Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Usingizi Wa Kutosha Unashauriwa, Ila, Je, Kuna Madhara Ya Kulala Sana?

3 min read
Usingizi Wa Kutosha Unashauriwa, Ila, Je, Kuna Madhara Ya Kulala Sana?Usingizi Wa Kutosha Unashauriwa, Ila, Je, Kuna Madhara Ya Kulala Sana?

Madhara ya kulala sana kwa zaidi ya saa 9 na zaidi ya dakika 90 wakati wa mchana huongeza hatari ya mtu kupigwa  na kiharusi.

Kwa kawaida usingizi huwa na manufaa kadhaa kwa binadamu. Lakini kama kila kilicho na  manufaa pia huwa na madhara. Madhara ya kulala sana huwa yepi?

Madhara Ya Kulala Sana

madhara ya kulala sana

Imebainika kutokana na utafiti kuwa, kulala kwa zaidi ya saa 9 na zaidi ya dakika 90 wakati wa mchana huongeza hatari ya mtu kupigwa  na kiharusi. Huo utafiti ulionyesha kuwa wale ambao hawakuwa na tatizo la kupooza  au shida nyingine kubwa za kiafya  ni wale wanaolala  chini ya saa nane.

Pia hatari ya kupooza ilionekana  kuongezeka  kwa asilimia 25 kwa watu ambao walipumzika kwa zaidi ya dakika 90 mchana.  Wale ambao hulala kwa muda mrefu usiku na kulala muda mrefu wakati wa mchana wana uwezekano wa asilimia 85 ya kupatwa na hali ya kupooza mwili.

Wakati uchunguzi huo ukifanyika,  watu walichunguzwa kwa muda wa miaka sita na 1557 kati yao walipooza kwenye harakati za kuchunguzwa. Kwa kawaida mtu mzima  mwenye umri wa kati ya miaka 18-64 anahitaji saa 7-9 za kulala kila usiku.

Sababu za kuwa na usingizi mwingi

Kuna aina mbili za usingizi usioisha zinazofahamika kama aina ya msingi na ya sekondari .  Aina ya msingi hutokea pale ambapo hakuna shida nyingine yoyote ndani ya mwili inayofahamika baada ya vipimo mbalimbali.  Chanzo chake hudhaniwa kuwa  madhaifu ndani ya  mfumo wa umeme.

Aina ya sekondari ni ule usingizi usioisha na sababu zake zinafahamika. Dalili kuu za usingizi usioisha ni kupata uchovu mkali wa mwili unaodumu, kusinzia sinzia na kushindwa kuamka kwa wakati kutokana  na kuwa na  vipindi virefu vya kulala. Dalili zingine ni pamoja na kuishiwa na nguvu, kuwa mkali, kuwa na hofu , Kukosa hamu ya chakula, kupoteza kumbukumbu, kutojihisi kufanya chochote.

madhara ya kulala sana

Kuna sababu nyingi ambazo huchangia usingizi usioisha aina ya sekondari. Hizi ni kama vile:

  • Magonjwa ya usingizi kama narcolepsy na sleep apnea
  • Kutolala vyema wakati wa usiku
  • Kuwa na uzani mkubwa
  • Matumizi ya pombe
  • Majeraha ndani ya kichwa au magonjwa ya  mfumo wa neva
  • Matumizi ya dawa Jamii ya tranquilizers
  • Msongo wa mawazo

Baadhi ya matatizo ya usingizi kupita kiasi hayawezi kuzuilika ila ni vyema kujikanga na vihatarishi.

  • Kufanya mazingira unayolala kuwa rafiki
  • Kupunguza matumizi ya pombe na kahawa
  • Kuacha kutumia dawa zinazosababisha kusinzia
  • Kutofanya kazi hadi usiku wa manane
  • Kutokula mlo mzito wakati wa kulala

Kwa kawaida wengi hufahamu umuhimu wa usingizi ila wachache huelewa madhara ya kulala sana. Kupooza ni athari moja inayoongaza  na inayotokana na kulala sana.

Chanzo: WebMd

Soma Pia:Manufaa 3 Ya Kumkanda Mtoto Kwa Mtoto Na Mama

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Health
  • /
  • Usingizi Wa Kutosha Unashauriwa, Ila, Je, Kuna Madhara Ya Kulala Sana?
Share:
  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

  • Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

    Je, Kiamsha Kinywa Kina Manufaa Mwilini?

  • Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

    Vyanzo 5 vya Kuhisi Uvimbe na Maumivu ya Tumbo

  • Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

    Dalili za Ugumba Kwa Wanaume na Jinsi ya Kujikinga Dhidi ya Hali Hii

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2023 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it