Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Sababu 3 za Kukosa Hedhi Baada ya Kutumia Uzazi wa Mpango

2 min read
Sababu 3 za Kukosa Hedhi Baada ya Kutumia Uzazi wa MpangoSababu 3 za Kukosa Hedhi Baada ya Kutumia Uzazi wa Mpango

Kufanya mazoezi magumu ama kubadilisha lishe na kupoteza uzito wa mwili kwa kasi kunasababisha kukosa hedhi baada ya kutumia uzazi wa mpango.

Uzazi wa mpango huwa njia ya kulinda dhidi ya kupata mimba isiyotarajiwa. Kuna mbinu nyingi za kupanga uzazi, kutumia tembe ama IUD. Tembe za uzazi wa mpango huwa na homoni zinazodhibiti mimba kukua. Mbinu za uzazi wa mpango hudhibiti mzunguko wa hedhi na kipindi cha hedhi kwa miezi ya kwanza kabla ya mwili kuzoea. Mwanamke huenda akakosa kupata kipindi cha hedhi ama kupata kipindi chepesi kuliko ilivyo kawaida. Kipi kinachosababisha kukosa hedhi baada ya kutumia uzazi wa mpango?

Kukosa hedhi baada ya kutumia uzazi wa mpango

  1. Kubadili lishe

kukosa hedhi baada ya kutumia uzazi wa mpango

Kubadili lishe kunaweza kukaathiri hedhi. Kwa mfano kutoka nchi moja hadi nyingine na kubadili vyakula ulivyozoea huenda kukafanya kipindi cha hedhi kupotea kwa muda. Kubadili hedhi na kupoteza uzito wa mwili kwa kasi pia kunaweza kusababisha hedhi kupotea kwa muda.

2. Kufanya mazoezi

kukosa hedhi baada ya kutumia uzazi wa mpango

Kufanya mazoezi magumu isivyo kawaida kutaathiri utenda kazi wa kawaida mwilini na kufanya kipindi cha hedhi kipotee kwa muda. Ikiwa unaanza kufanya mazoezi, anza kwa mazoezi mepesi hadi mwili wako utakapozoea. Wanariadha waliozoea kufanya mazoezi magumu huenda wakakumbana na tatizo hili hasa wanapofanya mazoezi ya kujitayarisha kuenda mashindano.

3. Kusombwa na mawazo

kukosa hedhi baada ya kutumia uzazi wa mpango

Kuwa na mawazo mengi huathiri mwili na ubongo na kufanya iwe vigumu kudhibiti vichocheo mwilini. Kugundua chanzo cha mawazo na kukitatua kutasaidia kusawasisha hedhi.

Kupata mimba ukipanga uzazi

Ni nadra kupata mimba unapokuwa ukitumia uzazi wa mpango. Ikiwa una panga uzazi na kugundua kuwa hujapata kipindi cha hedhi kama ilivyo kawaida, wasiliana na mtaalum wa afya. Ili kuangalia iwapo kuna suala la kiafya linalokutatiza ama una mimba.

Jinsi ya kuhakikisha kuwa hedhi ni ya kawaida

Kukosa kipindi cha hedhi ukitumia uzazi wa mpango sio ishara kuwa una mimba. Mbali, vichocheo mwilini havijasawasishwa. Hata hivyo ni muhimu kuzungumza na daktari ili kuhakikisha kuwa vitu vyote viko sawa. Unaweza kuzingatia vitu hivi:

1. Kufanya mazoezi mara kwa mara. Kunasaidia kusawasisha vichocheo mwilini.

2. Kupunguza mawazo mengi. Kwa kufanya mazoezi mepesi ama yoga, kutembea kwa dakika chache ama kukandwa mwili.

3. Kula lishe yenye afya. Inasaidia kudumisha uzito wa mwili wenye afya. Ikiwa unatatizika kula, wasiliana na daktari wako.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Vitu 6 Vinavyosababisha Kuumwa na Tumbo Bila Hedhi

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Sababu 3 za Kukosa Hedhi Baada ya Kutumia Uzazi wa Mpango
Share:
  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

  • Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

    Vidokezo Vya Ndoa Kwa Kila Mwanamke

  • Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

    Jinsi ya Kudumisha Ulaji wa Vitafunio Vyenye Afya Kazini

  • Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

    Lishe Bora Kwa Wanawake Waliofikisha Umri wa Kukoma Hedhi

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it