Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol

2 min read
Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti SolKutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol

Kutumia wimbo wenu ilikuwa ishara ya mapenzi raila odinga alisema katika tangazo kupitia kwa chama chake cha kisiasa.

Mitandao ya kijamii imekuwa na mjadala moto kuhusu wanasiasa na wasanii. Haya ni baada ya Azimio la Umoja ambacho ni chama cha kisiasa nchini Kenya kucheza wimbo wa Sauti Sol katika kampeni zao. Sauti Sol ni mojawapo ya boy band maarufu zaidi na duniani kote. Wanafahamika na kusifika kwa nyimbo za maana na za kupendeza wanazoimba kuwatumbuiza watu. Nyimbo kama Suzanna, Rhumba Japani, Lazizi, Short N Sweet na kadhalika.

Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol

Kikundi cha Sauti Sol

Kikundi kinachotukuka, kuheshimika na kuzungumziwa kwa hadhi kwani kwa muda mrefu kimefanya bendera ya nchi ya Kenya kupepea duniani kote wanapoenda kuimba.

Sauti Sol walivunja kimya chao kwa kuzungumzia hisia zao baada ya chama cha Azimio la Umoja kutumia wimbo wao katika kampeni bila kulipia leseni. Walitishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya chama hiki.

Muwania kiti cha urais wa chama cha Azimio la Umoja, mmoja Raila Odinga kupitia kwa chama chake cha Orange Democratic Movement (ODM), alisema kuwa, kucheza wimbo wao katika kampeni ilikuwa ishara ya mapenzi.

Katika ujumbe wake kwenye Twitter Raila Odinga aliandika, “Tungependa kuiashiria timu yetu ya muziki inayosherehekewa @sautisol kuwa tunawapenda na kuthamini muziki wao sana. Kikundi hiki kimebeba bendera yetu juu sana duniani kote na kila mwanaKenya anathamini jambo hili. Kucheza wimbo wao jana ilikuwa ishara ya kupenda kazi yao.”

Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol

Siku ya Jumatatu tarehe 16, 2022, chama cha Azimio la Umoja kilicheza wimbo wa Sauti Sol wa Extravaganza walipokuwa wakitangaza naibu wa rais wa chama chao katika kampeni za kirais. Hatukukipatia chama chochote kibali cha kutumia wimbo wetu katika uvumbuzi wa mgombeaji kiti cha naibu rais katika chama chao. Sauti Sol walisema.

Sauti Sol waliashiria kuwa utumizi wa wimbo wao bila kibali chao ni kuenda dhidi ya hakimiliki kama ilivyoandikwa kwenye Section 35, CAP 170 ya hakimiliki za Kenya.

Kikundi hiki kilijitenga na chama chochote cha kisiasa, Azimilio la Umoja na vikundi vingine vya kisiasa na wanasiasa wowote nchini.

Chanzo: Africaparent

Soma Pia:Mulamwah Kwenye Redio: Mulamwah Apata Kazi Milele FM

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Lifestyle
  • /
  • Kutumia Wimbo Wenu Ilikuwa Ishara Ya Mapenzi, Raila Odinga Aliwaambia Sauti Sol
Share:
  • Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

    Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

  • Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

    Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

  • Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

    Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

  • Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

    Sababu 7 Kwa Nini Watu Wanaogopa Ndoa Siku Hizi

  • Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

    Zari Hassan Amewasili Nchini Kenya Ambapo Anavumbua Nyumba Mpya

  • Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

    Lori Harvey na Michael B. Jordan Wametengana Baada ya Kuwa Pamoja Kwa Mwaka Mmoja

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it