Kuwa na urafiki na watoto wako kunawasaidia kufahamu kuwa wanaweza kueleza chochote kinacho wasumbua bila hofu ya kukemewa. Tazama baadhi ya mbinu ambazo wazazi wanaweza tumia kuboresha urafiki na watoto wao.
- Wapatie nafasi ya kufanya wanachotaka huku ukiwa rekebisha kwa mapenzi

Kuwa na mipaka yenye afya ni mojawapo ya mambo muhimu zaidi katika ulezi. Ikiwa wazazi wanawapatia nafasi, pia mama na baba wanapata chanya zaidi cha kufanya mambo yao na kutimiza malengo yao.
Unapo jaribu kuwasaidia jinsi ambavyo ungependa kusaidiwa ulipokuwa mtoto, hakuna uwiano. Tunakosa kuungana na watoto wetu na kutowasaidia wanavyostahili. Badala ya kugundua utu wao na wanachotaka, tunajaribu kuwatengeneza kwa picha tunayoitaka. Na sio sawa. Watoto wanahisi kuwa wazazi wao hawawaelewi.
2. Jinsi ya kuwa mzazi bora
Unafanya tofauti kwa kumsikiliza mtoto wako. Ni muhimu kuwaonyesha watoto wako kuwa unawaelewa, wanachofanya na wanachosema. Usikatae kila kitu wanachokifanya, huku kutafanya wahisi kuwa hakuna kitu wanachokifanya kinakubalika. wasaidie kuona mambo kutoka upande mwingine. Ikiwa mtoto wako anapenda kulia ovyo, tafuta njia ya kumtuliza kisha uzungumze naye.
3. Usiwakemee watoto
Unapohisi kuwa una filisika kimawazo, fahamu nguvu zako na ukubali nyanja usizokuwa mzuri katika. Usijishinikize kuwa bila doa, na usiwe mgumu sana kwako. Fahamu mahitaji yao ni yapi bila kuwalazimisha wachukue hiari ambayo ungechukua kama mtoto. Wafunze watoto wako kufahamu nyanja zao za ubora na wasizokuwa bora katika. Waulize, je, kuna jambo ambalo ungependa kujua sasa hivi?
4. Kuwa mkarimu

Kujitunza ni muhimu kwa wazazi. Wakati ambapo kuwafunza watoto kuwa wakarimu ni muhimu, wazazi wanapaswa kuongoza kwa mfano. Zaidi ya kuwa mkarimu kwa watu wengine, ni muhimu kwa wazazi kuwa wakarimu kwa wao wenyewe. Tenga muda kufanya mambo ambayo yalikufurahisha hapo awali kabla ya kuwa mzazi.
5. Wape fursa ya kufanya uamuzi
Kosa ambalo wazazi wengi hufanya ni kuwafanyia watoto wao uamuzi katika kila kitu. Unapompatia mtoto fursa ya kujiamulia anachotaka, unaboresha kujiamini kwake na kufahamu kuwa unamwamini. Anapokuwa mkubwa, hatakuwa na tatizo la kufanya uamuzi wala kungoja watu wengine wamfanyie uamuzi. Ni muhimu sana kwa wazazi kufahamu umuhimu wa kutowafanyia watoto uamuzi, badala yake, kuwasaidia wanapokwama. Kwa kufanya hivi, kunasaidia kuwa na urafiki na watoto wako na imani zaidi.
Soma Pia: Jukumu La Baba Katika Familia Na Maisha Ya Watoto Wake