Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Jinsi Ya Kuongeza Nafasi Ya Kushika Mimba Kwa Urahisi Katika Miaka Ya 30's

3 min read
Jinsi Ya Kuongeza Nafasi Ya Kushika Mimba Kwa Urahisi Katika Miaka Ya 30'sJinsi Ya Kuongeza Nafasi Ya Kushika Mimba Kwa Urahisi Katika Miaka Ya 30's

Mwanamke anaweza kuongeza nafasi zake za kushika mimba katika umri wa 30's kwa kuhakikisha kuwa anakula lishe bora na kufanya mazoezi.

Wanawake zaidi wanaamua kuwa wazazi katika miaka ya 30's. Kuna imani kuwa mwanamke hawezi tunga mimba katika miaka yake ya 30's, hiyo ni imani tu. Hata hivyo, nafasi zake za kutunga mimba zinapunguka na huenda akachukua muda zaidi. Hata hivyo, anaweza kuongeza nafasi zake za kushika mimba katika umri wa 30's kwa kufanya hivi!

Kushika Mimba Katika Umri Wa 30's

  • Kula lishe bora

kula mboga katika ujauzito

Lishe ni ina jukumu kubwa katika kumsaidia mwanamke kutimiza lengo la kushika mimba. Kuna baadhi ya vyakula vinavyo msaidia mwanamke kushika mimba kwa kasi. Hakikisha kuwa sahani yako ina mboga na matunda, pia punguza ulaji wa vitamu tamu, vyakula vilivyo chakatwa na vyenye ufuta mwingi.

  • Koma kutumia vileo na kuvuta sigara

kushika mimba katika umri wa 30s

Sigara na vileo vimedhihirishwa kupunguza nafasi za wanawake kujifungua kwa urahisi. Katika wanaume, sigara na pombe zinapunguza idadi ya manii na hivyo basi kupunguza uwezo wao wa kuzalisha mkewe. Kushika mimba kunafuzu kufuatia juhudi za mwanamke na mwanamme. Kwa hivyo wachumba wanapaswa kupunguza utumiaji wa sigara na pombe.

  • Koma kutumia uzazi wa mpango

kushika mimba katika umri wa 30s

Baadhi ya mbinu za kupanga uzazi huchukua muda kabla ya homoni mwilini kurudi kawaida. Hasa mbinu za kupanga uzazi zenye homoni. Mwanamke anaye jaribu kutunga mimba anapaswa kukoma kutumia uzazi wa mpango. Wasiliana na daktari wako, anaweza shauri dawa za kusaidia kurejesha viwango vya homoni mwilini kawaida.

  • Kudhibiti mawazo

Jinsi Ya Kuongeza Nafasi Ya Kushika Mimba Kwa Urahisi Katika Miaka Ya 30s

Maisha yana changamoto nyingi na ni vigumu kuto sombwa na mawazo katika wakati mmoja maishani. Mawazo ya kikazi, kifamilia, uhusiano ama gharama ya maisha kwa jumla. Kusombwa na mawazo kuna athari hasi mwilini na kupunguza nafasi za mama anaye tamani kushika mimba kwa kufanya iwe vigumu kwake kutimiza malengo yake.

  • Wasiliana na mtaalum wa afya ya kike

jinsi ya kutoa mimba ya wiki mbili

Kumtembelea mtaalum wa afya ya kike kabla ya kuanza juhudi za kushika mimba ni muhimu. Atafanya vipimo kuhakikisha kuwa mwanamke hana matatizo ya kiafya. Na iwapo ana matatizo ya kiafya, atamshauri anacho paswa kufanya ili kumsaidia kushika mimba kwa urahisi. Kliniki ni muhimu hata baada ya kushika mimba ili kufuatilia ukuaji wa mtoto na kukabiliana na matatizo yoyote ya kiafya.

  • Fanya mazoezi

kushika mimba katika umri wa 30s

Mazoezi ni muhimu katika umri wowote ule na kwa kila mtu. Ila, kwa mwanamke anayetaka kushika mimba, mazoezi ni muhimu sana. Kufanya mazoezi kunaupa mwili nguvu za kustahimili safari ya ujauzito. Misuli ya pelviki inapata nguvu za kumwezesha mama kujifungua kwa urahisi. Hata baada ya kushika mimba, mwanamke anahimizwa kuzidi kufanya mazoezi ili kupunguza maumivu ya mwili na kumwezesha kulala vizuri. Ni rahisi kwa mama anayefanya mazoezi kupunguza uzani wa mwili baada ya kujifungua.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Hatari Na Faida Za Kushika Mimba Baada Ya Miaka 35

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Trying To Conceive
  • /
  • Jinsi Ya Kuongeza Nafasi Ya Kushika Mimba Kwa Urahisi Katika Miaka Ya 30's
Share:
  • Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

    Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

  • Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

    Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

  • Vyakula Vya Rutuba: Kula Vyakula Hivi Ikiwa Unajaribu Kushika Mimba

    Vyakula Vya Rutuba: Kula Vyakula Hivi Ikiwa Unajaribu Kushika Mimba

  • Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

    Kufanya Mapenzi Kupata Mimba: Mambo 9 Wanandoa Wanapaswa Kujua

  • Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

    Mabadiliko 10 ya Kufanya Kabla ya Kupata Mimba

  • Vyakula Vya Rutuba: Kula Vyakula Hivi Ikiwa Unajaribu Kushika Mimba

    Vyakula Vya Rutuba: Kula Vyakula Hivi Ikiwa Unajaribu Kushika Mimba

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it