Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Je, Kuna Madhara Ya Kufanya Mapenzi Kwa Mjamzito?

2 min read
Je, Kuna Madhara Ya Kufanya Mapenzi Kwa Mjamzito?Je, Kuna Madhara Ya Kufanya Mapenzi Kwa Mjamzito?

Hakuna madhara makuu ya kufanya mapenzi kwa mjamzito ila kunapokuwa na ushauri wa daktari.

Kwa kawaida kina mama wengi wanaposhika mimba huegemea kutofanya mapenzi. Hii ni kwa kuwa wengi huwa na hofu kuwa inaweza kuathiri mtoto. Ila hii hofu ina msingi wowote na kuna madhara ya kufanya mapenzi kwa mjamzito?

Kuna Madhara Ya Kufanya Mapenzi Kwa Mjamzito?

madhara ya kufanya mapenzi kwa mjamzito

Kabla ya kuangazia iwapo kuna madhara ya kufanya mapenzi kwa mjamzito ni vyema kuelewa tumbo la uzazi. Mtoto huchukua nafasi kwenye uterasi.  Hapa huwa amezingirwa na tabaka linalojulikana kama amniotic fluid.  Hili tabaka humkinga mtoto kutokana na ajali. Pia humkinga mtoto kutokana na maambukizi.

Pili, uterasi na njia ya uzazi huwa imetenganishwa na mlango unaojulikana  kama servix. Huu mlango huwa kizuizi kwa chochote kinachoweza kujipenyeza kwenye uterasi na kumdhuru mtoto. Hizi kinga mbili huwa dhabiti na tosha kumsetiri mtoto kutokana na ajali ama maambukizi.

Kina mama wengi huwa na hofu kuwa kufanya mapenzi kunaweza kuathiri mtoto lakini kama tumevyoona hapo awali ni kuwa hilo sio sawa. Kwa hivyo inawezekana kwa mama mjamzito kujihusisha na kufanya  mapenzi kipindi chote cha ujauzito hadi pale atakapojifungua bila hofu ya kumjeruhi mtoto.

madhara ya kufanya mapenzi kwa mjamzito

Ila, kuna dalili ambazo zinaweza kuashiria hali ya hatari? Hizi ni kama vile:

  • Una historia ya mimba kuharibika. Iwapo una historia ya kuharibika kwa mimba kufanya mapenzi wakati wa ujauzito kunaweza kuwa sio wazo nzuri. Hii ni kwa kuwa inaweza kuhatarisha ama kuongeza nafasi zako za kumpoteza mtoto
  • Unavunja damu. Iwapo utagundua kwamba unavunja damu wakati wa kufanya mapenzi ni vyema kwanza kusitisha na kumwona daktari wako. Inaweza kuwa sio jambo la dharura ila kuondoa shaka ni vyema kupata ushauri
  • Iwapo unahisi uchungu wakati wa kufanya mapenzi. Jambo lingine la kuzingatia ni kama unahisi uchungu wakati wa kufanya mapenzi. Hii inaweza kuwa ishara ya maambukizi. Kwanza pata ushauri wa daktari  kwani maambukizi yanaweza kumwathiri mtoto ama njia ya uzazi
  • Mabadiliko ya homoni. Kina mama huwa tofauti, kuna wale huwa na hamu na ya mapenzi ilihali wengine hawapendelei kabisa. Hii hutokana na mabadiliko ya homoni kipindi cha ujauzito. Ni vyema mama kuelewa kuwa hii huwa ni sawa kabisa na hakuna jambo la kuhofia
  • Iwapo daktari wako ameshauri hivyo. Kama baada ya uchunguzi daktari atapendekeza kusitisha kufanya mapenzi  ni vyema kufuata ushauri wa daktari

Ni wazi kuwa madhara ya kufanya mapenzi kwa mjamzito sio makuu ila kunapokuwa na ushauri wa daktari. Jambo la msingi ni kuzingatia staili salama wakati wa kufanya mapenzi ili mtoto asiumie.

Soma Pia: Maswali 7 Maarufu Kuhusu Ngono Katika Mimba

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Je, Kuna Madhara Ya Kufanya Mapenzi Kwa Mjamzito?
Share:
  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

  • Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

    Makosa Ambayo Wanawake Wajawazito Hufanya

  • Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

    Vidokezo vya Ujauzito Wenye Afya kwa Mama Mjamzito

  • Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

    Chakula Bora cha Kujifungua Mtoto Mrembo

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it