Africaparent Logo
Africaparent Logo
EnglishSwahili
  • COVID-19
  • Becoming a Mama
  • Ages & Stages
  • Parenting
  • Health
  • Feeding & Nutrition

Madhara Ya Mjamzito Kutokula Kwa Afya Yake Na Ya Fetusi

2 min read
Madhara Ya Mjamzito Kutokula Kwa Afya Yake Na Ya FetusiMadhara Ya Mjamzito Kutokula Kwa Afya Yake Na Ya Fetusi

Madhara ya kutokula kwa mjamzito huongezeka kulingana na jinsi mama anavyokaa kabla ya kula tena baada ya mlo wake wa mwisho.

Kukosa lishe tosha na bora katika ujauzito huwa na madhara zaidi na sio kwa mtoto peke yake. Afya ya mama itadhoofika huku mwili unapozidi kusitiri ukuaji wa fetusi tumboni. Kwani mwili wa mama hauna virutubisho tosha kuhimiza ukuaji bora. Madhara ya kutokula kwa mjamzito huongezeka kulingana na jinsi mama anavyokaa kabla ya kula tena baada ya mlo wake wa mwisho. Kukosa mlo mara kwa mara sio vibaya ila kukaa muda mrefu bila kula kutakuwa na athari nyingi hasi.

Madhara ya mjamzito kutokula

madhara ya mjamzito kuto kula

Matatizo ya kuzaliwa

Kukosa virutubisho muhimu mwilini kunasababisha matatizo ya kuzaliwa ama ulemavu. Mama asipokula vyema anapokuwa na mimba, mtoto atakosa virutubisho muhimu katika ukuaji wake. Kukosa kalisi tosha husababisha kuzaliwa kwa mtoto mwenye matatizo ya kiafya kama mifupa isiyo na nguvu. Mama anastahili kula vyakula vilivyo na kalisi nyingi kama mchicha, bidhaa za maziwa na samaki wa salmon.

Kujifungua kabla ya wakati

Kwa mwanamke anayetatizika zaidi na kutokula, huenda hali hiyo ikamfanya ajifungue kabla ya wakati. Mama pia ako katika hatari ya kupoteza mimba ama kujifungua mtoto aliyefariki. Iwapo mama atabeba mimba hadi trimesta ya mwisho, huenda akazaliwa akiwa na matatizo ya mafua ama moyo.

Afya ya mama kudhoofika

Madhara Ya Mjamzito Kutokula Kwa Afya Yake Na Ya Fetusi

Mama asipokula apasavyo, ako katika hatari ya kukosa damu tosha mwilini. Anapokuwa na mimba, anastahili kula chakula tosha cha kuhimiza ukuaji wake na wa mtoto, kukosa kufanya hivi, kutasababisha kudhoofika kwa afya yake kwani mtoto anatumia virutubisho vyake kwa ukuaji wake. Mama anapokuwa na anaemia, atakosa nishati tosha mwilini na huenda akapata kizunguzungu.

Mama kutatizika kunyonyesha

Kuongeza uzito katika ujauzito humsaidia mama wakati wa kunyonyesha baada ya kujifungua. Wanawake wanaotatizika kukula wanapokuwa na mimba hutatizika kupata maziwa tosha ya mtoto. Mtoto hutegemea maziwa ya mama kupata vitamini muhimu katika ukuaji wake. Mama asipopata maziwa tosha ya mtoto, afya ya mtoto itaathirika.

Mama anapogundua kuwa anatatizika na kula anapokuwa na mimba, ni vyema kumweleza daktari wake ili ampe dawa zitakazo msaidia na hali yake.

Chanzo: Healthline

Soma Pia: Afya Yako Baada Ya Kupoteza Mimba, Fanya Haya!

Got a parenting concern? Read articles or ask away and get instant answers on our app. Download theAsianparent Community on iOS or Android now!

img
Written by

Risper Nyakio

  • Home
  • /
  • Pregnancy
  • /
  • Madhara Ya Mjamzito Kutokula Kwa Afya Yake Na Ya Fetusi
Share:
  • Je, Kulala Kwa Mgongo Katika Mimba Kuna Athari Hasi Kwa Mama na Mtoto?

    Je, Kulala Kwa Mgongo Katika Mimba Kuna Athari Hasi Kwa Mama na Mtoto?

  • Matatizo Katika Trimesta ya Tatu Utakayoshuhudia

    Matatizo Katika Trimesta ya Tatu Utakayoshuhudia

  • Je, Anita Nderu Ana Mimba?

    Je, Anita Nderu Ana Mimba?

  • Je, Kulala Kwa Mgongo Katika Mimba Kuna Athari Hasi Kwa Mama na Mtoto?

    Je, Kulala Kwa Mgongo Katika Mimba Kuna Athari Hasi Kwa Mama na Mtoto?

  • Matatizo Katika Trimesta ya Tatu Utakayoshuhudia

    Matatizo Katika Trimesta ya Tatu Utakayoshuhudia

  • Je, Anita Nderu Ana Mimba?

    Je, Anita Nderu Ana Mimba?

Get advice on your pregnancy and growing baby. Sign up for our newsletter
  • Becoming a Mama
    • Pregnancy
    • Delivery
    • Losing a Baby
  • Ages & Stages
    • Baby
    • Toddler
    • Kids
  • Parenting
    • News
    • Relationship & Sex
    • Parent's Guide
  • Health
    • Allergies & Conditions
    • Vaccinations
    • Diseases-Injuries
  • Feeding & Nutrition
    • Breastfeeding & Formula
    • Latching & Concerns
    • Weaning
  • More
    • TAP Community
    • Advertise With Us
    • Contact Us
    • Become a Contributor


  • Singapore flag Singapore
  • Thailand flag Thailand
  • Indonesia flag Indonesia
  • Philippines flag Philippines
  • Malaysia flag Malaysia
  • Sri-Lanka flag Sri Lanka
  • India flag India
  • Vietnam flag Vietnam
  • Australia flag Australia
  • Japan flag Japan
  • Nigeria flag Nigeria
  • Kenya flag Kenya
© Copyright Africaparent.com 2022 Tickled Media Pte Ltd. All rights reserved
About Us|Team|Privacy Policy|Terms of Use |Sitemap HTML

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it

We use cookies to ensure you get the best experience. Learn MoreOk, Got it