Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Vitu 6 Vinavyo Fanya Safari Ya Ujauzito Iwe Rahisi Zaidi

3 min read
Vitu 6 Vinavyo Fanya Safari Ya Ujauzito Iwe Rahisi ZaidiVitu 6 Vinavyo Fanya Safari Ya Ujauzito Iwe Rahisi Zaidi

Ujauzito unavyo zidi kukua, mama huenda akaanza kuumwa na miguu. Ni vyema kuwa na viatu vyenye starehe na saizi moja kubwa kuliko viatu vyake vya kawaida.

Ujauzito ni kipindi kilicho jazwa na furaha, mapenzi, kugundua mambo mapya na pia kina changamoto zake. Mwili wa mama unabadilika kwa njia nyingi. Uterasi inavyo zidi kukua na kuwa kubwa, ndivyo mama anavyo zidi kutatizika kufanya baadhi ya majukumu. Anaweza tatizika kulala. Kuna baadhi ya vitu vinavyo tumika kurahisisha safari ya ujauzito. Soma zaidi!

Kurahisisha Safari Ya Ujauzito

kurahisisha safari ya ujauzito

  1. Vitamini za kabla ya kujifungua

Vitamini hizi ni muhimu kwa mama ili atimize kiwango kinacho hitajika cha vitamini cha kila siku. Ni vigumu kupata virutubisho vyote na idadi tosha kutoka kwa vyakula ambavyo mama anakula kwa siku. Tembe za vitamini zinamsaidia kupata virutubisho vyote. Pia zinasaidia katika ukuaji wa mtoto na kumwepusha mtoto kutokana na changamoto ya maumbile.

2. Mto wa ujauzito wa kulalia

Ujauzito ni safari ya kupendeza ila huandamana na changamoto zake. Mojawapo ya changamoto zilizoko ni kutatizika kulala. Tumbo la mama linazidi kukua na kuifanya iwe vigumu kwake kupata namna ya kulala kwa starehe. Kuna mito maalum ya wanawake wajawazito. Mto huu unawekwa katikati ya miguu na chini ya tumbo na kumwezesha mama kulala kwa starehe zaidi.

3. Sindiria mpya

Ujauzito huandamana na mabadiliko mengi mwilini. Kama vile matiti ya mama kuongezeka kwa saizi. Mama anahitaji kuwa na sindiria zinazomtoshea vizuri katika safari ya ujauzito. Kuna sindiria za ujauzito, spesheli za wakati mama anapokuwa na mimba na hata anaponyonyesha mtoto.

kurahisisha safari ya ujauzito

4. Mavazi ya ujauzito

Mwanamke huongeza uzito na kuwa mnene anapokuwa na mimba. Kwanza, uzito wa mtoto kisha anakula chakula zaidi katika kipindi hiki. Mambo yanayomfanya kuwa mnene kuliko alivyo kwa kawaida. Ni muhimu kwa mama kuhakikisha kuwa anavalia mavazi yasiyom-bana, tumbo ama sehemu nyingine. Mavazi bora kuvalia katika kipindi hiki ni rinda ama suruali za mama mjamzito.

5. Viatu vyenye starehe

Ujauzito unavyo zidi kukua, mama huenda akaanza kuumwa na miguu. Ni vyema kuwa na viatu vyenye starehe na saizi moja kubwa kuliko viatu vyake vya kawaida. Huu sio wakati wa mama kuvalia viatu vyenye visigino virefu, atashinikiza miguu yake ama kuanguka na kujiumiza. Huu ni wakati wa kuvalia viatu vyenye starehe kwake.

6. Krimu ya kupunguza alama za kunyooka

Mwili hupata alama za kunyooka mtu anapo kuwa mnene ama kukonda kwa kasi. Tumbo la mama hukua kubwa kadri siku zinavyo zidi kusonga na kumfanya apate alama za kunyooka. Kupaka krimu za kudhibiti athari za alama hizi kunasaidia ngozi yake izidi kupendeza. Mama anashauriwa kuanza kujipaka krimu hii punde tu anapofahamu hali yake ya mimba.

Chanzo: healthline

Soma Pia: Vidokezo Vya Kuwa Mama Mwema Kwa Watoto Wako: Sifa 5 Za Mama Mwema

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Uncategorized
  • /
  • Vitu 6 Vinavyo Fanya Safari Ya Ujauzito Iwe Rahisi Zaidi
Share:
  • Mabadiliko Mwilini Mwa Mama Baada ya Kujifungua

    Mabadiliko Mwilini Mwa Mama Baada ya Kujifungua

  • Mabadiliko 5 ya Mwili Usiyotarajia Baada ya Kujifungua

    Mabadiliko 5 ya Mwili Usiyotarajia Baada ya Kujifungua

  • Kukandwa Baada ya Kujifungua Kuna Manufaa Gani Kwa Mama

    Kukandwa Baada ya Kujifungua Kuna Manufaa Gani Kwa Mama

  • Mabadiliko Mwilini Mwa Mama Baada ya Kujifungua

    Mabadiliko Mwilini Mwa Mama Baada ya Kujifungua

  • Mabadiliko 5 ya Mwili Usiyotarajia Baada ya Kujifungua

    Mabadiliko 5 ya Mwili Usiyotarajia Baada ya Kujifungua

  • Kukandwa Baada ya Kujifungua Kuna Manufaa Gani Kwa Mama

    Kukandwa Baada ya Kujifungua Kuna Manufaa Gani Kwa Mama

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it