Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Njia Tofauti Za Kuzuia Kupata Mimba Unaponyonyesha

3 min read
Njia Tofauti Za Kuzuia Kupata Mimba UnaponyonyeshaNjia Tofauti Za Kuzuia Kupata Mimba Unaponyonyesha

Kuna imani nyingi zinazo zingira kunyonyesha kama njia ya uzazi wa mpango na kuzuia mimba mama anaponyonyesha. Je, ni kweli? Tuna zungumzia haya kwa kina!

Mwanamke anapokuwa na mimba, huenda akawa ameambiwa mara nyingi kuwa kunyonyesha ni aina ya uzazi wa mpango. Je, imani hii ni kweli? Tuna dadisi zaidi kuhusu kunyonyesha kama njia ya uzazi wa mpango na kuzuia mimba mama anaponyonyesha.

Mama anaponyonyesha peke yake bila kumlisha mtoto kitu kingine na kumnyonyesha kwa muda mrefu, nafasi zake za kupata mimba zinapungua. Mbinu hii kama  njia ya kupanga uzazi huwa na ufanisi zaidi katika miezi ya kwanza sita baada ya kujifungua. Ili kufuzu, mama anastahili kunyonyesha mtoto baada ya kila masaa manne.

Ni vyema wakati wote kuzungumza na daktari wako baada ya kujifungua kuhusu njia bora za kuzuia mimba unaponyonyesha. Kuna baadhi ya njia za uzazi wa mpango zinazo punguza utoaji wa maziwa na kuathiri lishe ya mtoto.

Tazama baadhi ya njia za uzazi wa mpango unaponyonyesha

  • Kutumia mipira ya kondomu

kuzuia mimba mama anaponyonyesha

Mipira ya kondomu huwa salama kwa mama na ina uwezo wa kukinga dhidi ya kupata maambukizi na mimba kwa asilimia 98. Isipokuwa pale mpira unapovunjika katika tendo. Inapotumika ipasavyo, wanandoa hawana shaka ya kupata maambukizi ama mimba. Kuna aina tofauti ya kondomu, kuna za kike na za kiume na zilizo na lubricant na zile zisizo kuwa nayo.

  • IUD

kuzuia mimba mama anaponyonyesha

Zinafahamika kuwa na ubora wa asilimia 99 ya kukinga dhidi ya kupata mimba. Kuna aina mbili ya IUD, iliyo na homoni na isiyo na homoni. IUD zilizo na homoni huwa na kichocheo cha progesterone kinachofanya kamasi kutoka kwa kizazi kuwa kinene na kuzuia manii kutofika kwenye uterasi. Njia hii ya kupanga uzazi ni bora kwa wanawake walio na mchumba mmoja wa kimapenzi. Kuwa na wachumba wengi kunawaweka katika hatari ya kuugua maambukizi ya kingono. IUD zenye homoni humfanya mwanamke kukosa kupata hedhi yake ama ikawa nyepesi zaidi.

  • Tembe

athari hasi za tembe za kupanga uzazi

Tembe za jadi huwa na mchanganyiko wa vichocheo vya estrogen na progestin. Homoni ya estrogen inasemekana kuathiri utoaji wa maziwa na kumfanya mama kutoa maziwa iliyopunguka na kunyonyesha kwa muda mfupi zaidi.

Kuna tembe zilizo na homoni ya progestin peke yake na huwa bora zaidi kwani haziathiri utoaji wa maziwa. Mwanamke anapofanya uamuzi wa kupata mimba tena, huenda rutuba ikarudi punde tu anapokoma kutumia tembe hizi. Hata hivyo, ni vyema kuwasiliana na daktari wake.

  • Implant

Ina pachikwa chini ya mkono baada ya upasuaji mdogo. Ina uwezo wa kuzuia mimba kwa miaka minne. Implant zina homoni ya progestin inayo saidia kuzuia ovari kuachilia mayai. Ni vigumu mimba kufanyika pasipo na yai.

Mama anapaswa kuzungumza na daktari kuhusu njia za kuzuia mimba mama anaponyonyesha kabla ya kwenda nyumbani baada ya kujifungua.

Soma Pia: Jinsi Ya Kupanga Uzazi Kwa Kutumia Mbinu Za Kiasili!

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Relationship & Sex
  • /
  • Njia Tofauti Za Kuzuia Kupata Mimba Unaponyonyesha
Share:
  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

  • Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

    Imani za Kuchumbiana Zisizo za Kweli Unazostahili Kujua

  • Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

    Koma kufanya Hivi Ili Kuboresha Maisha Yako ya Kingono

  • Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

    Sababu 3 Kwa Nini Unapaswa Kuongeza Mara Unazofanya Mapenzi Kwa Siku

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it