujikinga Dhidi ya Baridi Nairobi Katika Msimu wa Baridi

2 min read
Siri 7 za Kujikinga Dhidi ya Baridi Nairobi Katika Msimu wa BaridiSiri 7 za Kujikinga Dhidi ya Baridi Nairobi Katika Msimu wa Baridi

Kuvalia soksi na sweta nzito ni muhimu ili kujikinga dhidi ya baridi katika msimu huu wa baridi nchini na kujilinda dhidi ya magonjwa.

Msimu wa baridi nchini huanza mwezi wa sita, saba hadi Agosti. Kujikinga dhidi ya baridi huwa muhimu katika miezi hii ili kujilinda dhidi ya kupata magonjwa.

Wakenya nchini kote wamekuwa wakiteta kuhusu baridi isiyo isha. Msimu wa baridi huandamana na changamoto zake. Tofauti na hapo awali ambapo utawapata watu wengi nje wakifanya shughuli bila kujali kuhusu hali ya anga. Katika msimu huu, watu wengi huwa ndani, ya manyumba ama maofisi zao. Mavazi wanayoyavalia huwa wamedhibitiwa. Lazima yaye mazito yenye joto, tofauti na siku zingine ambapo wanachagua kuvalia mavazi mepesi.

Je, umenunua sweta na soksi?

Tuna angazia siri za kukabiliana na baridi Nairobi katika msimu huu wa baridi.

Jinsi ya kujikinga dhidi ya baridi na kuhakikisha una joto katika msimu wa baridi

Sio kawaida kutoka nje saa nane mchana na kupata kuwa kunakaa kana kwamba kungali asubuhi. Lakini hii ndiyo imekuwa hali yetu kwa miezi michache sasa. Je, tutakabiliana vipi na hali hii na kuhakikisha kuwa tunapata joto na kujilinda dhidi ya baridi na magonjwa?

  1. Vali mavazi yenye joto

kujikinga dhidi ya baridi

Huu sio wakati wa kuvalia blausi nyepesi na kaptura. Hakikisha una sweta nzito. Zinalinda dhidi ya kuhisi baridi na kuhifadhi joto mwilini. Ongeza skafu kwa mavazi yako. Inalinda sehemu ya shingo kutopata baridi na kukupa joto zaidi.

2. Tumia kifaa cha joto ama heater

Kifaa hiki kinasaidia nyumba ama ofisi yako kuwa na joto. Usihisi kana kwamba uko ndani ya jokofu.

3. Pasha chakula na vinywaji joto

kujikinga dhidi ya baridi

Kula ama kunywa vinywaji na vyakula baridi hakushauriwi katika msimu huu. Badala yake, hakikisha kuwa wakati wote unakula vyakula na vinywaji moto. Kwa wanaopenda chai, hakikisha unainywa mara kwa mara, itaupa mwili joto zaidi. Kula mara kwa mara, kunaupa mwili joto baada ya chakula kuchakatwa mwilini.

4. Valia soksi 

Unapokuwa ndani ya nyumba, valia soksi kukupatia joto. Epuka kuvalia viatu wazi unapokuwa nje.

5. Fanya mazoezi

couple exercises

Unapofanya mazoezi, mwili unatoa joto na kuhimiza damu kuzunguka mwilini ipasavyo. Epuka kukaa mahali pamoja kwa muda mrefu bila kufanya lolote.

Baridi inahusishwa na magonjwa ya mfumo wa kupumua kama vile; homa, kukohoa, asthma na pneumonia. Hakikisha kuwa unajilinda na kuwalinda wapendwa wako.

Je, una vidokezo zaidi kuhusu jinsi ya kuhakikisha unapata joto katika msimu huu wa baridi? Tujuze kwa kuwacha ujumbe mfupi.

Chanzo: Africaparent

Soma Pia: Jinsi ya Kutumia Kondomu ya Kiume

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Siri 7 za Kujikinga Dhidi ya Baridi Nairobi Katika Msimu wa Baridi
Share:
  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it