Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Je, Nini Chanzo Cha Kukosa Usingizi Kwa Mama Mjamzito?

2 min read
Je, Nini Chanzo Cha Kukosa Usingizi Kwa Mama Mjamzito?Je, Nini Chanzo Cha Kukosa Usingizi Kwa Mama Mjamzito?

Kukosa usingizi kwa mjamzito ni jambo maarufu katika mimba. Haja ya kwenda msalani kila mara na maumivu ya mgongo humkosesha mama usingizi.

Kukosa usingizi kwa mjamzito ni jambo linaloshuhudiwa kwa sana katika safari ya ujauzito. Hasa katika muhula wa mwisho wa mimba, mama mjamzito huwa na vipindi virefu vya kukosa usingizi. Kuna sababu tofauti zinazosababisha hali hii.

Kukosa usingizi kwa mjamzito huchangiwa na:

kukosa usingizi kwa mjamzito

1. Maumivu ya sehemu za mwili kama mgongo na miguu kufuatia kukua kwa mimba na kulegea kwa ligaments

2. Kuhisi hamu ya kwenda msalani mara kwa mara. Kuamka baada ya kila dakika chache usiku hufanya usingizi kupotea na vigumu kulala tena

3. Mapigo ya mtoto tumboni, huenda yakafanya mama atatizike kulala

4. Baadhi ya wanawake hutatizika kutokana na hali ya kiungulia katika mimba, hii ni sababu nyingine ya mama mjamzito kukosa usingizi

5. Katika trimesta ya tatu, utoaji wa kichocheo cha estrogen mwilini huongezeka na kuathiri uwezo wa mama wa kulala vyema usiku

6. Mimba inavyozidi kukua, ndivyo inavyokuwa vigumu kwa mama kulala kwa upande mmoja. Na kumfanya ahisi maumivu na iwe vigumu kwake kulala

7. Mjamzito anapokula chakula kingi kabla ya kulala, huenda akatatizika kupata usingizi

8. Katika muhula wa tatu na wa mwisho wa ujauzito, mjamzito huenda akawa na mawazo na shaka kuhusu kujifungua kwake na kumfanya akose kupata usingizi

Jinsi ya kuboresha usingizi katika ujauzito

kukosa usingizi kwa mjamzito

1.Ili kulala vyema zaidi wakati wa ujauzito, mama aliye na mimba anashauriwa kufanya haya:

2. Kufanya mazoezi mepesi. Matembezi huwa magumu japo mimba inavyozidi kukua. Mazoezi husaidia kupunguza maumivu ya mwili na kumwezesha mama kulala vizuri usiku

3. Kutengeneza ratiba ya kulala. Awe na wakati maalum wa kuingia kitandani na kuamka

4. Kutumia mto wa wajawazito na kuuweka katikati ya miguu humsaidia mama kulala vyema zaidi

5. Kuepuka kutumia simu na vifaa vingine vya kielektroniki usiku

6. Kuepuka kunywa vinywaji vilivyo na kaffeini kama soda na kahawa usiku kabla ya kulala

7. Kutokula chakula kingi muda mfupi kabla ya kuingia kitandani

8. Kuhakikisha kuwa chumba cha kulala ni kisafi, kimetulia na hakina mwangaza mwingi usiku

Soma Pia: Mabadiliko Mwilini Mama Anapokuwa Na Mimba Ya Mwezi Mmoja

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Je, Nini Chanzo Cha Kukosa Usingizi Kwa Mama Mjamzito?
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it