Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Je, Kuna Madhara Hasi Ya Kufanya Mapenzi Katika Mimba Kwa Mama Mjamzito

2 min read
Je, Kuna Madhara Hasi Ya Kufanya Mapenzi Katika Mimba Kwa Mama MjamzitoJe, Kuna Madhara Hasi Ya Kufanya Mapenzi Katika Mimba Kwa Mama Mjamzito

Mama aliye na historia ya kupoteza mimba ako katika hatari ya juu ya kupoteza mimba tena na ni muhimu kwake kujadiliana kuhusu tendo la ndoa katika mimba na daktari wake.

Baada ya vipindi vingi chumbani cha kulala kujaribu kupata mimba, huenda hamu ya mwanamke ya kitendo cha mapenzi kufifia baada ya kushika mima. Ni jambo la kawaida na linalowafanyikia wanawake wengi na pia linaeleweka. Je, ni salama? Madhara ya kufanya mapenzi kwa mama mjamzito ni yapi? Kuna uwezekano wa kufanya mapenzi bila kumwumiza mama na fetusi.

Madhara ya kufanya mapenzi kwa mama mjamzito

madhara ya kufanya mapenzi kwa mama mjamzito

Kufanya tendo la katika mimba ni salama kwa mama na mtoto anayekua tumboni kwani amelindwa na amniotic fluid. Hata hivyo, ni vyema kwa mama kuzungumza kuhusu ngono katika mimba na daktari wake kuhakikisha kuwa hatakuwa na matatizo.

Mama aliye na historia ya kupoteza mimba ako katika hatari ya juu ya kupoteza mimba tena na ni muhimu kwake kujadiliana kuhusu tendo la ndoa katika mimba na daktari wake. Kwa visa kama hivi, daktari anaweza kumshauri mama kujitenga na tendo la ndoa hasa katika miezi ya kwanza.

Hata kama mtoto analindwa na amniotic fluid, ni muhimu kwa mama mjamzito kuwa makini kwani maambukizi ya kingono yanahatarisha maisha yake. Mchumba wake anapaswa kujitenga na kuwa na wapenzi nje ya uhusiano wao.

Wakati ambapo tendo la ndoa sio salama katika mimba

  • Mama anapokuwa na historia ya kupoteza mimba
  • Mama mwenye historia ya kujifungua kabla ya wakati
  • Maumivu ya tumbo yasiyoeleweka
  • Gunia la amniotic kuvuja
  • Kuwa na mimba ya zaidi ya mtoto mmoja

Manufaa ya kufanya mapenzi katika ujauzito

madhara ya kufanya mapenzi kwa mama mjamzito

Wapenzi wanapata nafasi ya kutangamana. Ujauzito huwa kipindi chenye panda shuke nyingi kwa wanandoa wote wawili. Kupata muda wa kudumisha utangamano wao ni muhimu katika kipindi hiki.

Kupunguza uchungu na kukosa starehe. Mama hushuhudia uchungu katika mimba, kama vile kuumwa na mgongo, kufanya mapenzi kunasaidia kupunguza maumivu haya.

Kuboresha hisia zake. Mimba humfanya mama awe na hisia nyingi tofauti

Kumsaidia mama kulala vyema. Mapenzi katika mimba humsaidia mama kulala vyema na pia kutoa homoni za kumfanya ahisi vyema.

Mitindo salama ya kufanya mapenzi katika ujauzito

madhara ya kufanya mapenzi kwa mama mjamzito

Katika mimba, ni muhimu kwa wanandoa kuzingatia mitindo ambayo ni salama kwa mama. Isiyomshinikiza wala kumfanya ahisi maumivu kwenye tumbo. Starehe kwake ni muhimu katika kipindi hiki. Ikiwa mtindo fulani mliokuwa mnaupenda hapo awali unamfanya mama akose starehe, ni muhimu kuuweka kando kwa sasa.

Chanzo: WebMD

Soma Pia: Njia Tofauti Ambazo Wanandoa Wanaweza Kufurahia Ngono Katika Mimba!

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Je, Kuna Madhara Hasi Ya Kufanya Mapenzi Katika Mimba Kwa Mama Mjamzito
Share:
  • Majina 50 ya Wasichana ya Kipekee na Yanayopendeza Zaidi

    Majina 50 ya Wasichana ya Kipekee na Yanayopendeza Zaidi

  • Sababu 3 Kuu Za Maumivu Ya Tumbo Katika Mimba

    Sababu 3 Kuu Za Maumivu Ya Tumbo Katika Mimba

  • Ukweli Kuhusu Kufanya Mapenzi Ukiwa Na Mimba

    Ukweli Kuhusu Kufanya Mapenzi Ukiwa Na Mimba

  • Majina 50 ya Wasichana ya Kipekee na Yanayopendeza Zaidi

    Majina 50 ya Wasichana ya Kipekee na Yanayopendeza Zaidi

  • Sababu 3 Kuu Za Maumivu Ya Tumbo Katika Mimba

    Sababu 3 Kuu Za Maumivu Ya Tumbo Katika Mimba

  • Ukweli Kuhusu Kufanya Mapenzi Ukiwa Na Mimba

    Ukweli Kuhusu Kufanya Mapenzi Ukiwa Na Mimba

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it