Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mambo Ya Kufanya Baada Ya Kuwachwa Na Mchumba Wako!

2 min read
Mambo Ya Kufanya Baada Ya Kuwachwa Na Mchumba Wako!Mambo Ya Kufanya Baada Ya Kuwachwa Na Mchumba Wako!

Sio jambo rahisi kuendelea na maisha yako baada ya kutengana na mchumba wako, ila kufanya vitu hivi kuta kusaidia kupona haraka.

Mapenzi yanapo noga, ni vigumu kufikiria kuhusu kitakacho tendeka wakati wewe na mchumba wako mtakapo achana. Mapenzi kweli ni kitu kizuri na sote tuna stahili kupata nafasi ya kupenda na kupendwa. Ila pale ambapo mambo huenda mrama na kuwafanya wapenzi kutengana. Hiki huwa kipindi cha kuhuzunisha na chenye maumivu mengi kwa wachumba walo kuwa katika mapenzi pamoja. Na kutengana kunapo fanyika, hakuna jambo unalo weza kufanya katika hatua hii. Ni vyema kufahamu jinsi ya kukumbana na kuwachwa na kumsahau mpenzi wako wa awali.

Vidokezo vya jinsi ya kumsahau mpenzi wako wa awali

Mambo Ya Kufanya Baada Ya Kuwachwa Na Mchumba Wako!

 

Ni muhimu kwako kujua jinsi ya kukabiliana na kuachwa katika uhusiano, jinsi ya kukabiliana na hili na kuendelea na maisha yako bila kuchukua muda mrefu sana ukiomboleza.

  1. Usisisitize kupatana mara ya mwisho

Kosa moja maarufu sana kwa wachumba walio tengana ni kusisisitiza kupatana ili mzungumze kuhusu kilicho sababisha kutengana kwenu. Hili huwa jambo mbaya na kamwe halishauriwi.

Kufanya hivi kutakufanya uendelee kushikilia hisia za hapo awali, za nyakati nzuri na uchungu ulio pitia. Na kurefusha wakati wako wa kupona baada ya kutengana.

2. Kulia sio hatia

Usiwasikize watu wanao sema kuwa, haupaswi kulia kwa sababu wewe ni mtu mzima. Watu wazima pia wana hisia na huumia wanapo tendwa. Kulia ni mojawapo ya njia ya kukubali kilicho tendeka na hatua ya kwanza ya safari yako ya uponaji.

3. Rudia maisha yako asili

exercise at home during coronavirus

Badala ya kujaribu kurudiana na mchumba wako wa hapo awali, wakati ambapo ashafunga kurasa yako, tia juhudi kurejesha maisha yako mahali yalipo kuwa.

Fanya vitendo vinavyo kufurahisha kama vile kusoma kitabu, kujumuika na marafiki zako wanapo safiri, kujiunga na darasa la mazoezi na kadhalika.

4. Kata mawasiliano yao

Unapo wasiliana na mchumba wako wa hapo awali, nafasi kubwa ni kuwa hisia za hapo awali zita anza kurudi. Kwa hivyo, hakikisha kuwa hauzungumzi nao tena. Kupitia kwa njia yoyote ile ambayo mlikuwa mna wasiliana hapo awali.

5. Jitahini

Huenda ukawa unamchukia sana mchumba wako wa hapo awali katika kipindi hiki. Lakini kwa kusema ukweli, baadhi ya wakati, huenda ikawa sisi ndiyo tuliokosea. Je, kuna kitu ulicho kosea ambacho ungefanya vitofauti? Kuna mambo uliyo soma kutoka kwa uhusiano huo? Katika uhusiano wako mpya, ni yapi ungependa kufanya kwa njia tofauti?

Ni vyema kujiuliza maswali haya, kwani baada ya muda utaingia kwa uhusiano mpya na itakuwa vyema kufanya uamuzi bora.

Soma Pia: Jinsi Kufikiria Sana Kutakavyo Haribu Uhusiano Wako

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Mambo Ya Kufanya Baada Ya Kuwachwa Na Mchumba Wako!
Share:
  • Jinsi Ya Kuachana Na Mtu Unaye Mpenda

    Jinsi Ya Kuachana Na Mtu Unaye Mpenda

  • Mahali Bora Zaidi Pa Kupatana Na Mchumba Wako!

    Mahali Bora Zaidi Pa Kupatana Na Mchumba Wako!

  • Utafiti: Wanaume Huumia Zaidi Baada Ya Kutengana Na Wachumba Wao

    Utafiti: Wanaume Huumia Zaidi Baada Ya Kutengana Na Wachumba Wao

  • Mambo 5 Ya Kufanya Mchumba Wako Anaposema Vitu Vya Kuumiza

    Mambo 5 Ya Kufanya Mchumba Wako Anaposema Vitu Vya Kuumiza

  • Jinsi Ya Kuachana Na Mtu Unaye Mpenda

    Jinsi Ya Kuachana Na Mtu Unaye Mpenda

  • Mahali Bora Zaidi Pa Kupatana Na Mchumba Wako!

    Mahali Bora Zaidi Pa Kupatana Na Mchumba Wako!

  • Utafiti: Wanaume Huumia Zaidi Baada Ya Kutengana Na Wachumba Wao

    Utafiti: Wanaume Huumia Zaidi Baada Ya Kutengana Na Wachumba Wao

  • Mambo 5 Ya Kufanya Mchumba Wako Anaposema Vitu Vya Kuumiza

    Mambo 5 Ya Kufanya Mchumba Wako Anaposema Vitu Vya Kuumiza

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it