Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Sababu 5 Kwa Nini Kupunguza Uzito wa Mwili Kunakutatiza Licha ya Kufanya Mazoezi Siku Tano Kwa Wiki

2 min read
Sababu 5 Kwa Nini Kupunguza Uzito wa Mwili Kunakutatiza Licha ya Kufanya Mazoezi Siku Tano Kwa WikiSababu 5 Kwa Nini Kupunguza Uzito wa Mwili Kunakutatiza Licha ya Kufanya Mazoezi Siku Tano Kwa Wiki

Kula chakula duni, kufanya mazoezi yasiyofaa na mtindo duni wa maisha huchangia katika kutatizika kupunguza uzito wa mwili.

Kutatizika kupunguza uzito kunakusumbua, licha ya kufanya mazoezi kila siku ya wiki? Kipi kinachosababisha kukosa kupunguza uzito wa mwili?

Vyanzo vya Kutatizika Kupunguza Uzito wa Mwili

  1. Chakula

kutatizika kupunguza uzito wa mwili

Chakula unachokila huchangia pakubwa katika kupunguza ama kuongeza uzito licha ya kufanya mazoezi. Ikiwa unakula chakula kisicho na afya, haijalishi masaa unayofanya mazoezi kwa siku. Ukweli ni kuwa, hautaona tofauti yoyote kwenye inchi za kiuno. Huenda zikaongeza hata.

Ikiwa lengo lako ni kupunguza uzito, lazima uangazie kalori unazotia mwilini. Punguza kiwango cha kalori unachokila. Zingatia kula kiwango kidogo cha kalori ikilinganishwa na nishati unayotumia kila siku. Pia, hakikisha kuwa unakula tu unapohisi njaa.

Jitenge na ulaji wa vitamu tamu vilivyo chakatwa, badala yake, kula njugu. Punguza ulaji wa vitu vilivyokaangwa kwa ufuta mwingi kama vile vibanzi.

2. Mtindo wako wa maisha

kutatizika kupunguza uzito wa mwili

Kupunguza uzito wa mwili huwa juhudi za vitu vingi tofauti. Kufanya mazoezi na kuwa na mtindo duni wa maisha hakutakuwa na faida zozote.  Mtindo wa maisha huchangia pakubwa katika kupunguza ama kuongeza uzito licha ya kufanya mazoezi magumu kila siku. Kutopata usingizi tosha kwa siku na kusombwa na mawazo husababisha kutopunguza uzito. Unaposombwa na mawazo, huenda ukatamani kula chakula kisicho na afya ili kujituliza. Unywaji wa pombe ili kupunguza fikira nyingi pia kutapunguza juhudi zako za kupunguza uzito.

3. Mazoezi

kuboresha ashiki

Ikiwa unafanya mazoezi na huoni mabadiliko yoyote, angalia mazoezi unayo yafanya. Usifanye cardio na kukimbia peke yake, hakikisha kuwa unainua chuma ama uzito pia.

4. Maumbile na jeni

Ikiwa umezaliwa katika familia ambapo kuna watu wanene. Huenda ikakuchukua muda zaidi ikilinganishwa na watu wengine kupunguza uziyo. Usikate tamaa na kutupilia mbali ufanyaji wa mazoezi. Badala yake,  zidisha juhudi zako na uwe mtulivu.

5. Homoni

Uvimbe baada ya kujifungua ni kawaida na sio jambo la kukutia shaka. Ila pale ambapo uvimbe huu unaandamana na ishara za hatari

Homoni huashiria akili kupunguza uzito. Ikiwa homoni za cortisol na thyroid hazifanya kazi ipasavyo, kupunguza uzito wa mwili kutakutatiza. Kuwa na hali za kiafya kama uzito zaidi, shinikizo la juu la damu na kisukari hutatiza upunguzaji wa kilo mwilini.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Jinsi Ya Kupunguza Uzito Wa Mwili Kwa Kutumia Lishe Ya Alkaline

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Sababu 5 Kwa Nini Kupunguza Uzito wa Mwili Kunakutatiza Licha ya Kufanya Mazoezi Siku Tano Kwa Wiki
Share:
  • Wanawake Kusombwa na Mawazo Katika Kipindi Cha Hedhi

    Wanawake Kusombwa na Mawazo Katika Kipindi Cha Hedhi

  • Koma Tabia Hizi Duni Za Lishe

    Koma Tabia Hizi Duni Za Lishe

  • Kutofautisha Endometriosis na Hedhi: Ishara Kuu za Endometriosis

    Kutofautisha Endometriosis na Hedhi: Ishara Kuu za Endometriosis

  • Wanawake Kusombwa na Mawazo Katika Kipindi Cha Hedhi

    Wanawake Kusombwa na Mawazo Katika Kipindi Cha Hedhi

  • Koma Tabia Hizi Duni Za Lishe

    Koma Tabia Hizi Duni Za Lishe

  • Kutofautisha Endometriosis na Hedhi: Ishara Kuu za Endometriosis

    Kutofautisha Endometriosis na Hedhi: Ishara Kuu za Endometriosis

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it