Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Kweli Kuhusu Endometriosis: Imani Kuhusu Endometriosis Na Iwapo Ni Kweli Ama La

3 min read
Kweli Kuhusu Endometriosis: Imani Kuhusu Endometriosis Na Iwapo Ni Kweli Ama LaKweli Kuhusu Endometriosis: Imani Kuhusu Endometriosis Na Iwapo Ni Kweli Ama La

Je, endometriosis ina tiba? Makala haya yanazungumzia kweli kuhusu endometriosis, vyanzo vyake na iwapo mama anaweza kupata mimba.

Kwa muda mrefu sasa, kumekuwa na imani zisizo za kweli kuhusu endometriosis. Tunafahamu zaidi kuhusu hali hii na jinsi inavyoathiri mimba.

Endometriosis ni hali sugu ambapo tishu zinazokuwa upande wandani wa uterasi hukua ndani ya fuko la uzazi. Na kumfanya mwanamke ahisi uchungu mwingi wakati wa tendo la mapenzi, hedhi ama anapoenda msalani. Hali hii katika wanawake huwafanya kuhisi uchovu mwingi, kuhisi kutapika, kusababisha matatizo ya uzalishaji ama hata kupata matatizo na afya yao ya kiakili.

Karibu asilimia 10 ya wanawake duniani kote walio katika miaka yao ya kujifungua hutatizika kutokana na endometriosis.

Sababu zinazoongeza hatari ya kupata endometriosis

kweli kuhusu endometriosis

  • Kuwa na mama aliye na hali ya endometriosis
  • Kuwa na vipindi vya hedhi vyenye mzunguko wa siku chache kuliko 27
  • Kuanzia vipindi vya hedhi kabla ya umri wa miaka 11
  • Kuwa na vipindi vya hedhi vichungu, kuvuja damu nyingi na kipindi kudumu zaidi ya wiki moja

Hakuna matibabu ya hali ya endometriosis. Tuna angazia baadhi ya imani zilizoko kuhusu hali hii na iwapo ni kweli ama la.

Kweli kuhusu endometriosis

1.Vipindi vya hedhi huwa chungu na vyenye damu nyingi

Asilimia kubwa ya wanawake huhisi uchungu wakati wa hedhi, lakini uchungu wa kupindukia katika hedhi huenda ikawa ishara ya endometriosis.

Hata kama vipindi vya hedhi kwa waliokuwa na endometriosis huwa vikali na vichungu lakini sio wakati wote. Kuna baadhi ya wanawake hata baada ya kuwa na endometriosis huwa na vipindi vyepesi na visivyo na uchungu mwingi.

2. Endometriosis huathiri sehemu za uzalishaji za kike

Vidonda vya endometriosis hukua kwenye sehemu ya tumbo ya chini na pelviki. Hata kama vidonda hivi vinaweza kupatikana katika sehemu tofauti mwilini. Ukweli ni kuwa endometriosis hujipandikiza kwenye upande wa ndani wa tumbo inayofahamika kama peritoneum na kusababisha uchungu. Mbali na sehemu hii, vidonda hivi vinaweza kupatikana kwenye mafua na ubongo.

kweli kuhusu endometriosis

3. Mimba huponya endometriosis

Mimba kamwe haiponyi endometriosis. Baadhi ya wanawake hushuhudia kupunguka kwa uchungu wanapokuwa na mimba wala sio wote. Mimba husababisha viwango vya homoni mwilini kubadilika na kufanya watu tofauti kuwa na viwango tofauti vya uchungu baada ya kujifungua.

4. Mwanamke aliye na endometriosis hawezi kujifungua

Asilimia 35-50 ya wanawake walio na endometriosis hutatizika kujifungua, lakini hali hii haimaanishi kuwa mwanamke hawezi kujifungua. Wanawake wanaokuwa na hali hii na wanataka kubeba mimba wanashauriwa kufanya kazi kwa karibu na madaktari ili kuhakikisha kuwa wana nafasi za juu kushika mimba.

5. Kutoa mimba husababisha endometriosis

Chanzo cha endometriosis kingali hakijadhibitika. Lakini kutoa mimba sio chanzo cha endometriosis katika mimba.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Vidokezo 5 Vya Kupata Mimba: Kuongeza Nafasi Za Kupata Mtoto Kirahisi

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Kweli Kuhusu Endometriosis: Imani Kuhusu Endometriosis Na Iwapo Ni Kweli Ama La
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it