Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Je, Kumshika Mtoto Mchanga Sana Kunamfanya Aharibike?

2 min read
Je, Kumshika Mtoto Mchanga Sana Kunamfanya Aharibike?Je, Kumshika Mtoto Mchanga Sana Kunamfanya Aharibike?

Ni kawaida kusikia wazazi wapya wakiambiwa kuwa kumshika mtoto sana kunamharibu. Ila, utafiti una dhihirisha jambo tofauti.

Kila mtoto anapolia, unampakata na baadhi ya wakati huenda ukawa unamshika zaidi kuliko unavyomlaza. Mara nyingi mzazi mpya anapofanya hivi, atasikia mamake mzazi ama mtu mwingine aliye na watoto wakubwa akimkemea. Na kumwambia kuwa kufanya hivyo kunamdekeza mtoto. Usimshike mtoto sana, unamharibu, mzazi mpya atasikia akiambiwa mara nyingi. Je, ni kweli kuwa kumshika mtoto sana kunamharibu?

Kumshika mtoto kunamdekeza?

kumshika mtoto sana kunamharibu

Hii ni imani isiyo ya kweli inayozidi kupitishwa kwa vizazi. Hata baada ya utafiti unaoegemezwa na wataalum kuwa huwezi kumharibu mtoto mchanga, wazazi bado wanazidi kushikilia imani kuwa kumpakata mtoto sana kunamdekeza. Masomo yaliyofanyika katika nyanja hii yamedhihirisha kuwa kumshika mtoto kwa muda mrefu kunapunguza mara anazolia.

Hakuna uwezekano wa kumharibu mtoto mchanga kwani akili yake ingali inakua na haelewi kinacho endelea.

Mzazi anapaswa kumwacha mtoto alie bila kumshika?

Wazazi wa hapo awali waliamini kuwa mtoto hapaswi kupakatwa mara tu anapolia. Anastahili kuwachiliwa alie kwa muda. Kulingana na utafiti, watoto waliowachwa kulia kwa muda kabla ya kupakatwa hawakuwa na matatizo ya kulia kwa sana walipotengana na wazazi wao katika umri wa mwaka mmoja. Hata hivyo, ni vigumu kwa wazazi hasa wa mara ya kwanza kuwaacha watoto wao walie kwa kipindi kirefu.

Kushughulikia mahitaji ya mtoto mchanga sio kumharibu

kumshika mtoto sana kunamharibu

Ni vyema kushughulikia mahitaji ya mtoto anapotaka na katika umri huo mchanga, sio kumharibu, mbali ni kumpa anachohitaji. Mama anapoelewa kila kilio cha mtoto na maana yake anaweza kufahamu mtoto anachotaka. Kuna kilio cha uchovu, cha njaa na cha kubadilishwa nepi.

Mtoto anapofikisha miezi sita kisha kuendelea kudekezwa, ana nafasi za juu za kuharibika. Katika umri huu, ni vyema kwa mama kufahamu mahitaji ya kimsingi na yasiyo ya kimsingi na kupunguza kumpatia vitu ambavyo sio vya kimsingi. Ili kupunguza nafasi za kumdekeza na kumharibu.

Mtoto angali mchanga, mama hapaswi kuwa na wasiwasi kuwa kumshika mtoto sana kunamharibu hasa kila mara anapolia ama kumnyonyesha mara kwa mara. Kumshika na kuwa na mguso wa ngozi kunasaidia kuboresha utangamano kati ya mzazi na mwanawe.

Chanzo: WebMd

Soma Pia: Kuwatenganisha Watoto: Faida Na Hasara Za Kujifungua Mtoto Wa Pili Baada Ya Miaka Fulani

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Parenting
  • /
  • Je, Kumshika Mtoto Mchanga Sana Kunamfanya Aharibike?
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it