Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Sababu 5 Za Kutoka Damu Wakati Wa Mimba Changa

2 min read
Sababu 5 Za Kutoka Damu Wakati Wa Mimba ChangaSababu 5 Za Kutoka Damu Wakati Wa Mimba Changa

Kutoka damu nyepesi wakati wa mimba changa sio chanzo cha wasiwasi. Damu inapogeuka na kuanza kutoka kwa matone makubwa, ni ishara kuwa kuna jambo hasi linalotendeka.

Kuvuja damu nyepesi isiyojaza pedi kwa siku moja ama mbili sio kisa cha shaka katika safari yako ya ujauzito. Ila, kuvuja damu huku kunapozidi kwa zaidi ya siku mbili na kwa kiwango kikubwa, ni muhimu kwenda kwenye kituo cha afya.

Sababu za kutoka damu wakati wa mimba changa

kutoka damu wakati wa mimba changa

  1. Damu baada ya yai kujipachika kwenye uterasi

Kitendo hiki kwa Kisayansi kinafahamika kama implantation. Ambapo yai lililorutubishwa linajipandikiza kwenye ukuta wa kizazi. Kutoa damu nyepesi kati ya siku 6 - 12 baada ya kufanya kitendo cha ngono ni ishara kuwa yai limejipandikiza kwenye ukuta wa uterasi. Damu ya kujipachika kwa yai huwa nyepesi na huisha ndani ya siku tatu. Tazama tofauti kati ya damu ya hedhi na ya implantation hapa.

2. Kuvuja damu baada ya tendo la ndoa

Kitu chochote kinachoingia ukeni wa mwanamke anapokuwa na mimba kinaweza kumjeruhi na kumfanya avuje damu. Kwa baadhi ya wanawake, wanapofanya tendo la ndoa, wao huvuja damu nyepesi. Huisha baada ya muda mfupi.

jinsi ya kujua kuwa una mimba

3. Kuharibika kwa mimba

Nafasi za kupoteza mimba huwa zaidi katika mimba ya chini ya miezi mitatu. Kuvuja damu inayogeuka na kuwa mabonge makubwa ni ishara kuwa mama anapoteza ujauzito. Kutokwa na mabonge ya damu kuna ambatana na maumivu makali ya mgongo na tumbo ya chini, na kuhisi kichefuchefu.

4. Mimba kutunga nje ya kizazi

Mimba ya ectopic inafanyika pale ambapo yai linajipandikiza nje ya mji wa mimba na mara nyingi kujipandikiza kwenye mirija ya uzazi. Ishara za kuwa na mimba ya ectopic ni kama vile kutokwa na damu nyepesi, kuumwa na tumbo vikali na maumivu ya mara kwa mara.

5. Kuwa na mimba ya mapacha

Mama aliye na mimba ya mapacha ana nafasi zaidi za kutokwa na damu nyepesi. Damu hii huisha baada ya muda.

Kutoka damu nyepesi wakati wa mimba changa sio chanzo cha wasiwasi. Lakini kuwa makini, damu inapogeuka na kuanza kutoka kwa matone makubwa, ni ishara kuwa kuna jambo lisilokuwa sawa. Enda ukaguliwe kwenye kituo cha matibabu.

Soma Pia: Vitu 6 Vinavyo Fanya Safari Ya Ujauzito Iwe Rahisi Zaidi

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Sababu 5 Za Kutoka Damu Wakati Wa Mimba Changa
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it