Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Mwanamke Anapaswa Kufanya Tendo La Ndoa Mara Ngapi Ili Kushika Mimba?

2 min read
Mwanamke Anapaswa Kufanya Tendo La Ndoa Mara Ngapi Ili Kushika Mimba?Mwanamke Anapaswa Kufanya Tendo La Ndoa Mara Ngapi Ili Kushika Mimba?

Mwanamke ana uwezekano wa kushika mimba baada ya tendo la ndoa baada ya muda upi? Kuna uwezekano wa kushika mimba baada ya kufanya mapenzi mara moja?

Kuna uhusiano mkubwa kati ya umri wa mwanadada na uzalishaji wake wa uzazi. Kadri mwanamke anavyozidi kuzeeka, ndivyo uwezo wake wa kupata mtoto unavyopunguka. Umri bora zaidi wa kubeba mtoto ni chini ya miaka 35. Baada ya umri huu, nafasi za kushika mimba kiasili hupunguka. Huchukua muda upi kushika mimba baada ya tendo la ndoa?

Wakati bora kutunga mimba

kushika mimba baada ya tendo la ndoa

Mwanamke huwa na siku sita katika kila mzunguko wa hedhi kila mwezi wa kushika mimba kwa urahisi. Siku ya kupevuka kwa yai huwa bora kwa mwanamke kushika mimba kwa urahisi. Ikiwa mwanamke hana uhakika wa siku yake ya kupevuka kwa yai, anaweza kuwasiliana na daktari wake ama kutumia kifaa cha kubaini siku hii. Baadhi ya mabadiliko yanayo fanyika mwilini katika kipindi hiki ni:

  • Ute kuongezeka
  • Maumivu kwenye tumbo
  • Matiti kuwa laini
  • Kubadilika kwa kizazi
  • Mabadiliko ya temprecha mwilini

Unapaswa kufanya ngono mara ngapi kushika mimba?

Kufanya ngono mara moja katika siku ambapo mwanamke anarutuba zaidi kunaongeza nafasi zake za kushika mimba. Kuwasiliana na mtaalum wa afya katika kipindi hiki ni bora zaidi ili awashauri kuhusu mara mnazopaswa kujihusisha katika tendo la ndoa.

Kuna uwezekano wa kushika mimba baada ya kufanya ngono mara moja

Naam. Ikiwa mwanamke alifanya tendo la ndoa siku alipokuwa na rutuba zaidi bila maarifa yake, bila shaka atapata mimba. Ni vyema wakati wote kutumia kinga iwapo hauko tayari kuwa mzazi.

Inachukua muda upi kushika mimba baada ya tendo la ndoa

kushika mimba baada ya tendo la ndoa

Huenda ikachukua hadi siku tano kwa manii na yai kupatana. Kisha siku kati ya sita hadi kumi kwa yai lililorutubishwa kujipandikiza kwenye kuta za uterasi. Kisha safari ya ujauzito kuanza.

Kuboresha rutuba

Wanandoa wanaweza boresha rutuba ili kuwasaidia kushika mimba kwa urahisi kwa kufanya mambo yafuatayo.

Kuzingatia lishe bora. Iliyo na virutubisho muhimu, hakikisha kuwa lishe ina protini tosha.

Kuwa na uzito wa wastani. Uzito wenye afya huifanya rahisi kwa wanandoa kushika mimba kwa urahisi.

Kukoma kutumia bidhaa zilizo na nicotine nyingi kama sigara.

Kufanya mazoezi. Mazoezi yana saidia kuzibua mishipa inayosafirisha manii na kumfanya mwanamke kuwa na afya bora, hivi basi kuboresha uzalishaji wake.

Kufanya tendo la ndoa mara kwa mara ili kuongeza nafasi za wanandoa kushika mimba kwa urahisi.

Soma pia: Umuhimu Wa Mazoezi Ya Kuleta Uchungu Wa Uzazi Katika Ujauzito

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Becoming a Mama
  • /
  • Mwanamke Anapaswa Kufanya Tendo La Ndoa Mara Ngapi Ili Kushika Mimba?
Share:
  • Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

    Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

  • Njia 5 za Kujitayarisha kwa Uchungu wa Mama

    Njia 5 za Kujitayarisha kwa Uchungu wa Mama

  • Vitu Vya Kufanya Kabla ya Kuenda Hospitali Kujifungua

    Vitu Vya Kufanya Kabla ya Kuenda Hospitali Kujifungua

  • Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

    Vidokezo 5 vya Kupata Mimba kwa Wanandoa Wanaolenga Kuwa Wazazi

  • Njia 5 za Kujitayarisha kwa Uchungu wa Mama

    Njia 5 za Kujitayarisha kwa Uchungu wa Mama

  • Vitu Vya Kufanya Kabla ya Kuenda Hospitali Kujifungua

    Vitu Vya Kufanya Kabla ya Kuenda Hospitali Kujifungua

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it